Matamko ya (baadhi) waislam (Dar na Mwanza)

Matamko ya (baadhi) waislam (Dar na Mwanza)

Status
Not open for further replies.
sorry to say this, usilazimishe watu wote waelewe ulivyoelewa wewe yawezekana wewe hujaelewa?

Sikulazimishi, ila na uhakika hujasoma tamko, maana hoja hujibiwa kwa hoja siyo emotions na kukurupuka
 
KUTUMIKA KAMA GOGO LA CHOONI KUBAYA SANA.
Waislamu fungueni macho you are being used!!!!!

Ndiyo maana mmechapwa kule arusha, sasa mnapiga makelele hatulalali. Msiige waislamu, waislamu majabari hawaogopi kufa. Na kama mngeuwawa kama walivyokuwa wanauwawa waislamu katika miaka ya nyuma si ingekuwa balaa. Msirudie tena watoto wazuri eehh, maana mkirudia tena mtachapwa mtoke vibogoyo wote.
 
@fundo mchundo.una matatizo ya msingi.ishu nikwamba tuliwafukuza wakoloni wote wazungu na waarabu ili tujitawale.lakin wazungu waliendelea na wanaendelea kutuibia kwa mgongo wa kanisa hata wewe unajua lakin hutaki kukubali tu.
 
Ndugu zetu hawa hawabebeki hata kwa guta!!

Waislam wanalilia mfumo kristo Masheikh wanasema Maaskofu walinyamaza kimya mauaji ya Mwembechai na kutoa karipio kwa CUF walipouwawa waandamanaji kupinga matokeo na kudai katiba mpya 2001. Wasema kwakuwa mgombea wao Padri Slaa ameanguka wamekuwa wakali kama pilipili wamefikia hadi kuwafuta uumini baadhi ya waumini wa kikristo Sumbawanga kwakuwa walienda kinyume na matakwa ya kanisa kwenye uchaguzi wa mwaka jana. Habari kubwa kwangu kumbe wenzetu mnaweza kupokonywa ukristo kwa barua? Kisha wakasema "TAMKO LA WAISLAMU DHIDI YA KAULI ZA MAASKOFU Waislamu wameiomba serikali kujiunga na OIC kama njia mojawapo itakayowezesha nchi yetu kupata misaada itakayotumika kuinua hali za Waislamu ambao wameachwa nyuma sana katika elimu na uchumi. Makanisa yote kwa kauli moja yamepinga kwa nguvu zao zote pendekezo hilo. Sababu ya kupinga kwao ni kuwa mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa Waislamu wanadhoofishwa katika kila hali, na ni makosa makubwa kuwaimarisha kiuchumi au kielimu maadui hao. Serikali ilipofanya utafiti wake wa kina ikajiridhisha kuwa kujiunga na OIC kuna manufaa na hakuna madhara yoyote. Na Mh. Bernard Membe alitamka hilo Bungeni. Mara akaitwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Cardinali Pengo na kukumbushwa mkakati wa kuwadhoofisha Waislamu. Msimamo wa serikali ukabadilika. Lakini propaganda za kuwazuga Waislamu zinasema Watanzania wote ni kitu kimoja na nchi hii haina ubaguzi!"
 
Waislam wanalilia mfumo kristo Masheikh wanasema Maaskofu walinyamaza kimya mauaji ya Mwembechai na kutoa karipio kwa CUF walipouwawa waandamanaji kupinga matokeo na kudai katiba mpya 2001.
Kwani walilazimika kutoa tamko? Wahindi walitoa tamko? Rasta walitoa tamko? mabudhist walitoa tamko? Mabaha'i walitoa tamko? Mbona hamuwasemi? Mnataka kutuambia kuwa roho zenu zingesuuzwa tu pale ambapo Kadinali Pengo angetoa tamko? Hauoni kuwa huku ni kujidhalilisha kuwa bila kupata barka ya huyo mnayeona amewazidi hamtulii! Itakuwa vyema ukiweza kutuambia hao maaskofu ( ututajie majina) walitoa karipio gani kwa CUF! Badala ya kuwalaumu CCM Zanzibar ( ambayo imejaa waislamu wenzenu), nyinyi mmebakia kuwaandama wakristu ambao idadi yao huko Zanzibar ni kiduchu mno!

Wasema kwakuwa mgombea wao Padri Slaa ameanguka wamekuwa wakali kama pilipili wamefikia hadi kuwafuta uumini baadhi ya waumini wa kikristo Sumbawanga kwakuwa walienda kinyume na matakwa ya kanisa kwenye uchaguzi wa mwaka jana. Habari kubwa kwangu kumbe wenzetu mnaweza kupokonywa ukristo kwa barua?
Usichanganye ukristu na dhehebu. Usichanganye kutengwa na kufutwa ukristu. Katika madhehebu mengi (pamoja na wakatoliki) hakuna mtu anayefutwa ukristu bali kuna kutengwa. Mtu anayetengwa anabakia kuwa mkristu na anaweza kurudishwa kundini anapotubu matendo yale yaliyomfanya atengwe. Mara nyingi mtu anatengwa kwa sababu vitendo vyake ( au maneno yake) vinatishia umoja wa jumuia anako -abudia. Kwa mfano, kwa wakatoliki, mtu akijulikana ametoa mimba anaweza kutengwa hadi hapo atakapotubu. Mtu akitengwa jumuia inafahamishwa kuwa fulani na fulani wamepetengwa na hawaruhusiwi kupokea sakramenti ingawa bado ni wakatoliki. Waluteri wanaweza kumtenga mtu kwa jumuia anakoabudu kupiga kura ya kumtenga.

Sishangai kushangaa kwako kwa matumizi ya barua kueleza jamii na mhusika kuhusu kutengwa kwao. Kwenu nyinyi adhabu ya mtu ambaye anaonekana kwa vitendo au maneno yake amejitenga kutoka uislamu ( apostasy-irtidad) ni nini? Adhabu yake si kupigwa mawe hadi kifo au kukatwa sehemu ya maungo yake? Unaona hii ni heri kuliko barua!

Kisha wakasema "TAMKO LA WAISLAMU DHIDI YA KAULI ZA MAASKOFU Waislamu wameiomba serikali kujiunga na OIC kama njia mojawapo itakayowezesha nchi yetu kupata misaada itakayotumika kuinua hali za Waislamu ambao wameachwa nyuma sana katika elimu na uchumi.
Yale yale ya kutegemea ankal aje awakwamue kutokana na matatizo yenu. Nitajie nchi moja ambayo imeendelea kutokana na kuwa mwanachama wa O.I.C. Pakistan? Sudan? Kwani waislamu mnaishi kwenye visiwa ambako hamna uwezo wa kuhudhuria shule zilizopo? Au ambako mnakatazwa kufanya biashara. Badala ya kubaki kulalamika, mngetiana hima kutumia nafasi ambazo zipo. Mbona wakina Bakhresa wameweza? Au nao ni wakatoliki?

Makanisa yote kwa kauli moja yamepinga kwa nguvu zao zote pendekezo hilo. Sababu ya kupinga kwao ni kuwa mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa Waislamu wanadhoofishwa katika kila hali, na ni makosa makubwa kuwaimarisha kiuchumi au kielimu maadui hao.
Makanisa yote? Wewe unajua kuna madhehebu mangapi Tanzania mpaka utoe statement kama hiyo? Halafu unaingia kichwani kwa hao usiowajua na kutaka kuwasemea. Hii ni demokrasia na kila raia ( mkristu, muislamu, mhindu, mfuasi wa imani za asili, rasta n.k.) ana haki ya kupinga kwa sauti kubwa kitendo chochote asichokubaliana nacho. Ni wajibu wenu kuja na arguments za kuonyesha udhaifu wa hoja zao. Kufyata mkia na kulalamikia chumbani hakusaidii hoja yenu. Mnatakiwa mje na hoja zilizoenda shule na si hiyo ya kutaka kulinganisha O.I.C. na Vatican.

Serikali ilipofanya utafiti wake wa kina ikajiridhisha kuwa kujiunga na OIC kuna manufaa na hakuna madhara yoyote. Na Mh. Bernard Membe alitamka hilo Bungeni. Mara akaitwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Cardinali Pengo na kukumbushwa mkakati wa kuwadhoofisha Waislamu. Msimamo wa serikali ukabadilika.
Tangu lini BERNARD Membe amekuwa Rais wa nchi hii? Au POLYCARP Pengo? Kama msimamo wa serikali ulibadilika wa kulaumiwa ni kiongozi wa serikali ambaye alikuwa na bado ni JAKAYA Mrisho Kikwete., Muislamu mwenzenu. Au nae ni mkatoliki wa siri? Ndiyo maana Membe alipoenda kumkumbushia alichoambiwa na Polycarp kuhusu mpango wao dhidi ya waislamu akaafik mara moja maana jina lake halisi ni JACOB na sio JAKAYA! Kweli hamna aibu.

Lakini propaganda za kuwazuga Waislamu zinasema Watanzania wote ni kitu kimoja na nchi hii haina ubaguzi!"
Mbona mnashindwa kila wakati kuthibitisha huo ubaguzi? Leo Rais ni muislamu, Makamu wake ni Muislamu, Jaji Mkuu ni Muislamu. Waziri wa ulinzi ni Muislamu, Waziri wa Mambo ya Ndani ni Muislamu. Mkuu wa Polisi ni muislamu. Mkuu wa Uslama wa taifa ni muislamu. Waziri wa Fedha ni Muislamu. Mmepewa Chuo Kikuu bure na rais Mkristu. Lakini bado mnadai kuwa mnabaguliwa. Sijui mkipendelewa ndio itakuwa vipi!

Amandla......




 
@fundo mchundo.una matatizo ya msingi.ishu nikwamba tuliwafukuza wakoloni wote wazungu na waarabu ili tujitawale.lakin wazungu waliendelea na wanaendelea kutuibia kwa mgongo wa kanisa hata wewe unajua lakin hutaki kukubali tu.

Mkuu, tafadhali naomba utaje sehemu kama mbili hata tano hivi ambapo wazungu kupitia kanisa wanaliibia Taifa letu...
 
Kwani Rais Kikwete ni MKATOLIKI?Makamba ni MLUTHERANI?Hivi sio hawa waliowaahidi mahakama ya Kadhi?Unapoandika "HAMTAKI" ni kama Kikwete au Makamba sio Waislam wenzenu.Tuondoleeni upuuzi wenu hapa.Kama mna malalamiko,mkalieni kooni ustaadh mwenzenu Kikwete.Mnajifanya kama hamjui kuwa JAMBAZI HANA DINI
wewe mjinga mlala hoi Mahakama ya kadhi iliwekwa kwenye ilani wakati wa uongozi wa Mkristo mwenzenu Mkapa, na akaachiwa Kikwete ku implement ulitegemea nini hapo?
siku zenu zinahesabika!
 
Waislam wanalilia mfumo kristo Masheikh wanasema Maaskofu walinyamaza kimya mauaji ya Mwembechai na kutoa karipio kwa CUF walipouwawa waandamanaji kupinga matokeo na kudai katiba mpya 2001. Wasema kwakuwa mgombea wao Padri Slaa ameanguka wamekuwa wakali kama pilipili wamefikia hadi kuwafuta uumini baadhi ya waumini wa kikristo Sumbawanga kwakuwa walienda kinyume na matakwa ya kanisa kwenye uchaguzi wa mwaka jana. Habari kubwa kwangu kumbe wenzetu mnaweza kupokonywa ukristo kwa barua? Kisha wakasema "TAMKO LA WAISLAMU DHIDI YA KAULI ZA MAASKOFU Waislamu wameiomba serikali kujiunga na OIC kama njia mojawapo itakayowezesha nchi yetu kupata misaada itakayotumika kuinua hali za Waislamu ambao wameachwa nyuma sana katika elimu na uchumi. Makanisa yote kwa kauli moja yamepinga kwa nguvu zao zote pendekezo hilo. Sababu ya kupinga kwao ni kuwa mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa Waislamu wanadhoofishwa katika kila hali, na ni makosa makubwa kuwaimarisha kiuchumi au kielimu maadui hao. Serikali ilipofanya utafiti wake wa kina ikajiridhisha kuwa kujiunga na OIC kuna manufaa na hakuna madhara yoyote. Na Mh. Bernard Membe alitamka hilo Bungeni. Mara akaitwa na Askofu Mkuu wa Jimbo la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Cardinali Pengo na kukumbushwa mkakati wa kuwadhoofisha Waislamu. Msimamo wa serikali ukabadilika. Lakini propaganda za kuwazuga Waislamu zinasema Watanzania wote ni kitu kimoja na nchi hii haina ubaguzi!"

Kama hakuna agenda iliyojificha ndani ya IOC kwa nini wasiwapatie waislamu misaada, kuna ulazima gani wa secular state kujiunga kama nchi ya kiislamu ndo ipewe misaada?

Hali kadhalika ningependa unishawishi mimi kama mwananchi ni faida zipi taifa letu litapata kwa kujiunga na IOC zaidi ya kuendelea kuwa omba omba? Hii ni aibu kubwa kushabikia nchi yako kujiunga IOC ili iwe ombaomba!
 
wewe mjinga mlala hoi Mahakama ya kadhi iliwekwa kwenye ilani wakati wa uongozi wa Mkristo mwenzenu Mkapa, na akaachiwa Kikwete ku implement ulitegemea nini hapo?
siku zenu zinahesabika!

Sasa kwa nini JK haku implement? Na inakuwaje waislamu wanakuwa na Imani na serikari kuanzisha Mahakama ya kadhi wakati wanatuhumu serikari hiyo hiyo kuwahujumu waislamu kupitia BAKWATA? huu si ni unafki mkubwa jamani! on other hand unasema serikari inakuhujumu but on other side you ask the some government to implement KADHI issue, this is outrageous!
 
We kweli shule imepanda?
MOU ni makubaliano baina ya serikali na makanisa ambapo serikali inachota pesa hazina zinaenda kusaidi taasisi za kanisa kama hospitali na vuyo.Sasa pesa zikishatoka hazina maana yake ni kwamba mlipa kodi yeyeote bila kujali dini yake kodi yake ipo hapo.Hatukatai kanais kuwa na taasisi zake lakini waendesha wenyewe bila kuchota pesa zetu hazina.

Ukiwa unajibu hoja jibu pande zote. Mbona husemi serikali ilivyosaidia BAKWATA kila kitu mpaka uchaguzi Wa kumchagua MUFTI aliyeko sasa. Vp kuhusu Morogoro Islamic University kwani hizo pesa sizimetoka hazina ambayo pia no kodi ya wakristo...! Fikiri kwa makini
 
Nionavyo mimi nakuona wewe ni mtu unaelewa tunachodai ila kwakuwa unaangalia kwa jicho faida mnayopata wakristo katika upendeleo wa keki ya taifa umeamua kuwa mute (kuwa kipofu kwa makusudi), in summary tunadai haya:-

1. Kwakuwa kanisa lina mkataba na serikali wa kupewa remmittance in millions kutoka serikalini kwa ajili ya ku-finance hospitali per bed increment kila mwaka na kwakuwa waislamu hatukulalamika wakati wote tunaomba maaskofu waache kulalamika kuhusu process ya mahakama ya kadhi kwani ni mazungumzo yetu na serikali na wale viongozi wa serikali Hasa Pinda aache double standard kulishulikia hilo

2. Kwakuwa imeshapita miaka mingi na MoU imewafaidisha wakristo na kupendelea kwa kutoa pesa za umma kwenye taasisi zake ..hizo remmitance ziachwe, au zitolewe pia remmitance of the same scale kwa taasisi za kiislamu au zifutwe zote kama maaskofu wanakasirika pesa kwenda kwa taasisi za kiislamu (is this not just?) is this too much christians? au mmezoea kuchota pesa za serikali? ufisadi?

3. Kwakuwa nchi imeongozwa kwa muda mrefu kwa mgawanyiko wa kidini katika nafasi mbalimbali tunaomba swala hilo liwepo katika katiba, mgawanyiko uzingatie dini na qualifications ila kusiwe na ubaguzi wa kidini

Mahakama ya Kadhi ni sehemu ya ibaada ya kislamu hivyo serikari haiwezi ku play a role hapo, mzee wewe mbona unakuwa kihiyo hivyo, huwezi linganisha MOU na mahakama ya kadhi na MOU, unadhalilisha uislamu ndugu, kwa nini waislamu wasifuate taratibu za dini ya kislamu na kuanzisha KADHI, Kama waislamu wanataka MOU ya kutoa social services kwa jamii hilo halina ubishi na hakuna mtu atakaepinga, lakini sio swala kadhi, that will never happen.

Kama Nyinyi ni waislamu wa kweli kwa nini mnasema Mahakama ya kadhi itashughulikia maswala ya mirathi na ndoa tu? kwa nini msifuate jinsi quraan tukufu inavyosema yaani sheria law! mwizi wa kislamu akikamatwa anakatwa mkono, mzinifu wa kislamu akikamatwa apigwe mawe! mbona hivyo vipengele mnavikwepa wa ndugu, Tuache unafki wa kujifanya nyinyi ndo mnaujua sana uislamu kuliko watu wote, nyinyi ni wanafiki tu ambao ni wa kupuuzwa
 
wewe mjinga mlala hoi Mahakama ya kadhi iliwekwa kwenye ilani wakati wa uongozi wa Mkristo mwenzenu Mkapa, na akaachiwa Kikwete ku implement ulitegemea nini hapo?
siku zenu zinahesabika!
Nguzo hata huoni aibu inachosema kwamba Kadhi iliwekwa na Mkapa ambaye ni mkristo akaachiwa Kikwete ambaye ni mwislam kuitekeleza lakini ameshindwa sasa hapo mchawi nani? Mkristo Mkapa au Mwislam Kikwete
 
Mkuu, tafadhali naomba utaje sehemu kama mbili hata tano hivi ambapo wazungu kupitia kanisa wanaliibia Taifa letu...

Vuta subira kidogo ninamalizia kuscann document inayoonesha namna makanisa yalivyo na viwanja vya ndege maeneo yenye rasilimali zetu za taifa nchi nzima na huruka na madini na mali nyinginezo za taifa bila kukaguliwa hii ni tangia ukoloni,uhuru hadi leo.Hakuna Tra wala uhamiaji huko.Zamani nilikuwa nawa-admire wazungu kuwa wanapenda dini yao na wako tayari kuitumikia hadi maeneo ya ndani kabisa ya nchi nilipokuwa nikiwaona huko kumbe maskini wako kwa ajili ya kutuibia kwa jina la kanisa.Tumeumizwa sana na watu hawa.Hapa simaanishi kuwa ukristu unaruhusu wizi wa aina hii lakini hii ni tamaa ya mwanadamu akiongozwa na shetani.Tamaa hiyo hiyo waliyoitumia kututawala na kuuwa babu zetu wengi huku wameshika bunuki mkono wa kulia na biblia mkono wa kushoto wakisema ukipigwa shavu la kulia geuza na la kushoto.Ukristu hauruhusu haya lakini wao wamefanya tena kwa jina la ukristu huo huo.
Wazungu hao hao bado ni kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu,si ndo hao hao tunawapigia kelele hapa kwamba wanatupunja kwa mrahaba wa asilimia 3 wanapochimba madini yetu? Si ndo hao hao wanaotuingiza mkenge na mikataba mibovu wakishirikian na akina Sultani mangungu wetu wa zama hizi?Ukizungumzia ndege mbovu ya Rais,Rada,buzwagi nk ni wazungu wanaohusika.Wakti wanafanya hayo nchi zote za ulaya hasa magharibi bendera zao zina alama ya msalaba kama ishara ya mkombozi wao Yesu lakini hawatuonei huruma.We unataka ushahidi gani zaidi ya huo? Lakini subiri nilete ushahid mwingine.
 
Kaa chini fikiria kwa makini, je kabla ya kuja warabu na wazungu babu zetu walikuwa wana abudu nini, kwanini waje waseme hicho mnachoabudu si kweli, acha fuata cha kwetu {Uislamu au Ukristo}, wakati walikuwa wanaishi kwa kufuata mila na tamaduni zao kiasili, hii si haki kabisa, maaskofu na masheikh ni wanaoendeleza utumwa huu wa kidini na hawasemi ukweli kwa waumini wao, kibaya zaidi dinin hizi zilikuja kuchukua mababu zetu na kuwafanya watumwa katika nchi zao {Angalia Bagamyo-bandari ya zamani kuna nini-minyororo}.Jamani watu weusi tujitmabue asili yetu na tuthamini mila zetu, mtu anaona fahari kuitwa stephen badala ya masanja,ahmed badala ya matumla, kabila langu ndiyo dini yangu
 
Vuta subira kidogo ninamalizia kuscann document inayoonesha namna makanisa yalivyo na viwanja vya ndege maeneo yenye rasilimali zetu za taifa nchi nzima na huruka na madini na mali nyinginezo za taifa bila kukaguliwa hii ni tangia ukoloni,uhuru hadi leo.Hakuna Tra wala uhamiaji huko.Zamani nilikuwa nawa-admire wazungu kuwa wanapenda dini yao na wako tayari kuitumikia hadi maeneo ya ndani kabisa ya nchi nilipokuwa nikiwaona huko kumbe maskini wako kwa ajili ya kutuibia kwa jina la kanisa.Tumeumizwa sana na watu hawa.Hapa simaanishi kuwa ukristu unaruhusu wizi wa aina hii lakini hii ni tamaa ya mwanadamu akiongozwa na shetani.Tamaa hiyo hiyo waliyoitumia kututawala na kuuwa babu zetu wengi huku wameshika bunuki mkono wa kulia na biblia mkono wa kushoto wakisema ukipigwa shavu la kulia geuza na la kushoto.Ukristu hauruhusu haya lakini wao wamefanya tena kwa jina la ukristu huo huo.
Wazungu hao hao bado ni kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu,si ndo hao hao tunawapigia kelele hapa kwamba wanatupunja kwa mrahaba wa asilimia 3 wanapochimba madini yetu? Si ndo hao hao wanaotuingiza mkenge na mikataba mibovu wakishirikian na akina Sultani mangungu wetu wa zama hizi?Ukizungumzia ndege mbovu ya Rais,Rada,buzwagi nk ni wazungu wanaohusika.Wakti wanafanya hayo nchi zote za ulaya hasa magharibi bendera zao zina alama ya msalaba kama ishara ya mkombozi wao Yesu lakini hawatuonei huruma.We unataka ushahidi gani zaidi ya huo? Lakini subiri nilete ushahid mwingine.

Usisahau za wale WAZUNGU waliomegewa Loliondo na ambao wanaondoka na wanyama wetu kuwapeleka ULAYA! Au wale WAZUNGU ambao wanawinda wanyama wetu na A.K. 47! Na yule pilot MKRISTU aliyekamatwa red-handed akisafirisha dhahabu nje ya nchi lakini MKATOLIKI mwenzake ALI Hassan Mwinyi akamwachia akidai mama yake alimlilia sana! Na yule MKRISTU aliyesaini mikataba ya madini HOTELINI ambamo amewapa carte blanche waheshimiwa hao kukomba madini yetu. Juhudi zako za kuonyesha kuwa WAKRISTU NA WAZUNGU peke yao ndio wanaohujumu taifa letu ni lazima ziungwe mkono na wale wote wanaolitakia mema taifa letu.

Amandla.....
 
Kaa chini fikiria kwa makini, je kabla ya kuja warabu na wazungu babu zetu walikuwa wana abudu nini, kwanini waje waseme hicho mnachoabudu si kweli, acha fuata cha kwetu {Uislamu au Ukristo}, wakati walikuwa wanaishi kwa kufuata mila na tamaduni zao kiasili, hii si haki kabisa, maaskofu na masheikh ni wanaoendeleza utumwa huu wa kidini na hawasemi ukweli kwa waumini wao, kibaya zaidi dinin hizi zilikuja kuchukua mababu zetu na kuwafanya watumwa katika nchi zao {Angalia Bagamyo-bandari ya zamani kuna nini-minyororo}.Jamani watu weusi tujitmabue asili yetu na tuthamini mila zetu, mtu anaona fahari kuitwa stephen badala ya masanja,ahmed badala ya matumla, kabila langu ndiyo dini yangu

Mkuu umenifurahisha kwa upembuzi wako...harafu na wewe umejiita Donkey.......kazi kwe kweli............
 
Usisahau za wale WAZUNGU waliomegewa Loliondo na ambao wanaondoka na wanyama wetu kuwapeleka ULAYA! Au wale WAZUNGU ambao wanawinda wanyama wetu na A.K. 47! Na yule pilot MKRISTU aliyekamatwa red-handed akisafirisha dhahabu nje ya nchi lakini MKATOLIKI mwenzake ALI Hassan Mwinyi akamwachia akidai mama yake alimlilia sana! Na yule MKRISTU aliyesaini mikataba ya madini HOTELINI ambamo amewapa carte blanche waheshimiwa hao kukomba madini yetu. Juhudi zako za kuonyesha kuwa WAKRISTU NA WAZUNGU peke yao ndio wanaohujumu taifa letu ni lazima ziungwe mkono na wale wote wanaolitakia mema taifa letu.

Amandla.....

We Amandla nakushauri usikurupuke.Fuatilia vizuri kwanza mjadala ndo uchangie. Nilikuwa najibu swali mwanajamvi aliyetaka nimtajie japo mifano miwili ya wazungu wanavyotuibia.Sasa ningekuwa mtovu wa nidhamu badala ya kujibu swali nianze kuelezea orodha ndefu ya wote wanaotubia. Ninaamini wapo wengi wanotuibia na sio wazungu peke yao.lakini hao uliowatolea mifano hawajatumia taasisi za kidini kama miskiti kufanya uhalifu wamefanaya kama watu binafsi.Kinachoumiza ni kuona wazungu wanatumia taasisi za kidini kukomba mali zetu.Wanaotufilisi zaidi ni wazungu kuliko kabila lingine lolote.Lakini uko huru kuwataja wote unaowajua wanaotuibia sitajali mwizi wetu ana dini gani,ninachojua na kuamini hakuna dini yenye asili ya Mungu inayofundisha au kuruhusu unyama wa aina yoyote.Wahalifu wako katika dini zote uwe Uislam au Ukristu
 
Vuta subira kidogo ninamalizia kuscann document inayoonesha namna makanisa yalivyo na viwanja vya ndege maeneo yenye rasilimali zetu za taifa nchi nzima na huruka na madini na mali nyinginezo za taifa bila kukaguliwa hii ni tangia ukoloni,uhuru hadi leo.Hakuna Tra wala uhamiaji huko.Zamani nilikuwa nawa-admire wazungu kuwa wanapenda dini yao na wako tayari kuitumikia hadi maeneo ya ndani kabisa ya nchi nilipokuwa nikiwaona huko kumbe maskini wako kwa ajili ya kutuibia kwa jina la kanisa.Tumeumizwa sana na watu hawa.Hapa simaanishi kuwa ukristu unaruhusu wizi wa aina hii lakini hii ni tamaa ya mwanadamu akiongozwa na shetani.Tamaa hiyo hiyo waliyoitumia kututawala na kuuwa babu zetu wengi huku wameshika bunuki mkono wa kulia na biblia mkono wa kushoto wakisema ukipigwa shavu la kulia geuza na la kushoto.Ukristu hauruhusu haya lakini wao wamefanya tena kwa jina la ukristu huo huo.
Wazungu hao hao bado ni kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu,si ndo hao hao tunawapigia kelele hapa kwamba wanatupunja kwa mrahaba wa asilimia 3 wanapochimba madini yetu? Si ndo hao hao wanaotuingiza mkenge na mikataba mibovu wakishirikian na akina Sultani mangungu wetu wa zama hizi?Ukizungumzia ndege mbovu ya Rais,Rada,buzwagi nk ni wazungu wanaohusika.Wakti wanafanya hayo nchi zote za ulaya hasa magharibi bendera zao zina alama ya msalaba kama ishara ya mkombozi wao Yesu lakini hawatuonei huruma.We unataka ushahidi gani zaidi ya huo? Lakini subiri nilete ushahid mwingine.

Ndugu yangu, nakuomba upunguze kusoma ma-conspiracy theory ya ajabu ajabu, yatakupeleka pasipo marejesho. Wazungu ni wezi, ndiyo. Waarabu ni wezi, ndiyo. Miafrika tunachezewa na hawa watu kutokana na ujinga, upumbavu, tamaa, ubinafsi wetu. Dini ni kigezo tu. Msingi wa kutenganisha dini/imani na mambo yetu kama binadamu au jamii/taifa ni muhimu zaidi. Ukisoma signature yangu nimeashiria hili. Angalia sasa thread ifuatayo: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/104941-atcl-sued-for-breach-of-contract.html .... unafikiri wazungu wametumia kanisa hapa kuiba, au ni ubinafsi na tamaa ya mitanzania myenzetu??!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom