Jana nilibahatika kusikiliza majadiliano ambayo kupitia radio imani kulikuwa na majadiliano ambayo ni muendelezo wa tamko la waislamu walilolitoa katika ukumbi wa karimjee.Kilichonivutia kufuatilia majadiliano hayo ni baada ya kusikia kuwa baadhi ya wajumbe waliokuwa studio (Iman Radio)ni maprofesa kutoka chuo kikuu cha Kiislam morogoro. Nilikuwa na uhakika kabisa kuwa kutokana na heshima kubwa waliyonayo maprofesa ni lijua pengine mchango wao ungetosha kutoa au hata kueleza mambo yenye mantiki na manufaa kwa Taifa letu ambalo kwa miezi kadhaa sasa lina kila dalili ya kutoka katika mstari ulionyooka na kama hatua za dhati hazitachukuliwa ni dhahiri hatutaweza kubaki salama tena.
Katika majadiliano hayo, wajumbe hao (wakiwemo maprofesa) walitoa shutuma kali kwa viongozi wa kanisa hasa kanisa katoliki wakidai kuwa kanisa ndiyo linaendesha serikali na kwamba serikali inafuata maagizo ya kanisa aidha wajumbe hao walilaumu magazeti karibu yote ya jana/juzi kwa kushindwa kutoa habari za kina wakidai kuwa ni hujuma (pengine za kanisa)
Mashehe hao (wakati wa mjadala) pamoja na mambo mengi walijaribu kumlaumu waziri mkuu Mizengo Pinda pamoja na Mzee John malechela wakidai kuwa kitendo cha kuwaomba radhi maaskofu kwa matamko machafu yaliyotolewa na baadhi ya viongozi wa ccm (mzee makamba na mama chatanda) ni ukiukwaji mkubwa wa katiba na hivyo hawaoni kwa nini waziri Mkuu asijiuzuru (ushauri huo ulitolewa na shehe mwanasheria aliyejiita amebobea katika taaluma hiyo japo alipoulizwa na mtangazaji aeleze kifungu alichokiuka alishindwa kubaini kifungu hicho)
Lawama nyingine waliitupia serikali kwa kuacha Kanisa liendeshe nchi kwa kuachia Kanisa kuwa na Hospitali nyingi, vyuo vingi, na shule nyingi kitu ambacho vitu hivyo walidai kama vingemilikIwa na serikali kanisa lisingekuwa na nguvu. Kutokana mafanikio haya ya kanisa washehe hao (waliokuwa studio za Iman Radio) walikubaliana kwa pamoja kuwa njia pekee ya kufanya ni kuhamasishana kwa sasa na kudai wapewe eneo lao wajitawale ili kuepuka uonevu wa kutawaliwa na kanisa.
Naamini kuna wana JF ambao walisikiliza kipindi hicho kwa umakini na kupima hoja za wanazuoni hao. Kimsingi mimi sikushangaa kusikia matamshi hayo maana ndiyo hoja tulizozizoea ila kilichonisikitisha ni kuona kuwa hata wasomi waliobobea wanaliangalia tatizo walilonalo waislam kwa jicho na ufahamu wa mtu wa kawaida kabisa.
Pili nilishangazwa na taharuki ya hao mashehe kujumuisha sauti ya maaskofu wachache wa Arusha kama tamko la Kanisa la Tanzania kitu ambacho si kweli na hakipo.
Profesa analaumu Kanisa kuwa na idadi kubwa za Hospitali zinazotibu watanzania wote bila kujali dini katika matibabu hata ajira? mashehe hao walilaumu kanisa kupewa chuo cha Uhasibu Iringa Huku wao wakipewa cha morogoro. Wamesahau kabisa kuwa chuo cha Nskela Iringa kiliuzwa kwa kanisa kwa utaratibu wa kawaida huku chuo cha tanesco wakipewa bureee na Mkapa wala haijasikika mtu akihoji.
Wanazuoni hao walifika mbali kiasi cha kudai kuwa wabunge wengi kiasi cha 75% ni wakristo, wakati wanajua kuwa mbunge anaingia bungeni kwa kura? kama karne hii kuna watu wanamawazo hayo basi Tanzania ina safari ndefu ya kufikia hapo tunapotaka kufika.
Nashindwa kuelewa mpaka sasa kuwa tamko hili la mashehe lililoibua taharuki hii miongoni mwa waislam ni kufuatia tamko la maaskofu wa mkoani Arusha au kuna lingine? Nilitegemea tamko lingelenga hayo yaliyotokea Arusha badala yake kumeibuka hoja tofauti kabisa. inawezekana kuna tatizo ambalo sijaliona hivyo nimeona tueleweshane humu JF kuwa taharuki hii yenye hoja hata za kugawana nchi ni hili tu la Arusha au kuna lingine?
Katika majadiliano hayo, wajumbe hao (wakiwemo maprofesa) walitoa shutuma kali kwa viongozi wa kanisa hasa kanisa katoliki wakidai kuwa kanisa ndiyo linaendesha serikali na kwamba serikali inafuata maagizo ya kanisa aidha wajumbe hao walilaumu magazeti karibu yote ya jana/juzi kwa kushindwa kutoa habari za kina wakidai kuwa ni hujuma (pengine za kanisa)
Mashehe hao (wakati wa mjadala) pamoja na mambo mengi walijaribu kumlaumu waziri mkuu Mizengo Pinda pamoja na Mzee John malechela wakidai kuwa kitendo cha kuwaomba radhi maaskofu kwa matamko machafu yaliyotolewa na baadhi ya viongozi wa ccm (mzee makamba na mama chatanda) ni ukiukwaji mkubwa wa katiba na hivyo hawaoni kwa nini waziri Mkuu asijiuzuru (ushauri huo ulitolewa na shehe mwanasheria aliyejiita amebobea katika taaluma hiyo japo alipoulizwa na mtangazaji aeleze kifungu alichokiuka alishindwa kubaini kifungu hicho)
Lawama nyingine waliitupia serikali kwa kuacha Kanisa liendeshe nchi kwa kuachia Kanisa kuwa na Hospitali nyingi, vyuo vingi, na shule nyingi kitu ambacho vitu hivyo walidai kama vingemilikIwa na serikali kanisa lisingekuwa na nguvu. Kutokana mafanikio haya ya kanisa washehe hao (waliokuwa studio za Iman Radio) walikubaliana kwa pamoja kuwa njia pekee ya kufanya ni kuhamasishana kwa sasa na kudai wapewe eneo lao wajitawale ili kuepuka uonevu wa kutawaliwa na kanisa.
Naamini kuna wana JF ambao walisikiliza kipindi hicho kwa umakini na kupima hoja za wanazuoni hao. Kimsingi mimi sikushangaa kusikia matamshi hayo maana ndiyo hoja tulizozizoea ila kilichonisikitisha ni kuona kuwa hata wasomi waliobobea wanaliangalia tatizo walilonalo waislam kwa jicho na ufahamu wa mtu wa kawaida kabisa.
Pili nilishangazwa na taharuki ya hao mashehe kujumuisha sauti ya maaskofu wachache wa Arusha kama tamko la Kanisa la Tanzania kitu ambacho si kweli na hakipo.
Profesa analaumu Kanisa kuwa na idadi kubwa za Hospitali zinazotibu watanzania wote bila kujali dini katika matibabu hata ajira? mashehe hao walilaumu kanisa kupewa chuo cha Uhasibu Iringa Huku wao wakipewa cha morogoro. Wamesahau kabisa kuwa chuo cha Nskela Iringa kiliuzwa kwa kanisa kwa utaratibu wa kawaida huku chuo cha tanesco wakipewa bureee na Mkapa wala haijasikika mtu akihoji.
Wanazuoni hao walifika mbali kiasi cha kudai kuwa wabunge wengi kiasi cha 75% ni wakristo, wakati wanajua kuwa mbunge anaingia bungeni kwa kura? kama karne hii kuna watu wanamawazo hayo basi Tanzania ina safari ndefu ya kufikia hapo tunapotaka kufika.
Nashindwa kuelewa mpaka sasa kuwa tamko hili la mashehe lililoibua taharuki hii miongoni mwa waislam ni kufuatia tamko la maaskofu wa mkoani Arusha au kuna lingine? Nilitegemea tamko lingelenga hayo yaliyotokea Arusha badala yake kumeibuka hoja tofauti kabisa. inawezekana kuna tatizo ambalo sijaliona hivyo nimeona tueleweshane humu JF kuwa taharuki hii yenye hoja hata za kugawana nchi ni hili tu la Arusha au kuna lingine?