Mimi nakerwa sana na hii tabia ya kikundi kidogo cha watu kusema wale wanayo taka sema kisha kusingizia eti ni tamko la dini fulani, na mbaya zaidi wengine pia hukurupuka na kujibu kwa ujumla wake. maaskofu wa Arusha walivyotoa tamko kwanza hawakusema lile ni tamko la maaskofu wote nchini, maana tamko ili liwe la maaskofu wote ni lazima litolewe na baraza la maaskofu Tanzania. Sasa kinachosikitisha zadi ni hiki kikundi kidogo cha mashehe wa Dar nao kukurupuka na kujibu hoja, na basi wangejibu kama wanajibu Maaskofu wa AR, wao wametoa tamko la kujibu wakristo kwa ujumla wao, mbaya zaidi suala hili linazidi kuchochewa na vyombo vya habari tukiwemo JF. kwa jinsi nalivyosoma maoni ya wachangiaji, ni kama tunaelekea kule kulke walikotaka mshehe tuelekee, yaani kuufanya mgogoro wa AR, kuwa ni wa kidini. Mimi nafikiri tuache kujadili kwa kusema waislamu hivi waislam vile , wameskosa hiki wako hivi au vile, au kusema Wakristo ni bora, wanahiki na kile wana hivi wamefanikiwa au vile. Ni bora tuwajadili hao wachache waliotoa matamko, na mimi ningefikiri ingelikuwa bora zaidi kama tungewapuuza, maana kama tunawapa coverage kubwa hivi ni kuwapa wote Maaskofu na Mashehe waliotoa matamko, umuhimu ambao hawastahili kwa jambo hili. Sisi ni wamoja licha ya tofauti zetu nyingi tu baina ya dini zetu na hata baina ya sisi kwa sisi wa dini na imani moja!