Uchaguzi 2020 Marekani: Kuanzia leo, tunaweka vizuizi kwa waliohusika na kuvuruga Uchaguzi nchini Tanzania

Hawajafungia mitandao Bali ac ya trump
Katiba imempa kila raia wa US uhuru wa kujieleza kwa kufunga acc ya Trump manake umemnyima haki yake ambayo imetambulika kikatiba na kwa kufanya hivyo wameenda kinyume na katiba na kwenda kinyume na katiba ni kosa.
 
Account ya twitter ya Trump imefungiwa na CEO wa Twitter sio serikali ya Marekani..

Ni sawa leo umtukane Dewji afu akufungie kushabikia mikia na kukuzuia kuja mechi zao halafu uwe mkali unalalamikia serikali ya Tz.
Kwa hiyo CEO wa Twitter yupo juu ya katiba,manake kufanya hivyo ni kumnyima Trump uhuru wa kujieleza na siku zote US wanakuaga wakali kama akitokea mtu akaubana uhuru wa kujieleza.

Sasa kwa nini hawa kumwambia kwamba hicho alicho kifanya ni kosa.
 
Huyu kibarua chake kinakwisha kesho, itakuwaje kuhusu haya matamko yake?
Hilo ni tamko la Serikali ya Marekani ambayo ipo wakati wote hata vibarua vya wafanyakazi fulani vitakwisha, wengine wanapokea saa hiyohiyo kuendeleza maamuzi ya huko nyuma yenye maslahi kwa Taifa. Kama kuna maamuzi ya nyuma Serikali mpya itagundua hayafai, mchakato wa kutupilia mbali ni mrefu sana lazima upitie vitengo vyote viwili vya Bunge na kukubalika lakini inakuwa vigumu sana kwa sababu Wabunge fulani walikuwepo wakati maamuzi yanafanywa. Tofauti na Serikali ya Marekani, Serikali ya Magufuli ikimaliza muda wake madarakani, maamuzi na mamiradi mengi yasiyo na tija yatatupiliwa mbali na wahusika kuswekwa lupango. Mamiradi kama madege tupa baharini yasibane nafasi ya Uwanja wa Dar na likiwanja la Chato kuwarudishia wakulima wasiyo na mashamba ya kulima walionyang'anywa ardhi yao kupisha Mradi usiyo na tija. Mamiradi mengine yataachwa tu magofu maana yatakuwa yametekelezwa chini ya kiwango!
 
Marekani hahudumii sana wakimbizi ungesema Scandinavian countries ningekuelewa!
Una uhakika na ulisemalo?mashirika yote yaliyochini ya UN, marekani ndio mchangiaji mkubwa!!bado hiyo.misaada ya kibinadamu duniani kote ni yeye!!
 
Marekani ilikuwa zamani bhana!

We wasema.

Bila shaka umewakumbusha mabosi wako ambao hadi leo wanafungua akaunti huko na kurundika pesa wanazotufisidi huku kisha kila kukicha wao ni kiguu na njia kwenda kula bata huko.

Mjomba Trump alitudokeza: “Their leaders, these shthl countries, they rob their people blind and deposit their filthy loot in our banks here. They are always here spending their ill gotten wealth while their people at home go hungry. And still they have the audacity to ask us for relief! We should be arresting them next time the show up here.”

Na US akikuwekea pini basi allies wake wote wanakupiga nyota. Hata washindani kama Urusi na China wanakuchukulia kwa tahadhari.
 
..unadhani Joe Biden na Antony Blinken watafumbia macho ukatili wa serikali ya Magufuli dhidi ya vyama vya upinzani?
Nakuapia wazi kuwa kutokana na foreign policy principles za marekani, hakuna watakalofanya, kwa vile kuchokonoa serikali kunaweza kuleta instability kwenye region hii. Hawataigusa Tanzania, wala Uganda wala Rwanda. Hilo nakuapia kabisa.

Ni afadhali kama vyama vya upinzani vingekuwa na nguvu, lakini hivi vyetu bado kindergarten tu.
 
Kwani demokrasia yetu lazima ifanane na yao? Nyerere alisema, democracy is not like a bottle of Cocacola that you can just import from some other place, democracy should be self grown to suite the needs of our country, they can shove their sanctions up their stinky azz holes
Kwa wengine waibe, watese wapinzani, wawaengue kizembe, vituo hewa yote sawa tu. Tuondolee ujinga
 
Hapo kesho paramagamba utakuja live kwwnye tv akitumbua macho yake kama chura kadabwa na kamongo.
 
Kwa Taarifa yako waliozuiliwa wengi ni viongozi wako japo wa Tume nao wamo , kuna lundo la viongozi wanaokutumikisha , halafu kingine unachopaswa kufahamu ni kwamba ukizuiliwa na USA , basi kuna mataifa mengine kama 10 hivi hutakanyaga , omba Mungu msiugue Tezi dume au maradhi mengine ya kukata viungo kama naniliuu aliyekatwa vidole
Acha uongo wewe umewajuaje kwani Marekani hawajatoa hiyo orodha ya majina, kwa taarifa sio lazima mtu aende Marekani,nani ana demokrasia zaidi Tanzania au Marekani kwa wahuni wanaovamia bunge,Pompeo na timu yake ni sawatu na akina Amsterdam.
 
Juzi Kim Jong Un wa Korea kaskazini amesema, american policy des not change with Presidents.

Korea kaskazini wanaijua vizuri sana Marekani.

Wanaoweka vikwazo sio wanasiasa, ni career officers wa wizara ambao hua hawabadiliki kama wanasiasa.
 
Kwa Taarifa yako waliozuiliwa wengi ni viongozi wako japo wa Tume nao wamo , kuna lundo la viongozi wanaokutumikisha , halafu kingine unachopaswa kufahamu ni kwamba ukizuiliwa na USA , basi kuna mataifa mengine kama 10 hivi hutakanyaga , omba Mungu msiugue Tezi dume au maradhi mengine ya kukata viungo kama naniliuu aliyekatwa vidole
Kamanda, ni kina nani hao waliozuiliwa? Wakati wa Makonda walitaja jina kabisa, mbona wakati huu wanatupiga mafumbo jumla jumla tu?
 
Pompeo kwaheri ya kuonana,

Huyu mzee aliichukia Sana Tanzania,

Alikua anatuadhibu while hakukua na any grave reasons to do so compared to other countries.

Kama kulikua na grave mistakes za kupelekea sisi kupata adhabu za nchi kama Somalia na za aina hiyo wakaangalie Zanzibar, kule kuna SUK na amani tele.

Vikwazo hivi vina agenda nyingine ya siri ya kupambana na sisi, hakuna demokrasia it's all about the economy.

Marekani analia kwamba investments zake zimeathiriwa sasa hivyo naye anaamua kupambana nasi kupitia kivuli cha demokrasia.

Haya ni madhara yaliyoletwa na wale wote waliokuwa wanalitakia Taifa letu mabaya kwa kupeleka Taarifa mbaya juu yetu, Maria Sarungi, Fatma Karume, Tundu Lisu na wenzake hao hawatakii mema Taifa letu hata chembe.
 
Back
Top Bottom