Sisi Arteta alijichanganya kwenye mid akapaweka hovyo hovyo tukapasuka 3. Kama mid yenu itakua imara Palace hawana ukali huo.Juzi nilisema hapa kama United wanataka kujihakikishia Europa League basi wapate angalau point 1 kwenye mechi ya Brighton na nilijua kabisa kwa jinsi timu inavyocheza ni ngumu kupata points 3. Kwa hali ilivyo wangefanikiwa kupata point 1 matumaini yetu tungewaachia City ambao bila shaka wasingetuangusha.
Kama tungefanikiwa kupata point 1 maana yake tungesubiri tu West Ham afungwe na City na tungekuwa tumeshafuzu UEL. Sasa hali ilivyo sasa endapo tutafungwa na Palace na West Ham akamfunga Brighton ni wazi tutatolewa kwa Goal difference na kuna possibility kubwa United hataondoka na points 3 kwa Palace na kama West Ham atapata droo game ya City (which is possible) game ya mwisho pressure itakuwa juu zaidi na tumeshaona kikosi tulichonacho hakiwezi ku-handle games zenye pressure kubwa so nategemea game ngumu zaidi na Palace hawana cha kupoteza so wata-relax na watakuwa na utulivu zaidi.
Pia Westham akimfunga city aisee itakua ni miongoni mwa upset za kimichezo katika mpira ingawa kimtazamo ni ngumu.


