Castr
JF-Expert Member
- Apr 5, 2014
- 37,925
- 75,787
Nimeandika kadri ninavyoweza.Timu yoyote kabla ya kuanza ligi au kuanza game lazima tambo ziwepo, wakati wa usajili tambo lazima ziwepo, United hata kama tunajua kua mechi ya leo tunaenda kufungwa lakini kabla mechi kuanza lazima tulete tambo kibao muulize allypipi analijua hilo yaani ile manchester leo ipo uwanjani na dunia nzima inafuraha.
Ila baada ya mechi kuisha hua ndio muda wetu wa kuondoa stress kwa kukosoa, kukebehi, hata kutukana inapobidi na ndio maana timu yetu ndio timu inayojulikana kua ni timu ya furaha dunia nzima
Tukifunga ni furaha, tukifungwa pia furaha inatawala, Maguire akitoa boko tukachezea pia tunachukulia kama kibwagizo cha furaha yetu.
Ila nyie mbuzi mkifungwa sasabado mnang'ang'ania kutetea upumbavu, na akitokea mmoja wenu kuelezea hata hisia zake mnamjia juu kwelikweli.
Mpira ni burudani ndugu zangu, nyie kila kitu mnachukulia serious ndio maana hua mnajinyonga mbuzi nyie.
Kuweni japo kama OllaChuga Oc ili muendelee kufaidi mema ya nchi.
Bahati mbaya haujanielewa.


