Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Watu awaelewi wanachukulia mupira seriyaz ndio maana majitu hapa ukiyatania tu kidogo mzee yanaporomosha matusi adi shety( shetani) anaomba poo ..hahaha usipokubali kutaniwa ..Basi mtu kaa Mimi ndio naongezaga mautani adi zile asira za kuweka mguu mfukoni au kumeza wembe zinakushika hahahaha na Mimi nasema hiiiiii😂😂😂😂
bora hata wewe unakimbilia jukwaa la mapishi ukifungwa
 
Ndio naona hapa muda sio mrefu kutoka kwa Fabrizio kumbe majirani zetu tayari wamemalizana na 'Lukaku' mpya?
ile taarifa nilifanikiwa kuisoma asubuhi kutoka kwa mtaalamu david ornstein, nafikiri yeye ndiye muandishi wa mwanzoni kuripoti taarifa hiyo. Kwa nini awe erling haaland na si harry kane?. Any tips.
 
Watu awaelewi wanachukulia mupira seriyaz ndio maana majitu hapa ukiyatania tu kidogo mzee yanaporomosha matusi adi shety( shetani) anaomba poo ..hahaha usipokubali kutaniwa ..Basi mtu kaa Mimi ndio naongezaga mautani adi zile asira za kuweka mguu mfukoni au kumeza wembe zinakushika hahahaha na Mimi nasema hiiiiii😂😂😂😂
Mpira ni mchezo wa hisia unapotoka kufungwa kwa dakika kadhaa nyongo inakuwa imechafuka mtu akileta utani ni kama anaweka chumvi ktk kidonda sasa hapo tuna tofautiana jinsi ya ku-handle hizo reactions. Kadri unavyozidi kuwa mtu mzima hisia za maumivu hupungua (above 25 yrs old).

Binafsi nimeanza kuangalia mechi za United toka mwaka 1999 May, 26 mpaka sasa labda nimekosa michezo isiyozidi 30. Unaweza kujionea hapo nimepitia vipigo vingapi ndani ya miaka karibu 23. Nishawahi kunyata kurudi chumbani kwangu nilipokuwa chuo kikuu baada ya kufungwa na Barcelona fainali.

Michango ya watu waliokomaa hata timu ikifungwa hujikita ktk mchezo zaidi ni wapi palikuwa na mapungufu na nani kazingua na nini kifanyike ila watoto wadogo wengi labda hata wewe pia ni mmoja wao hujikita zaidi ktk mizaha ila mimi huchukulia kawaida najua wapo ktk kipindi cha umri sahihi kufanya hayo.
 
ile taarifa nilifanikiwa kuisoma asubuhi kutoka kwa mtaalamu david ornstein, nafikiri yeye ndiye muandishi wa mwanzoni kuripoti taarifa hiyo. Kwa nini awe erling haaland na si harry kane?. Any tips.
Huu usajili Pep Guardiola hakuhusishwa moja kwa moja alikuwa mshauri zaidi nafikiri umelenga mkakati wa muda mrefu wa City.

Pep mkataba wake unaisha mwakani. Habari za chini chini zinasema Ferran Sorriano na Txiki wameanza mazungumzo ya awali na Luis Enrique.
 
Huu usajili Pep Guardiola hakuhusishwa moja kwa moja alikuwa mshauri zaidi nafikiri umelenga mkakati wa muda mrefu wa City.

Pep mkataba wake unaisha mwakani. Habari za chini chini zinasema Ferran Sorriano na Txiki wameanza mazungumzo ya awali na Luis Enrique.
ninachokiona usajili wa erling haaland kuelekea manchester city utawarudisha manchester united kwenye mbio za kumuwania harry kane. Mwezi mmoja uliopita muandishi laurie whittwell (tier 1) aliripoti taarifa inayowahusu viongozi wa manchester united kuwalenga wachezaji wawili au watatu wanaotarajia kuwasajili msimu huu na kati yao ni declan rice au kelvin phillips, harry kane au darwin nunez. Laurie anasema licha ugumu wa dili hizo lakini tayari viongozi wa manchester united wakiongozwa na ed woodward walishafanya mazungumzo na daniel levy juu ya usajili wa harry kane tokea msimu uliopita lakini kikwazo ilikuwa ni dili la sancho. Kama city watakwenda kwa haaland basi united watajaribu bahati yao kwanza kwa kane na wakati huo jorge mendez alishachukua tenda ya kufanya dili la darwin nunez kuelekea tottenham hotspurs au manchester united na hapo itategemea na dili la kane.
 
Laurie whitwell akaendelea kusema: ndani ya manchester united mchakato wa usajili unafanywa kwa njia ya veto, kwa maana ya scouting pamoja na bodi wanakuwa na target zao na kocha naye anakuwa na target zake. Hizo pande mbili zinajadiliana na baadae kufanya mchakato wa usajili na mchezaji atakayepatikana ndiye huyo na tukumbuke mchezaji anapatikana kwa factors nyingi, hapo ndipo zinapokuja zile hadithi za kocha fulani kaletewa mchezaji ambaye si chaguo lake. Mfano mdogo rejeeni usajili wa donny van de beek chini ya ole. Donny alisajiliwa kwa sababu ya urahisi wa mchakato wake wa kusajiliwa na si kwa sababu ya mwalimu ndio maana hakumpa nafasi. Vile vile rejeeni usajili wa fred chini ya mourinho.
 
Kwa mfano tujiulize kwa nini jina la tchouameni halitajwi mara kwa mara kwenye maandishi ya hawa waandishi mashuhuri wa kuripoti habari za manchester united kama vile james ducker, howson, stone, whitwell na wengineo. Kwa nini jina lake lihusishwe zaidi na liverpool pamoja na real madrid. Mbona declan rice anatajwa sana, ruben neves anatajwa kwa sababu ya uzoefu wake wa premier league na si target lengwa hivyo upo uwezekano wa kuwa backup ya declan rice au kelvin phillips. si ajabu watu wa ndani kabisa ya manchester united wakawa hawamtambui tchouameni. Scouting yetu ni bora sana lakini decisions zinanachelewa kufanywa na kwa usahihi.
 
Cha umuhimu tuombe ten hag awe mgumu ila kinyume na hapo tujiandae na cycles ile ile ya makocha kulalamikia usajili baada ya kufukuzwa kazi. Target tajwa za ten hag ni jurrien timber na winga kutoka brazil pia anachezea ajax. Hawa watakwenda kuunganishwa na wale wa bodi.
 
Nagelsmann anamtaka konrad laimer kutoka leipzig kwa euro millio 15 hadi 30 tu. Technical si mbora sana lakini ni pressing machine. Ni DM na ana miaka 24 tu, jiulizeni kwa nini jina lake halitajwi sana ukicompare na declan rice au kelvin phillips. Bila ya shaka huyu amependekezwa na ralf rangnick kama ilivyo kwa nkunku christopher.
 
ninachokiona usajili wa erling haaland kuelekea manchester city utawarudisha manchester united kwenye mbio za kumuwania harry kane. Mwezi mmoja uliopita muandishi laurie whittwell (tier 1) aliripoti taarifa inayowahusu viongozi wa manchester united kuwalenga wachezaji wawili au watatu wanaotarajia kuwasajili msimu huu na kati yao ni declan rice au kelvin phillips, harry kane au darwin nunez. Laurie anasema licha ugumu wa dili hizo lakini tayari viongozi wa manchester united wakiongozwa na ed woodward walishafanya mazungumzo na daniel levy juu ya usajili wa harry kane tokea msimu uliopita lakini kikwazo ilikuwa ni dili la sancho. Kama city watakwenda kwa haaland basi united watajaribu bahati yao kwanza kwa kane na wakati huo jorge mendez alishachukua tenda ya kufanya dili la darwin nunez kuelekea tottenham hotspurs au manchester united na hapo itategemea na dili la kane.
Japo siwakubali waingereza ila Harry Kane ni proven player wa EPL.

Darwin au Erling hakuna uhakika kama wanaweza ku-deliver au lah.
 
Tuna dirisha gumu sana, kila pembe itaangaliwa manchester united. Hivi hawa wahuni wamebadilika kweli au ndio biashara ile ile?.. Kiupande wangu sina matumaini yeyote, nimejikatia tamaa baada ya kushuhudia failure ya aibu kwa msimu huu.
EtH akipewa backup nzuri ya uongozi pamoja na sisi mashabiki bila kuwa na kiraru cha kutaka kurejea haraka haraka ktk ubora wetu tunaweza kufanya jambo ktk kujenga msingi wa awali.

Dirisha hili lina wachezaji wengi sana wazuri wa bei chee kila idara kuliko msimu wowote ule toka nimeanza kuangalia mpira ila hawaimbwi ktk vinywa vya watu. Hawa niliowa-list hapa chini wote wana umri wa miaka 20 ~ 23 na bei zao hakuna anayeweza kuzidi hata Euro 50M.

Beki wa kati: Alessandro Bastoni, Nico Schlotterbeck, Josko Gvardiol

Beki wa kushoto: Borna Sosa, Tyrell Malacia

Viungo: Boubacar Kamara (free agent, 150k/weekly), Matheus Nunes
 
EtH akipewa backup nzuri ya uongozi pamoja na sisi mashabiki bila kuwa na kiraru cha kutaka kurejea haraka haraka ktk ubora wetu tunaweza kufanya jambo ktk kujenga msingi wa awali.

Dirisha hili lina wachezaji wengi sana wazuri wa bei chee kila idara kuliko msimu wowote ule toka nimeanza kuangalia mpira ila hawaimbwi ktk vinywa vya watu. Hawa niliowa-list hapa chini wote wana umri wa miaka 20 ~ 23 na bei zao hakuna anayeweza kuzidi hata Euro 50M.

Beki wa kati: Alessandro Bastoni, Nico Schlotterbeck, Josko Gvardiol

Beki wa kushoto: Borna Sosa, Tyrell Malacia

Viungo: Boubacar Kamara (free agent, 150k/weekly), Matheus Nunes
schlotterback ameshasajiliwa na borussia dortmund, ujio wake pamoja na sule kunatengeneza mazingira ya kuondoka kwa manuel akanji anayewaniwa na manchester united. pia kuna pau torres naye analengwa ila khofu yangu ipo kwenye ushindani dhidi ya chelsea wanaokwenda kupoteza walinzi wakati watatu.
 
EtH akipewa backup nzuri ya uongozi pamoja na sisi mashabiki bila kuwa na kiraru cha kutaka kurejea haraka haraka ktk ubora wetu tunaweza kufanya jambo ktk kujenga msingi wa awali.

Dirisha hili lina wachezaji wengi sana wazuri wa bei chee kila idara kuliko msimu wowote ule toka nimeanza kuangalia mpira ila hawaimbwi ktk vinywa vya watu. Hawa niliowa-list hapa chini wote wana umri wa miaka 20 ~ 23 na bei zao hakuna anayeweza kuzidi hata Euro 50M.

Beki wa kati: Alessandro Bastoni, Nico Schlotterbeck, Josko Gvardiol

Beki wa kushoto: Borna Sosa, Tyrell Malacia

Viungo: Boubacar Kamara (free agent, 150k/weekly), Matheus Nunes
boubacar kamara alizungumzwa sana dirisha la january, tusubiri tuone kama tutajishughulisha kutafuta saini. Kuhusu harry kane nachukizwa na thamani yake inayoegemea paundi million 100 au zaidi na ukijumlisha umri wake naingiwa na khofu japo kuwa lewandowski na benzema wametuondoa kwenye ile dhana ya kuwapuuza wachezaji wenye miaka 30.
 
Back
Top Bottom