Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

mufc's defensive stats in the Premier League this season:

Goals conceded (15): 16th
Clean sheets (1): 18th
Shots on target faced (43): 14th
Tackles (104): 20th
Errors leading to shots (8): 20th
Expected goals against (14.3): 15th
 
Hamjambo ndugu zangu vipi bado tunaimani na Ole au sasa tuko na kauli moja?? Plastic fan hapa nawasalimu kwa jina la Ole tunaimani na Ole wetu.

Eti kuna mtu kabisa aliwaza tunaweza kuwafunga Liverpool kwa uchezaji wetu hehehe, nilisema hapa last week kwa moto wa yule mtoto wa farao tutawezana kweli haya kaweka record sasa miongo mingapi sijui anyway nilikuja kuwasalimu ndugu zangu die hard fans.
Ni mimi plastic
 
Haya hawapo na tayari 3 bila dakika ya 40
Belo my braza, nakusalimu mkuu. Pole najua ni kwa kiasi gani unaumia na hii club iliyopewa malegendar ambao hawajui soka la mbinu zaidi ya lile walilocheza kipindi chao.
Kwa taarifa yako tu braza, sosha hatakiwi pale OT, lakini ni nani atakuwa mbadala wake? Coach wa viwango vya juu wa kufundisha club kubwa kama united ni nani?
Menegement yote na body pia wanashindwa kujua nani wampe huu mzigo ausogeze. Conte! Hawezi kukubali kuchukua timu kwenye mazingira yaliyopo sasa.
Nani kwa mtazamo wako anaweza kupokea hii timu toka kwa ole?
Poleni sana.
 
Kuna rekodi za kutosha zimewekwa leo
Kwa haraka haraka izi hapa
Liver ndio mara yao ya kwanza kupata ushindi wa bao tano pale ot

Mo salah ndio kiumbe wa kwanza from liver kupiga hat trick ot

Klopp ndie kocha wa kwanza kwenda unbeaten game saba pale ot


Kama nimekosea nirekebishwe
 
Tufike mahali tudadavue tatizo liko wapi? Wengi ni kulaumulaumu tu hakuna ujuzi wa kutambua shida iko wapi.

Kipindi cha kwanza nafasi za kufunga za Manutd zilikuwa nyingi kama za Liverpool lakini ukabaji wa Liverpool ni bora kuliko wa Manutd na pia umaliziaji uligoma leo.


Kushinda hii ligi, inabidi Solksier apunguze striker mmoja wabaki wawili kwa sababu left na right backs wanaweza kushambulia.

Jawabu ni kumchezesha Dalot amsaidie Luke Shaw upande wa kushoto na kumweka bench Rashford.

Mabao yote yamepitia kwa Luke Shaw kwa sababu Luke Shaw anapenda kucheza kama Central Midfielder wakati ni left back


Hii inamaanisha Manutd hujikuta na three central defenders na inapungukiwa na left back na hapo Atalanta na Liverpool wameliona hilo na nina uhakika Spurs na Manchester City wameliona.

Ukiona Dalot hajapangwa next mechi ujue fika Manutd watafungwa kupitia left back. Mipira itaelekezwa upande wa left back na Luke Shaw ataendelea kugongana na Maguire na pasi zitapelekwa left back Luke Shaw atakuwa hayupo bao litafungwa.

Leo angepanga five defenders Liverpool hata bao moja asingelipata na angefungwa.

Kikosi cha ushindi

Left back Dalot, right back Wan Bissaka na three central defenders yaani Luke Shaw, Maguire na Lindelof.

Kati Fred, McTominay na Fernández

Washambuliaji CR7 na Greenwood.


Pogba auzwe desemba hii anawavunja moyo wenzie. Ukiona timu kubwa inamwendekeza mchezaji ambaye hataki kuongeza mkataba ndani ya miaka miwili kabla ya mkataba kwisha huyo hana mapenzi na timu. Hivyo, kumuuza tu hata kwa dau la kutupa.

Pogba mkakati wake ni kuacha mkataba uishe halafu ajiunge na aidha Real Madrid au PSG na dau la usajili apewe yeye badala ya Manutd. Inasemekana atalipwa £25MILL akijiunga na PSG kama mchezaji huria.

Pogba kiwango kimeshuka kwa sababu yuko kibiashara zaidi kulikoni kiuchezaji.
 
Kuna wanachezaji hawastahili kucheza United

Wan bisssaka

Magwaya

Lindelof

Mctominay

Rashford

Shaw

Fred

Hawa wote hawana hadhi ya kucheza United trust me sio kocha tu mtakuwa mnamwonea hao wachezaje ni averega players kabisa wanastahili kucheza norwish city au stoke city

Duh
 
Gary Neville amemkingia kifua Ole, pumbavu kweli kweli

FE38693F-E4A2-4A1D-BADF-74468482A788.jpeg


DCF27C0F-7353-4377-A927-BCE56834418F.jpeg
 
This Solskjaer 4-2-4 that he’s gone for in recent games, is a candidate for the worst tactical setup in Premier League history. The spaces available for the opposition to penetrate in midfield and behind the defensive line, are incredible.
 
tunaanza lini kujadili sajili zilizofanywa na ole gunnar solskjaer.
  1. daniel james
  2. harry maguire
  3. wan bissaka
  4. donny van de beek
  5. bruno fernandez
Hapo kwa bruno mbona umeweka red mkuu.?
Huyu kocha ni hana plan team haina pattern of play na makosa ni yale yale naye kaendekeza wachezaji walewale.

Huwa nawaza kocha huwa anaangalia hata marudio na ku address haya makosa kwenye mazoezi?
 
Back
Top Bottom