Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

pale alishakubali matokeo na bahati mbaya tunafunga magoli 2 haliyakuwa tushafanya sub mara tatu.
nakuhakikishia pale angalimuingiza mata au james kama ingelikuwa bado hajamaliza round 3 za mabadiliko.

jamaa ni mjinga sana
Pogba anapiga krosi hamna hata mtu kwenye boksi..mata na ighalo bora hata wangeingia na sio fosu mensah..

Tutapata tabu sana mkuu na huyu Ole
 
luke shaw alikuwa vizuri sana kiulinzi hapo jana, ikiwa ole amemtoa alex telles kwa sababu ya timu yetu kukosa mchezaji tishio kwenye box atakayeweza kuendana na movement za telles na kuwafanya leipzig wawe bize hususani kwenye crossing basi hilo ni tatizo jengine la ole, ina maana ameshindwa kutengeneza system bali ametengeneza utegemezi wa mtu fulani.

huhitaji mtu special atakayeweza kuendana na movement fulani bali unahitaji mfumo na huo mfumo hutengenezwa kupitia mazoezi.

labda munisaidie:
ukiondoa mechi ya everton ambayo tulishuhudia keane na holgate wakilinda kizembe kwenye box na kumruhusu bruno afanya kile alichokifanya, je ni mechi gani nyengine tulioshuhudia rashford au greenwood akifunga au alizofunga kwa mpira wa kichwa?
naomba munikumbushe
 
PTER na Chifu-Mkwawa embu tieni neno kidogo bwana

Jana tumecheza na wakabaji 7(mabeki watano+two immobile mids) lakini ndani ya dakika 15 tupo two goals down..Coward defending+coward tactics

Kiilichokuja kunivunja mbavu ni zile SUB za wale mabeki kina Fosu Mensah
Labda kocha alitaka kuwachezesha timu nzima vijana toka academy (Fosu-Mensah,Brandon,Tuanzebe,Pogba,McTominay,Rashford,Greenword)
 
PTER na Chifu-Mkwawa embu tieni neno kidogo bwana

Jana tumecheza na wakabaji 7(mabeki watano+two immobile mids) lakini ndani ya dakika 15 tupo two goals down..Coward defending+coward tactics

Kiilichokuja kunivunja mbavu ni zile SUB za wale mabeki kina Fosu Mensah
Sikubahatika kuangalia kabisa mechi ya jana hata matokeo ndiyo nimejua sasa hivi.

Mimi niliamini UEFA tulitoka siku tuliyopoteza mechi na Instanbull hiyo mechi ndiyo imetuondoa kwenye haya mashindano.

Yote kwa yote Laisez Faire attitude ya Ole imekuwa ikitugharimu kila mara tunalazimika kutafuta ushindi wa lazima.

Pamoja na kufungwa wa kumfukuza Ole kazini ni bodi ya United.

United inacheza hovyo sana inapokuwa na pressure sababu kubwa ni kuwa kikosi bado hakina balance kwenye maeneo mengi uwanjani.
 
Paul Merson uko Sky sport kashamaliza kazi, OGS poor tactics

Woodwad sielewi kwann anachelewa

Screenshot_20201209-145339.jpeg
 
kaka yangu PTER hii kazi ya kumtetea mwendawazimu Ole kuanzia leo rasmi nakuachia wewe na bwana chief mkwawa.
kwa ufupi nimechoka,
acha niunge mkono juhudi.
=================
kama kuna mshabiki wa manchester united anayefikiria ya kwamba siku moja Ole atafanikiwa kumfunga klopp ndani ya uwanja kimbinu (si ubabaishaji) basi wazo hilo aliondoe kwani hiyo siku haitojitokeza.
acha aendelee kumvizia guardiola asiyebadilika na mbinu uchwara zake
==================
tumekuwa mabingwa wa kusifia makipa wa timu pinzani kwa sababu ya kukosa kwetu umakini.
  • mendy wa chelsea hodari (ameokoa michomo dhidi yetu)
  • kipa wa sevilla hodari (ameokoa michomo dhidi yetu)
  • kipa wa leipzig hodari (ameokoa michomo dhidi yetu)
  • kipa wa southampton hodari (ameokoa michomo dhidi yetu)
  • kipa wa west bromwich hodari(ameokoa michomo dhidi yetu)
shots conversion rate yetu ni mbovu kuwahi kutokea,
Mimi huwa namtetea Ole pale anayefanya vizuri lakini alifanya vibaya sina time nae.

Nilishasema toka siku nyingi Attitude ya Ole inatugharimu big time.

Anyway mimi sikuangalia mechi jana hata highlights sitazingalia pia.
 
Sikubahatika kuangalia kabisa mechi ya jana hata matokeo ndiyo nimejua sasa hivi.

Mimi niliamini UEFA tulitoka siku tuliyopoteza mechi na Instanbull hiyo mechi ndiyo imetuondoa kwenye haya mashindano.

Yote kwa yote Laisez Faire attitude ya Ole imekuwa ikitugharimu kila mara tunalazimika kutafuta ushindi wa lazima.

Pamoja na kufungwa wa kumfukuza Ole kazini ni bodi ya United.

United inacheza hovyo sana inapokuwa na pressure sababu kubwa ni kuwa kikosi bado hakina balance kwenye maeneo mengi uwanjani.
Unazunguka sana more than 2 years tunasema UWEZO WA KOCHA NI MDOGO tunaenda mbele hatua 2 tunasahau then tunarudi hatua 7 nyuma ndio tunashtuka weekend atamfunga Man City atapewa sifa zote
 
Mimi huwa namtetea Ole pale anayefanya vizuri lakini alifanya vibaya sina time nae.

Nilishasema toka siku nyingi Attitude ya Ole inatugharimu big time.

Anyway mimi sikuangalia mechi jana hata highlights sitazingalia pia.
bora usiangalie.
jamaa wametudhalilisha sana kipindi cha kwanza,
halftime tungeliondoka na magoli matatu ya kufungwa ila bahati mbaya kuna mchezaji wa leipzig alikuwa offside kidogo sana
 
✓Ole aondoke,na Pogba afuatie..

✓Tu-hire kocha aliyeprove kitu hasa kutoka ligi ya Germany,atakayekuja na falsafa za kutufanya mpira wa uhakika uchezwe na mafanikio yapatikane

°°°Tukiendelea kubaki na Ole naamini hata top four hamna this season°°°
Kocha mpya bila shaka atataka kikosi chake. Mko tayari kufanya overhaul? Usidhani kuwa kocha atakipokea tu kikosi anachokikuta kwa kuwa wachezaji wengi wazuri. Kuna suala la personalities ambalo makocha wazuri huangalia zaidi.
 
imeshaniongezea presha na msongo wa mawazo kana kwamba nafaidika nayo kiutajiri..
leo nimepata usingizi saa 11 alfajiri (mawazo yamenitawala nafsini)

cha kwanza kinachoniuma ni kwamba jana jioni nilitembelea ukurasa wa instagram wa george ambangile alipost video yake akiwa ndani ya kipindi cha michezo akiwazungumzia leipzig jinsi wanavyocheza kuanzia pale katikati wanavyojazana kwa kuua winga zao, jinsi wanavyotumia angelino kuset mashambulizi baada ya kufanikiwa kumhamisha mlinzi wa pembeni eneo lake, pressing yao na ball possession na jinsi wanavyokuwa watano pale nyuma wasipokuwa na mpira kama umewaangalia vizuri(alitolea zaidi mfano wa mechi ya bayern munich).

yaani george anayeishi Tanzania anawafahamu leipzig kiundani kuliko kocha wetu na benchi lake la ufundi linaloongozwa na football analyst na wataalamu wa IT wanaotambulikana duniani.

kipindi chote cha kwanza wan bissaka alikuwa analazimika kuwa nje ya eneo lake(mara nyingi alikuwa anacheza katikati), ina maana leipzig walifanikiwa kimbinu ya kumhamisha eneo lake ili asikutane mara kwa mara na angelino (one against one) na hapo ndipo angelino alipata fursa ya kutukhanithi anavyotaka (goli zote zimetokea kwake na hata hizo walizokosa zinatokea kwake)

baadae nikaangalia video statman dave (kwa mashabiki wa man utd wengi wao watakuwa wanamfahamu) naye alikuwa anawafanyia analysing leipzig na jinsi gani unaweza kuwabypass (kuwadhibiti), huyu ni mzungu mwenzake ina maana kama ameangalia ile video basi angalijifunza, cha ajabu aliyoyazungumza dave ndio yale yale yaliokwenda kujitokeza uwanjani masaa matano baadae.

second half yule baradhuli wa kinorway anamtoa telles (sidhani kama ameumia) then anambakisha shaw ambaye hana match fitness kwa wiki za karibuni na dakika 20 baadae anamtoa luke shaw then anamuingiza brandon williams.

nilitamani televisheni niivunje kwa hasira.

watu mnamakasiriko sana leo wengine tushazoea tuliliona hili mda tu ole mweupe.
 
Na huku kazi anayo kidogo EZZ CHEZZ timu yako ilipigwa na timu gani vile huku Europa halafu mkasuluhu tatu tatu?
Siye hatuna shida. Wala hata hatukosi usingizi maana tushafuzu hata kabla ya game ya kesho, ndiyo ni kesho (noma sana kucheza alhamisi ila kwa kuanzia siyo mbaya).
 
Na huku kazi anayo kidogo EZZ CHEZZ timu yako ilipigwa na timu gani vile huku Europa halafu mkasuluhu tatu tatu?
Shida ya Spurs ni squad depth. Ukiacha wachezaji 11 wanaoanza hawa wengine ambao Jose hupenda kuwatumia kwenye Europa hawana motivation kabisa. Ndiyo sababu hata juzi kwenye game na hao wakulima LASK sare ilikuwa matokeo mazuri sana ukilinganisha na performance.

All in all Jose yeye anajua namna gani atadeliver kikombe kwa Levy.
 
Pogba ni mjinga sana, halafu haonagi kwamba umri unamtupa mkono. Anatimiza miaka 28 soon. Yeye ana amini bado ni mdogo eti ana bright years ahead. Hajui kwa ile mentality mbovu ataishia kuwa wonderful talent with no meaningful achievement. France kushinda WC sio kwamba ni direct credit kwake tu. Anatakiwa aoneshe anaweza ku shine nje ya kuwa covered na Kante na Matuidi
United itakapomuachia Pogba atakuwa na miaka karibu 30. Raiola anajua tafsiri yake ndiyo sababu anajitahidi kufanya fujo ili United ifanye muamala mapema. Sema Woodward keshaijua janja yao maana yeye ni genius wa biashara ya soka. Unaweza usiamini Pogba akaja kuishia OT.

Wachezaji wengi wafaransa kipaumbele chao siyo mafanikio ya uwanjani ndiyo sababu wana low mentalities kunako game. Angalia Martial, Bakayoko, Griezmann, na sasa Mbappe. Sisi ilibidi Levy aingilie kati ili asiingie hasara kwa Ndombele. Angalia namna anavyoisadia timu sasa hivi wakati msimu uliopita alikuwa anajifanya mgonjwa kila mechi.

Display zao uwanjani haziwiani kabisa na potential zao.
 
Back
Top Bottom