Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Baada ya kufanya tathmini ya kina nimegundua kwamba man u tatizo co tm bali ni kocha, mana kiukweli kabisa ukiangalia kikosi chetu kina wachezaji wengi tu classic pengine kuliko tm nyingi pale England ukiacha city na Liverpool but kocha hana mbinu ndomana wachezaji wanashindwa kuelewana.

Kocha ndiyo kila kitu kwenye tm, kazi ya kocha inaanzia mazoezini mpk kwenye vyumba vya kubadilishia nguo, kocha inatakiwa awe ambae amemudu wachezaji yn mchezaji akae benchi lkn akikubali kwamb nastahili kukaa benchi, kocha anatakiwa awe na hamasa kwa wachezaji kiasi kwamba mchezaji anajihisi yupo sehemu salama.

Lakini kocha wetu hana ushawishi kuanzia mazoezini mpk kwenye mechi, kocha wetu mda wote amekaa juu tu hana uhakika na kazi yake anawaachia wachezaji wapambane.

Ifike kipindi mashabiki tugundue kwmb Ole ameshafeli na ndiyo maana kuna makosa mengi tu ya kiuchezaji yanafanyika uwanjani lkn kocha haoni, km Ole ataendelea kuwa kocha tutegemee maumivu hata akiletwa Messi mwishowe ataonekana ni mchezaji wa Barca Tu na co tm nyngne.
Mkuu huu ndio ukweli ambao unauma watu wanaleta ushabiki kwenye ukweli
 
★The One en Only VERON★

#Legend
#GGMU
IMG_20200920_223438_849.jpeg
 
As i've said, Ole has to prove this season.

Mnaweza mjazia World Class Players wote 11 and still akashindwa ku-deliver.

Tusijifiche kwenye mgongo wa rebuilding wakati uwezo wa kocha ni mdogo.
Napinga kwa nguvu zangu zote, mpaka povu lina nitoka.
Ole, anatolewa sadaka tu.
Tatizo lipo kwa Grazza family & Ed wood.
Ifike hatua tuseme ukweli tu, timu yetu tangu wakabidhiwe hawa Grazza family na upepo wa furaha kwa mashabiki ukapotelea hapo.
 
Napinga kwa nguvu zangu zote, mpaka povu lina nitoka.
Ole, anatolewa sadaka tu.
Tatizo lipo kwa Grazza family & Ed wood.
Ifike hatua tuseme ukweli tu, timu yetu tangu wakabidhiwe hawa Grazza family na upepo wa furaha kwa mashabiki ukapotelea hapo.
Anaetakiwa kupanga kikosi ni kocha na sio Ed.

Wachezaji kucheza vibaya ni kocha na sio Ed.

Unamuuza Lukaku ukisema Rashford na Martial wanatosha, baada ya msimu mmoja unataka mchezaji wa kuziba hiyo nafasi.

Wachezaji wengi wameshuka viwango. Sio kosa la Ed wala Glazers.
 
Ubora wa wachezaji unatokana na kocha imara.

Kikosi cha Bayern hakina majina ya kutisha, ila mpira ukipigwa hapo utafurahi na roho yako.

Binafsi naamini tukiwa na kocha anayejua mbinu, hata hao kina Lingard watakichafua.

Sancho na wengine wakija, hakuna la maana watakalochangia kwa timu yenye kocha asiejua kuwatumia.

Tusifananishe rebuilding ya Klopp na ya Ole. Arteta na Lampard wanaonesha mwanga kuliko Ole.

Tuanze na kutafuta kocha kwanza. Wachezaji hawahawa lazima wakamuliwe vya kutosha.
Ivi, Ole, ni kocha wangapi tangu aondoke Ferguson?
Ni kocha gani alie leta maajabu?
Nb. Tuta muomba mpaka Mungu aje atu fundishe lkn hakita badilika chochote.
Leo tuna laumu kocha, kesho tuna laumu wachezaji, lkn mimi ninaimani kuwa Bodie ndio inatuua.
 
Anaetakiwa kupanga kikosi ni kocha na sio Ed.

Wachezaji kucheza vibaya ni kocha na sio Ed.

Unamuuza Lukaku ukisema Rashford na Martial wanatosha, baada ya msimu mmoja unataka mchezaji wa kuziba hiyo nafasi.

Wachezaji wengi wameshuka viwango. Sio kosa la Ed wala Glazers.
Kwani lukaku na martial nani ana nafuu?
Serious unamhukumu Ole kisa kumuuza lukaku, tafuta sababu nyingine.
 
Je ni first target zake!? Ktk misimu sita hivi walimu wote waliokuja ukiondoa Ole wamelia kilio kimoja kwamba hawakuwahi kutimiziwa demands zao za machaguo ya kwanza. Hata huyu ole nae siku akifurushwa tunaweza kuja sikia nilimtaka fulani, Fulani, na Fulani sikupewa. ED Woodward hakwepi lawama ila na kocha nae uwezo ni Mdogo.
Mkuu tuna fanana mitazamo.
Hapo Grazza family na ED Wood ndio wenye matatizo.

Hao jamaa ni kama wawekezaji wa Madini, yani wanachukua madini na kutuachia mashimo tu.
 
Hao wachezaji ndo walitupa Europa.

Ole akauza Herrera na Lukaku kisa hawafiti kwenye mfumo wake. Huo mfumo mpaka sasa haueleweki na hauonekani.

Leo hii anataka atafutiwe Striker wa kati wakati alimuuza Lukaku.

Ole aondoke kwanza.
Nliwahi kusema humu humu kwamba kumuuza lukaku will prove to be a huge mistake mbeleni
 
Louis Van Gaal alisema

"Bayern ina CEO na watendaji ambao ni watu wa mpira, wanajua nini ni nini ila Manchester CEO alikua ni mwekezaji benki unaweza ona kwanini usajili hauchukuliwi serious"

Hapo Van Gaal alikua ni mhanga mwingine. Moyes alimsajili Fellaini ambaye miezi kadhaa mbele alikua anaenda kua free agent na market value ikiwa ni 23M ila bodi (Woodward) ikalipa 27M kumpata Fellaini.

Mourinho akaja na kutaka wachezaji 5. Kati ya hao 5 aliletewa Fred tu, kisha akasema anamtaka Maguire bodi (Woodward) akasema Maguire ni ghali sana kwa pesa iliyotajwa na kiwango chake hivyo waachane naye.

Otea ni beki gani amekuja kua ghali kuliko wote duniani....

So Mourinho akapigwa chini huku analalamika juu ya usajili. Kaja Ole, akauza striker akasema ana Rashford na Martial, hali ikawa mbaya wakafanya usajili kwa kupaniki wakamsajili Ighalo.

Familia ya Ighalo ilifanya sherehe baada ya kujua Ighalo kaenda Man U.

Kisha wakati wa usajili umefika timu inatafuta mabeki, wingers na viungo hakuna sehemu waliyosema wanahitaji striker ila kama kawaida mwisho wa yote lawama zitakuja kwa kocha na atatimuliwa aje mwingine.

System ya Man U ipo designed kufukuza makocha, tatizo la kweli ni kutokua na DOF nafasi ambayo Woodward aliifuta hiyo nafasi na kujikaimisha yeye. Na akasema hawana mpango wa kuajiri DOF.

Hii timu morali ipo chini, hili tatizo tulikumbwa nalo Arsenal chini ya Emery. Watu hawajielewi wanazomewa hawajiamini yaani vururu vururu naona Man U inapita same route na tayari hata mashabiki baadhi wanaamini Ole ana matatizo.

The system.
Babu, kama kungekua kuna uwezekano wa kutoa Like nyingi, basi ninge kupa hata mia.
Mkuu ulichokiongea ndio kweli tupu, sema kuna watu wanaona fahari kubadili makocha kila siku, bila kujua kila kocha anae kuja, maana yake tunaanza upya.

Laiti tunge kuwa na CEO mwenye chembe chembe za soccer tusinge fika hapa.

Tatizo la timu yetu sio kocha wala wachezaji (hao wanatolewa kafara tu)

Ivi kuna mtu anashaka na uwezo wa LVG, ama Morinho?
 
Najaribu kufikiria kama OGS asingekuwa mmoja wa kina Neville, Giggs, Ferdinand, Keane na wenzao, sasa hivi angekuwa anashambuliwa sana.

Timu mliyonayo siyo ya kufungwa kwa manyanyaso vile na Crystal Palace, hata kama ni swala la kwamba hamjasajili, timu iliyowafunga imemsajili nani?
Waingereza wanafiki sana na hapo umemsahau Scholes
 
Kuna watu humu wanasema ni sababu man utd haijasajili ... ni sababu haina wachezaji world class kwenye baadhi ya maeneo ... lakini twende mbele turudi nyuma ... unahitaji kikosi kizima cha world class ndo uweze kupata points kwa Crystal Palace?

Ya kwamba kikosi hiki cha wakina Pogba, Fernandez, VDB na wengineo, ni dhaifu kiasi cha kutokuweza kupata points dhidi ya mid-table teams? Haingii akilini. Ingekuwa ni UEFA sawa.

Kuna shida mahali.
Hapo mahali palipo na shida ndipo watu wanaparuka na kuwa shushia lawama wachezaji na Makocha.
 
Anaetakiwa kupanga kikosi ni kocha na sio Ed.

Wachezaji kucheza vibaya ni kocha na sio Ed.

Unamuuza Lukaku ukisema Rashford na Martial wanatosha, baada ya msimu mmoja unataka mchezaji wa kuziba hiyo nafasi.

Wachezaji wengi wameshuka viwango. Sio kosa la Ed wala Glazers.
Ni kweli mkuu. Na kocha anaejitambua huwa anakuwa na nguvu za kuamua aonavyo yeye inafaa.

Bodi ya arsenal walishakubaliana AMN auzwe ila kocha akasema laa. Lukaku kumuondoa ilikuwa ni kosa kubwa sana
 
Baada ya kufanya tathmini ya kina nimegundua kwamba man u tatizo co tm bali ni kocha, mana kiukweli kabisa ukiangalia kikosi chetu kina wachezaji wengi tu classic pengine kuliko tm nyingi pale England ukiacha city na Liverpool but kocha hana mbinu ndomana wachezaji wanashindwa kuelewana.

Kocha ndiyo kila kitu kwenye tm, kazi ya kocha inaanzia mazoezini mpk kwenye vyumba vya kubadilishia nguo, kocha inatakiwa awe ambae amemudu wachezaji yn mchezaji akae benchi lkn akikubali kwamb nastahili kukaa benchi, kocha anatakiwa awe na hamasa kwa wachezaji kiasi kwamba mchezaji anajihisi yupo sehemu salama.

Lakini kocha wetu hana ushawishi kuanzia mazoezini mpk kwenye mechi, kocha wetu mda wote amekaa juu tu hana uhakika na kazi yake anawaachia wachezaji wapambane.

Ifike kipindi mashabiki tugundue kwmb Ole ameshafeli na ndiyo maana kuna makosa mengi tu ya kiuchezaji yanafanyika uwanjani lkn kocha haoni, km Ole ataendelea kuwa kocha tutegemee maumivu hata akiletwa Messi mwishowe ataonekana ni mchezaji wa Barca Tu na co tm nyngne.
Mkuu tushabadili makocha wangapi?
Hivi LVG Morinho sio makocha wazuri?

Jamaniiii, mchawi wetu ni Edwoodwad na mabosi wake, hao makocha tunawaonea tu.
Kwa timu kama Dortimund ama Bayan, hata kocha awe Mwambusi bado watapata matokeo mazuri tu.
 
Back
Top Bottom