Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Umeenda mbali sana, sio kubadili kikosi bali ni kumpata kocha bora ambaye ni mbunifu atakayevumbua na kuutumia ubora wa kila mchezaji uwanjani + Mbinu nzuri za kimchezo kama Arteta.
Hao wachezaji ndo walitupa Europa.

Ole akauza Herrera na Lukaku kisa hawafiti kwenye mfumo wake. Huo mfumo mpaka sasa haueleweki na hauonekani.

Leo hii anataka atafutiwe Striker wa kati wakati alimuuza Lukaku.

Ole aondoke kwanza.
 
Louis Van Gaal alisema

"Bayern ina CEO na watendaji ambao ni watu wa mpira, wanajua nini ni nini ila Manchester CEO alikua ni mwekezaji benki unaweza ona kwanini usajili hauchukuliwi serious"

Hapo Van Gaal alikua ni mhanga mwingine. Moyes alimsajili Fellaini ambaye miezi kadhaa mbele alikua anaenda kua free agent na market value ikiwa ni 23M ila bodi (Woodward) ikalipa 27M kumpata Fellaini.

Mourinho akaja na kutaka wachezaji 5. Kati ya hao 5 aliletewa Fred tu, kisha akasema anamtaka Maguire bodi (Woodward) akasema Maguire ni ghali sana kwa pesa iliyotajwa na kiwango chake hivyo waachane naye.

Otea ni beki gani amekuja kua ghali kuliko wote duniani....

So Mourinho akapigwa chini huku analalamika juu ya usajili. Kaja Ole, akauza striker akasema ana Rashford na Martial, hali ikawa mbaya wakafanya usajili kwa kupaniki wakamsajili Ighalo.

Familia ya Ighalo ilifanya sherehe baada ya kujua Ighalo kaenda Man U.

Kisha wakati wa usajili umefika timu inatafuta mabeki, wingers na viungo hakuna sehemu waliyosema wanahitaji striker ila kama kawaida mwisho wa yote lawama zitakuja kwa kocha na atatimuliwa aje mwingine.

System ya Man U ipo designed kufukuza makocha, tatizo la kweli ni kutokua na DOF nafasi ambayo Woodward aliifuta hiyo nafasi na kujikaimisha yeye. Na akasema hawana mpango wa kuajiri DOF.

Hii timu morali ipo chini, hili tatizo tulikumbwa nalo Arsenal chini ya Emery. Watu hawajielewi wanazomewa hawajiamini yaani vururu vururu naona Man U inapita same route na tayari hata mashabiki baadhi wanaamini Ole ana matatizo.

The system.
Unauza striker unataka uletewe striker.

It's not amount you spend, it's what you with the players you've got.

Mou alitupa Europa na haohao.
 
Mtu Kama Daniel James Ni wa caliber ya kuichezea utd ?

Mensah ?
Lingard ?
Jones ?
Kuna majinga jinga mengi Sana pale !!!!

Time will tell !!!

This time hata big sex Ni ya kupigania Sana !!!

Everton msimu huu Yuko vizuri , Carlo amesajili vzr na wameingia vzr kwenye mfumo !

Wovls wapo
Leicester wapo !!!


Bado
Arsenal
Liverpool
Man City
Chelsea
!! Kaz ipo Sana iseee !!!!!
Hao mbwa unaowaponda ndiyo walioitwa kina Cr7 wapya.
 
Mechi ya kwanza maneno yamekuwa mengi hivi.
Sioni sababu ya kumlaum Ole wala wachezaji kwani ligi ndo kwanza imeanza.
Eti arsenal nao wanaisema man u, Arsenal acheni vituko.
Wa ulivyo nyanyaswa na palace kwako Acha arsenal atambe tu.
 
OGS tunampenda ila Manchester United ni kubwa kuliko OGS
Naionea huruma timu yangu, mbele naona giza nene
Timu ina mapungufu baadhi ya maeneo ila sio kuzidiwa kila kitu na Crystal Palace ndani ya Old Trafold

Carlo Ancelot (CV) ukiangalia Everton inavyocheza ni mtu sahihi kupewa Man Utd, pia nampenda yule kocha wa Leeds ni mtu hatari sana kwa mbinu

Pia tukumbuke fundi Pochetino yupo bench anataka kazi
 
OGS
FB_IMG_16005902919120331.jpg
 
Jana ilikuwa siku mbaya, Ila niliangalia mechi nzima kiukweli mapungufu ni yaleyale ya Defence na striker. Pia hata kocha jana sikumuelewa maana ni kama vile alikuwa anafanya majaribio ya wachezaji,, na hata Degae hakuwa na kosa maana Defence ilishindwa kumlinda.

1. Kwa upande wa Bruno kutotengeneza nafasi ni kitu cha kawaida hata De bruyne na Jack grealish kuna mechi hawatengenezi nafasi na kukosa ujanja.

2. Kwa Rashford Makame na Antony martial pale wanajiangusha sana, na wamekosa competition ya kuwakarisha benchi hivyo tutegemee kuona wakiendeleza utoto wao.

3. Kocha jana aliniudhi ila sio kisingizio cha kufungwa mechi moja kwamba aondoke , maana matatizo ya Kocha wa Arsenal, Lampard na Ole ni yaleyale. Hata akija Klopp akapata wasaidizi wake wakawa Guardiola na Ancelloti bado siamini kama tutabadilika kwa hiyo bodi ya Man u.

4. Kwa kumalizia, mashabiki wa Man u tusiwe vigeugeu pale tunapopoteza mechi, maana nakumbuka ujio wa Bruno tulimsifu sana Ole kwa 19 unbeaten runs ambacho hakijafanyika for 7 years,, bali tuangalie wapi naye ajirekebishe maana Hiyo fukuza makocha kama Yanga it doesn't work pale Old Trafford.
 
Hao wachezaji ndo walitupa Europa.

Ole akauza Herrera na Lukaku kisa hawafiti kwenye mfumo wake. Huo mfumo mpaka sasa haueleweki na hauonekani.

Leo hii anataka atafutiwe Striker wa kati wakati alimuuza Lukaku.

Ole aondoke kwanza.
game moja ndio imeibua yote haya
 
Ubora wa wachezaji unatokana na kocha imara.

Kikosi cha Bayern hakina majina ya kutisha, ila mpira ukipigwa hapo utafurahi na roho yako.

Binafsi naamini tukiwa na kocha anayejua mbinu, hata hao kina Lingard watakichafua.

Sancho na wengine wakija, hakuna la maana watakalochangia kwa timu yenye kocha asiejua kuwatumia.

Tusifananishe rebuilding ya Klopp na ya Ole. Arteta na Lampard wanaonesha mwanga kuliko Ole.

Tuanze na kutafuta kocha kwanza. Wachezaji hawahawa lazima wakamuliwe vya kutosha.
Hebu ona ancelotti anachokifanya pale everton na wakati jose anatimuliwa kuna wadau humu walimpigia sana chapuo apewe timu cha ajabu mabosi wakampa mwanafunzi asiejua nini anachofundisha....acha tuteseke tu

Liva vs everton nasubiria hii game maana najua sie tutafungwa tu everton
 
Mimi binafsi kufungwa kwa chama langu nimefurahi sana. Kwa sababu naona kuna faida kadhaa tutapata kabla dirisha la usajili halijafungwa. Ya kwanza tutasajili wachezaji siyo chini ya mmoja, sancho uhakika. Vilevile naona jinsi martial na rashford watakavyotengenezewa competition mulemule, ataanza martial then rashford sub and vice versa is true, kitu ambacho ole na benchi lake la ufundi, lazima wamekiona. Mwisho ole nimwonavyo ni mnafki mwenye faida upande mwingine, ile timu imecheza kiboya vile usikute waliambiwa na kocha na benchi la ufundi, maana bila hivyo hakuna njia nyingine ya kuwashawishi board ya man utd, maana ni vichaa wale(kumbuka waliwahi muambia mourinho kuhusu kutokubaliana na hoja ya kumuuza martial kwa sababu wanamuona kama nacmento pele). Hayo ni mawazo yangu.
 
Unafungwa na crystal palace mbeleni kuna hawa pia mnaweza msiambulie point leeds utd wao funga 2 watafunga 3, funga 4 watakufunga 5.
Bado everton na wolves.
Kwa big 4 pale kama kawaida game zote huwa ngumu yeyote anashinda.
 
Najaribu kufikiria kama OGS asingekuwa mmoja wa kina Neville, Giggs, Ferdinand, Keane na wenzao, sasa hivi angekuwa anashambuliwa sana.

Timu mliyonayo siyo ya kufungwa kwa manyanyaso vile na Crystal Palace, hata kama ni swala la kwamba hamjasajili, timu iliyowafunga imemsajili nani?
 
Louis Van Gaal alisema

"Bayern ina CEO na watendaji ambao ni watu wa mpira, wanajua nini ni nini ila Manchester CEO alikua ni mwekezaji benki unaweza ona kwanini usajili hauchukuliwi serious"

Hapo Van Gaal alikua ni mhanga mwingine. Moyes alimsajili Fellaini ambaye miezi kadhaa mbele alikua anaenda kua free agent na market value ikiwa ni 23M ila bodi (Woodward) ikalipa 27M kumpata Fellaini.

Mourinho akaja na kutaka wachezaji 5. Kati ya hao 5 aliletewa Fred tu, kisha akasema anamtaka Maguire bodi (Woodward) akasema Maguire ni ghali sana kwa pesa iliyotajwa na kiwango chake hivyo waachane naye.

Otea ni beki gani amekuja kua ghali kuliko wote duniani....

So Mourinho akapigwa chini huku analalamika juu ya usajili. Kaja Ole, akauza striker akasema ana Rashford na Martial, hali ikawa mbaya wakafanya usajili kwa kupaniki wakamsajili Ighalo.

Familia ya Ighalo ilifanya sherehe baada ya kujua Ighalo kaenda Man U.

Kisha wakati wa usajili umefika timu inatafuta mabeki, wingers na viungo hakuna sehemu waliyosema wanahitaji striker ila kama kawaida mwisho wa yote lawama zitakuja kwa kocha na atatimuliwa aje mwingine.

System ya Man U ipo designed kufukuza makocha, tatizo la kweli ni kutokua na DOF nafasi ambayo Woodward aliifuta hiyo nafasi na kujikaimisha yeye. Na akasema hawana mpango wa kuajiri DOF.

Hii timu morali ipo chini, hili tatizo tulikumbwa nalo Arsenal chini ya Emery. Watu hawajielewi wanazomewa hawajiamini yaani vururu vururu naona Man U inapita same route na tayari hata mashabiki baadhi wanaamini Ole ana matatizo.

The system.
Mkuu me nadhan ole apewe muda.. hiv unajua klop katumia miaka zaid ya mi nne kuijenga hii team.....? Watu wanamlaumu ole bure tu
 
OGS tunampenda ila Manchester United ni kubwa kuliko OGS
Naionea huruma timu yangu, mbele naona giza nene
Timu ina mapungufu baadhi ya maeneo ila sio kuzidiwa kila kitu na Crystal Palace ndani ya Old Trafold

Carlo Ancelot (CV) ukiangalia Everton inavyocheza ni mtu sahihi kupewa Man Utd, pia nampenda yule kocha wa Leeds ni mtu hatari sana kwa mbinu

Pia tukumbuke fundi Pochetino yupo bench anataka kazi
Watu wanamsifia arteta kisa kashinda games 2 .. kwan ole hajawah shida games 5 mfululizo...?
 
Ole apewe muda unbeaten run 19 matches watu wamesahau
Najaribu kufikiria kama OGS asingekuwa mmoja wa kina Neville, Giggs, Ferdinand, Keane na wenzao, sasa hivi angekuwa anashambuliwa sana.

Timu mliyonayo siyo ya kufungwa kwa manyanyaso vile na Crystal Palace, hata kama ni swala la kwamba hamjasajili, timu iliyowafunga imemsajili nani?
 
Back
Top Bottom