Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mashabiki wa Man youu ni empty kabisa. Leo baada ya kutunguliwa magoli 3 na chelsea wanakuja na vioja kuwa wanajiandaa na UEFA yaani FA haina adhi kwao

Sasa msichokijua ni kwamba FA Cup ina mpunga mkubwa kuliko la Ligi.

Pia advantage yake ni kuwa ukishinda unacheza Uropa. Je vip wewe ukikosa top 4 na Uropa ukose utacheza hiyo UEFA?

Kama kombe halikuwa la muhimu kwann sosha ameingiza mastaa?wote?

Na vipi mngefunga chelsea haya maneno mngeyasema kuwa tunajiandaa na Uefa? Sipati zile tambo zenu.

Nashukuru Chelsea IMEWAZIMA Midomo hamna cha kusema tena. Mmebakini na visingizio vya ohoo Uefa

Man U 1 vs Chelsea 3

Tambo zote kwishineiiii.
 
Mimi nimeongea kwa vigezo na nikakutajia, United hawajapaki basi, tumegawana vipindi na Chelsea, wao wamecheza kipindi cha kwanza, sisi tumecheza kipindi cha 2

Kikosi chetu cha kwanza ni bora sana, kikicheza chote kwa kuanza na kumaliza hata mechi ya leo tungeshinda bila kutumia nguvu nyingi

OGS kajaribu ku manage injury na fatigue ya wachezaji kutokana na mbio za top 4, na haya ndio matokeo yaliyopatikana

Bado CV ya Arsenal na Spurs ya Mourinho hamuachani
This is one of the worst excuses of Man Utd fan. Kwa sisi tumechezesha kikosi chenyewe mkuu? Mkuu kubali tu nimekuzidi ubora mbali sana
 
Ndugu, goli la Mount nakubali Degea katoa zawadi lakini goli la kujifunga la Maguire, kasi ile na krosi ya Alonso beki yeyote angejifunga
Goli la kwanza la Giroud ni Master class, iliminywa kwa haraka bila ya Maguire kushtuka kinachotokea
Ule ni uzembe.

Alilegeza mguu mpira ukamgonga ukaingia.

Angekuwa Baily kusingekuwa na uzembe wa aina ile.

Maguire anafanya makosa ya wazi kabisa.
 
Kuna mambo yanashangaza sana, kikosi kilichokuwa na akina Phil Jones, Valencia, Ashly Young na Lingard mlitaka kichukue UEFA chini ya Mourinho, ila baada ya sajili kubwa zote , mnapigania kuingia nne bora huku wale pundits uchwara wakiwa wamefunga midomo. Unafiki ni kitu kibaya sana.
Tunaingia top 4 ila hatuna timu ya kupambana UCL.

Tunaenda kutia aibu tena.
 
Kuna mambo yanashangaza sana, kikosi kilichokuwa na akina Phil Jones, Valencia, Ashly Young na Lingard mlitaka kichukue UEFA chini ya Mourinho, ila baada ya sajili kubwa zote , mnapigania kuingia nne bora huku wale pundits uchwara wakiwa wamefunga midomo. Unafiki ni kitu kibaya sana.
Mourinho tulishamfukuza kazi bro mfuate huko aliko.
 
Hapa sina haja ya kubishana

Ukweli wa Man Utd ulionekana baada ya Pogba, Martial, Greenwood kuingia

Usitake kuniambia majembe yenu mnayoyaaminia ni akina Tomori, Abraham
This is one of the worst excuses of Man Utd fan. Kwa sisi tumechezesha kikosi chenyewe mkuu? Mkuu kubali tu nimekuzidi ubora mbali sana
 
Angali kocha wenu alivyo maskini, anategemea LFC au Chelsea waboronge ndio nyie muingie top 4, poor MANURE

Solskjaer on the race for the top four

It is between us, Chelsea and Leicester for those last two positions, the more help we get from others the better, of course, but we know we must do our job on Wednesday.
 
Jose Mourinho comments on David De Gea a year ago prove he was right
Jose Mourinho stated that David de Gea was 'lucky' to be handed a mega-money contract by Manchester United in September last year and it seems that the Tottenham boss was on the money
 
Kati ya epl na FA kombe lip linampunga? Panga kwanzia UEFA na kushuka ukijumlisha supercup, club bingwa..

EPL bingwa anachukua around £150m, ingawa hapishani sana na mshindi wa pili, na wakati mwingine namba mbili anaweza kuvuta zaidi ya bingwa, kuna vigezo.

UEFA hawachezi mbali na £80 - 90m.

Europa sina uhakika, mpaka kucheki kwenye mitandao.

FA ni around £3.5 mpaka 5m.

Hizo supercup pia sina uhakika lakini haziwezi kufika £1m.
 
Mkuu kama mpira utachezeshwa fair kama alichofanya refa wa jana wewe hauna uwezo wa kunifunga mimi! Mara zote uliponifunga wewe pamoja na jamaa zako mnakuja jukwaani kusumbua na siyo huko tu Whatsapp, Instagram na Twitter huwa kunachafuka. Mtaani ndio hatuna amani ni kejeli na matusi wiki nzima.

Lakini sisi tumeshinda huu utani hauta chukua zaidi ya siku mbili tunawaza mbele.
Mkuu huoni vurugu hizi mnazoleta huku?? Jamaa yako mzee wa kujipiga BAN Ollachuga Oc kaweka kambi hapa.

Lakini tuongee Ukweli, unataka kuniambia mara tatu zote nilizokupiga nilisaidiwa?? Mimi nakubali jana mmetufunga kutokana na uzembe wa Kocha, Magwaya na De Gea, ila hamna kikosi cha kutufunga tukikamilika.

Anyways, hongereni mmeshinda isingekuwa vizuri mpoteze mara nne ndani ya msimu mmoja kwa timu moja.

Tukutane top 3, nani ataingia kule.
 
Back
Top Bottom