tumeamua kujificha zaidi kwenye hoja ya uchovu uliosababishwa na mapumziko mafupi tulioyapata baada ya kucheza na crystal palace, labda ni kwa sababu ni jambo rahisi zaidi kuliongelea kuliko tactics, set up ya timu, team choice, aina ya wachezaji tulionao na style yetu ya kiuchezaji.
kwa kuweka kumbukumbu zetu kwa usahihi ni mason greenwood, pogba na martial ndio walianzia benchi kwenye mechi yetu ya jana kwa wachezaji wa kikosi cha kwanza baada ya corona.
tukirudi nyuma Southampton kabla ya mechi yetu ndani ya siku sita walicheza na manchester city pamoja na everton na zote hizo ni team zinazocheza vizuri sana, soton hawana kikosi kipana kama sisi hivyo basi kwa kiasi kikubwa unakuta wachezaji wao wa kikosi cha kwanza wanacheza kwa dakika nyingi (lack of rotation) , kilichotokezea kwenye mechi ile wao walicheza vizuri zaidi kana kwamba wana kikosi kikubwa kutuzidi sisi.
hata kwa upande wa chelsea nao walikosa huduma ya pulisic na ngolo kante ambao wote ni wachezaji wa kikosi cha kwanza lakini bado walionekana kuwa vizuri zaidi kiuchezaji kuliko sisi,
kwa ufupi timu yetu inasumbuliwa na matatizo mawili makubwa sana ambayo hatupendi kuyazungumzia.
- tunateseka mno tunapocheza na timu zinazojilinda (two blocks) hatupigi cross, hatuingii kwenye eneo la adui kiurahisi, rejea mechi yetu ya spurs kwa raundi ya pili na mechi zetu nyingi tulizocheza round ya kwanza ukiondoa ile ya chelsea (ile mechi walicheza kama kundi la walevi)
- tunateseka zaidi na zaidi pindi tunapocheza na timu zinazo pressing: na hili tatizo limeendelea kuwa sugu zaidi na limeshakosa tiba na litaendelea kutusumbua, rejea mechi zetu na liverpool, manchester city, southampton (mechi zote mbili)
tofauti na manchester city (guardiola ni mwanadamu anayeishi na fikra zisizobadilika) , jana chelsea waliingia uwanjani huku wakiwa wameyafahamu fika matatizo yetu hayo mawili hivyo basi walihakikisha wanajilinda vizuri ( didn’t exploit their space ), pia wanatupa presha muda wote (kovacic ameendelea kuwa ni master wa kuzivunja timu pinzani) bila ya kusahau pressing in the final third wakiongozwa na giroud (muda mwingi alisababisha defence line yetu ivunjike)
ukicheza hivyo tu basi baadhi ya wachezaji wetu ukimuondoa nemanja matic wanakuwa clueless, panicky, lacking calmness under pressure na bahati mbaya zaidi hili tatizo hata benchi letu la ufundi nahisi wameshindwa kulifanyia kazi.
our pressing return imeendelea kuwa ni poor dhidi yao, Too often passes were misplaced, wachezaji wetu wanalose possession ovyo (
wan bissaka anaongoza kulose possession and poor ball control) na hatimaye tunakosa mtego sahihi wa kuwawekea maadui (tunajificha kwenye failure counter attack)
kwa mfano
- mechi yetu ya mwanzo dhidi ya southampton tulilose possession mara 183 na mechi yetu ya marejeo dhidi ya hao southampton tulilose possession mara 141, ina maana benchi la ufundi walishindwa kuja na mbinu sahihi ya kuondokanwa na hilo tatizo
- United’s passing accuracy kipindi cha kwanza dhidi ya soton ilikuwa ni 81% lakini kipindi cha pili ilikuwa ni 71%
Swali la kujiuliza laiti kama tungelicheza na timu mfano wa cystal palace, aston villa, bournermouth na nyenginezo tungelicheza mpira ule wa jana kwa hoja ya uchovu?
sidhani
====================================
Sevilla wanatusalimia kwenye michuano ya Europa, kinyume chake tuombe watolewa na AS ROMA (tunalihitaji lile kombe)
marcelo bielsa amerudi (wengi wetu tunaikumbuka ile adhabu aliyotupatia akiwa atletico bilbao, waliokuwa hawajazaliwa kwenye soka kipindi hicho basi kamtafute iker munian, ander herrera wa siku ile na llorente).
klopp bado yupo
Southampton bado wapo na mjerumani
arteta msingi wake umeshaanza kukaza nadhani tumeiona pressing na rebuilding ya arsenal mechi za karibuni (goli la juzi waligusa mpira takribani mara 30)
tuendelee kujificha kwenye mfumo wa 3-4-3 au 3-5-2 huku tukiendelea kulipuuzia tatizo kubwa zaidi.
GGMU
===================