Kuanzia mechi ya tarehe 11/8/2019 tulipocheza na Chelsea hadi tarehe 06/10/2019 tulikuwa na midfielder 4 waliopo fiti ukijumlisha na Pereira lakini OGS ali prefer hiyo formation ya kutumia midfielder 2 na si 4-3-3
Kwa mechi 4 za awali ambazo Ole aliitumia mfumo wa 4-2-3-1 Ole hakumweka Fred hata benchi, means ana viungo wa kutosha. Mechi ya kwanza Ole anamweka Fred kikosini, sio first eleven, ilikuwa ni September 14 (hapa bado hakuwa fiti kwa mujibu wako)
Huyo Fred akaanza kupata namba 06/10/2019 dhidi ya Newcastle (kwa mujibu wako hapa ndio akawa ana fitness) na Matic ghafla akapoteza fitness, akapoteza namba hivyo akawa anaanzia benchi, maana mechi ya Newcastle hakuanza lakini alikuwepo benchi
Kama nilivyosema awali United imekuwa na viungo 3 walio fit au zaidi mara nyingi sana hivyo suala la OGS kuchezesha mid 2 badala ya 3 ni uamuzi wake na si kwa sababu hana viungo. Narudia tena pia kuwa, kuchezesha mid yoyote iwe 2 au 3 haiifanyi timu kupata matokeo mazuri. Timu inapata matokeo mazuri kwa kuwa na wachezaji wazuri na coaching nzuri.
Unasema Maguire alikuwa fit ndio maana yeye alianza direct kwenye kikosi cha United. Narudia tena kwamba fitness ya Maguire haiwezi ku tofautiana na Fred, pengine Fred alikuwa fit zaidi.
Pre season ya Fred alicheza mechi 4 kama Maguire, pre season ya Fred alicheza dhidi ya Inter Millan, Tottenham, Kristiansund na Ac Millan wakati pre season ya Maguire alicheza dhidi ya Scunthorpe, Cheltenham, Cambridge Utd na Stoke City (ukiacha Stoke City ambayo nayo ni ya 21kwenye msimamo kati ya timu 24 za Championship, team hizi nyingine ni team flani za mchangani, ndizo Maguire alizojipima nazo pre season na zikamfanya awe fiti kuliko Fred aliyejipima na wababe wa Ulaya

Mara ya pili tena nakwambia mpira wa miguu si playstation, mchezaji alieumia siku 76 almost miezi 3 huwezi tegemea kapona tu ukamchezesha, even hizo under 23 ambazo wachezaji wanacheza kuregain fitness hawamalizi dakika 90 kabla ya mechi ya liverpool dalot hajacheza mechi hata moja ya Epl january ametoka majeruhi wewe kama kocha ungempiga benchi bissaka na kumpanga dalot?
Matic yupi mkuu? Huyu alieumia kuanzia mwezi wa 10 mpaka wa 12 na kumiss mechi 14? Ama kuna matic mwengine? Fred aliporudi kwenye kikosi Matic nae akaenda hospitali.
Mfano wa hio mechi?
Mkuu kuna kitu kikubwa unachanganya hapa
-match fitness
-kuzoeana na wachezaji wenzako.
Maguire alikuwa match fit anajiunga man utd tayari yupo fit, ameshiriki pre season ya leicester na amecheza mechi za kirafiki.
Fred yeye hakuwa fit, alivyokwenda pre season alikuwa akitrain mwenyewe means alikuwa na fitness ndogo sana.
Ni kama situation ya sasa, bruno ni match fit amekuja kikosi cha kwanza moja kwa moja ila Ighalo anahitaji wiki mbili hadi mwezi sababu gombea goli wanalocheza china sio Epl.
Ole anamsifia fred, Fred anamsifia ole wanapendana na dressing room yetu yote ni kitu kimoja ila wewe mzee upo huku unajua zaidi na kutoa kashfa.
Na ndio kazi ya shabiki kuwa nyuma ya Kocha na wachezaji hata kundi kubwa kabisa la mashabiki la Red Armies hio ndio motto yao, sio kazi ya shabiki kumfundisha kocha na kuponda kila anachofanya.
Nilikuwa nyuma ya LVG, mou na hata ole, watapata support yangu popote pale mpaka siku watakapokuwa hawahusiani na Man utd.
Sent using
Jamii Forums mobile app