Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Bruno hatakuwepo kwenye match day squad ya Sporting CP jumatatu, kwa asilimia kubwa tutamsajili

Lakini, chini ya Ole hamna cha maana tutakacho improve

Hivi kumfunga Burnley unahitaji uwe na BF? Hivi kucheza mpira unaoeleweka unahitaji usajili mkuuuubwa kiivyo hii January?

On paper ni Wachezaji wangapi wanaingia first 11 yetu kutoka Sheffield United, lakini mbona mpira wa Sheffield unaeleweka kuliko wetu, Ukiangalia mpira wetu unategemea individual brilliance kuliko team brilliance

OGS anajificha kwenye kichaka kinachoitwa rebuild, patience, United way

Hivi Rodgers mbona alihitaji mwezi 1 tu, kubadili uchezaji wa Leicester........ Ole anaomba miaka 4 kama Klop, laughable

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi mbona unakuwa na hype ya Bruno kuja ilihali hakuna kocha?
Unadhani Bruno ni standard yetu? Aende timu zinazojielewa kama Halland.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
duh! kumbe mjomba ole gunnar ameshasafisha wengi sana klabuni kwetu, huyu jamaa anastahili kupewa muda mrefu wa kujenga timu.

  1. antonio valencia
  2. Marouane fellaini
  3. Ander Herrera
  4. Matteo darmian
  5. romelu lukaku
  6. Ashley young
  7. Alex Sanchez
  8. Chris smalling
what next?
Ander Herrera? Lukaku?

Unamuacha Jones, Lingard.

You must be smoking weed.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Daemusin,naunga mkono hoja yako kulingana na target za Ole tangu amekuja OT.
Kwanza kabisa sajili zake 3 za mwanzo alisajili damu za malkia ingawa kwa kipindi hicho kulikuwa na option bora zaidi ya hizo. Maguire dhidi ya Koulibaly,James dhidi ya Ziyech. Kulikuwa na ushaidi mkubwa kuwa chaguzi mbili zilizoachwa ndio zilikuwa/ni bora kuliko tulioletewa. Utetezi wa Ole ukawa ni kutafuta DNA ya united.
Pili hata targets tunazohusishwa nazo hadi leo hii zimekuwa na asili ya uingereza kama vile Sancho, Madison, Grealish. Eriksen amekuwa sokoni kwa bei ndogo kabisa na ni mara mia ya lingard,ila kama ole hajamuona walau kumtumia kwa miezi iliyobaki tu.
Nina imani Ole anatafuta kupendwa na waingereza kwa kulundika waingereza wengi kwenye timu bila kuzingatia ubora.
Kwenye media amekuwa optimistic kuwa wana improve wakati kila mtu anaona mapungufu ya waziwazi kwa kila mchezo tunaocheza.
Just imagine.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bavaria,
Bruno hata asije United. Ataharibika kama kina DiMaria

Umeongea ukweli mtu hapo ktk hii comment yako. Mimi narudia tena kusema kama tunataka kuiokoa timu yetu, tuwaangalie upya wale watu waliopo corner offices yaani the board running Man United, especially the executive vice chairman Ed Woodward (He's the one responsible for overseeing the club's operations), who think they can solve any problem by just throwing money.

Hii ndo ilikuwa comment yangu Jan, 10. #124,779

Muda ni mwalimu mzuri sana kuna siku watu watakuja kuelewa kuwa tuna-fix tatizo pande mbili tu tunasahau eneo la muhimu zaidi. Timu imejikita ktk wachezaji na bench la ufundi toka Ferguson amestaafu mwaka 2013 tumebadili wakufunzi 5 mpaka sasa na tumetumia pound sterling 840.15 million kununua wachezaji tumezidiwa na Manchester City tu. Ndani ya hii miaka sita iliyopita tokea Ed Woodward awe football executive rasmi kama executive vice chairman akichukuwa nafasi ya David Gill timu nyingi zimefanya vizuri kuliko sisi kwa budget pungufu kuliko yetu kwa vipindi tofauti kuanzia Leicester, Chelsea, Liverpool na Spurs(Hawa wame-maintain big 4 kwa misimu 4 mfululizo sisi tumeingia mara 2 kwa miaka 6).

Hoja yangu hapa matatizo yetu sisi ni zaidi ya bench la ufundi na wachezaji, kwanza tunahitaji viongozi wenye uelewa mpana wa masuala mpira ambao wana-track record ya kuendesha vilabu vikubwa vya mpira sisi tunawakosa wanaoweza kufanya maamuzi faster na kwa wakati sahihi endapo mwalimu atahitaji mtu. Tunakosa msuka mipango mwenye uelewa mpana sana wa soka na anayejua kusoma alama za nyakati na kwenda sambamba na upepo unavyovuma.

Kwa sasa hata tumlete Messi na Ronaldo wata-struggle tu. Ni ukweli mchungu ila ndio hali halisi, Siku ambayo viongozi (hasa hasa familia ya Glazer) watakapoukubali huu ukweli kuwa nafasi ya Ed Woodward hahitaji ushikaji ndo tutarudi ktk ubabe wetu wa siku zote. Tuna option mbili either Ed to leave the football decisions to someone else with extensive experience in the running of a football club, that person should then sit on the Board as independent director or Ed akae pembeni au arudi kuwa commercial director kama zamani nafasi yake ichukuliwe na mtu anajielewa.
 
Ila tusijilaumu sana kumkosa Haaland na hata Bruno asipokuja sawa tu mana hakuna haja ya kuwaleta talented players ilihali uwezo Wa kutumia na kuendeleza vipaji vyao hatuna. Kocha aliyepo hana uwezo Wa kutumia vema na kuendeleza kipaji cha mchezaji. Bodi imejaa mijitu ya hovyo ambayo haijali maendeleo ya timu ndio mana inaona ni sawa tu kuendelea kuwa na mwalimu Wa bei ndogo asiyejua kufundisha mpira na kufanya sajili za kisengesenge.
 
IMG_7544.JPG



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ila tusijilaumu sana kumkosa Haaland na hata Bruno asipokuja sawa tu mana hakuna haja ya kuwaleta talented players ilihali uwezo Wa kutumia na kuendeleza vipaji vyao hatuna. Kocha aliyepo hana uwezo Wa kutumia vema na kuendeleza kipaji cha mchezaji. Bodi imejaa mijitu ya hovyo ambayo haijali maendeleo ya timu ndio mana inaona ni sawa tu kuendelea kuwa na mwalimu Wa bei ndogo asiyejua kufundisha mpira na kufanya sajili za kisengesenge.
Itafika muda mtazoea tu...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samahani lakini kama hii habari ni ya ukweli mkuu Financial Analyst ,ni kwanini wamechagua dakika ya 58?
Dak ya 58,hii inatokana na ile ajari ya ndege kule Muninch iliyotokea tarehe 6 feb 1958

Kwa hyo wamechukua hyo namba ya 58 ikiwa kama kushinikiza na bado pia itakuwa ni wiki ya kumbukumbu ya ajari hyo.
 
Back
Top Bottom