Alichosema G.Nevil kuhusu rebuild ya United
United wanaelekea uelekeo sahihi licha ya matokeo mabaya wanaopata na watakayopata siku za mbele. Ukiwatazama kwa sasa wana timu ya vijana wadogo wenye njaa, wengine wanasajiliwa na wengine kutoka mfumo wa timu ya watoto (academy)
Anachofanya OGS kwa sasa ndicho alichofanya SAF kipindi anatoka Abarden kuja United. Wakati anachukua timu, alilenga kuleta utamaduni mpya kwenye timu changa anayoijenga. Pamoja na kukuta baadhi ya wachezaji wenye vipaji kama Paul McGrath na Norman Whiteside aliamua kuwaondoa ili kuleta sura mpya ambazo zina vipaji lakini zinaendana na kile anachotaka kukianzisha klabuni. Si ajabu sasa OGS amewaondoa Rom, Sanchez, Valencia, Smalling n.k. Na dalili zinaonesha kuna wengine wataondoka madirisha yanayofuata.
Ni ukweli usiopingika kuwa, Pep alipofika City alikuta timu nzuri lakini alihitaji kati ya madirisha 3 na 4 ya usajili kujenga kitu anachotaka kujenga. Kwa upande wa Klop alihitaji kati ya miaka 3 na 4 kujenga timu yenye taswira ya falsafa zake (kwa wale msiopenda kujenga hoja kwa kutaja mifano ya timu nyingine, mtanisamehe hapa


)
Usajili wa Wan Bissaka, Maquire na Daniel James unadhihirisha adhma ya OGS kujenga timu kwa taswira/falsafa yake. OGS Anachofanya anahitaji muda, na akipewa muda ataleta mapinduzi ya kiuchezaji ndani ya United, kwani hata sasa timu inaonesha kucheza kwa style inayoeleweka.
Kikubwa OGS anachohitaji ni kupewa muda na Board