1. Kuna tier system kwenye uvumi/taarifa na Kuna waandishi ambao Ni official wa club wanapata taarifa direct toka kwenye club, mfano Ni huyo Cooper niliemtaja kuhusu issue ya ole, hivyo si Kila mwandishi Ni uvumi wa Twitter wengine maneno Yao yana uzito zaidi.
2. Tuje kwenye budget ya timu.
Club za mpira wa miguu haziendeshwi Kama serikali ama kampuni nyengine, ukipewa budget kiasi kadhaa unaweza ukaiongeza hio budget kwa kuuza wachezaji, kusema kwamba hela ya mchezaji ulioiuza inaingia mwaka mwengine si kweli. Club za mpira Zina wachezaji fixed hawazidi 30 hivyo unapopewa let's say 50M kuspend inamaanisha unatakiwa kuongeza hio value on top of current value, inapotokea current value imepungua inabidi uiongeze.
Chukulia mfano wa duka, una duka lenye bidhaa za milioni 5, na ukauza bidhaa za milioni 2, bosi wako akakuongeza milioni 1 ya kununua bidhaa zaidi,
Je utarudisha milioni 2 kwa bosi na kuchukua ile milioni na kushusha thamani ya duka hadi milioni 4, ama utarudisha zile milioni 2 dukani na ile milioni 1 na kupandisha thamani ya duka?
Unapoona hizi deals sijui Adidas, Mara Chevrolet, na wengineo, nyingi thamani ya hizi deals zinazotokana na thamani ya club, hivyo Kila mchezaji anapoondoka thamani ya club inapungua, na inabidi hio hela itumike kuiongeza thamani iliopungua.
Kuhusu Arsenal nisiwaongelee Sana sababu sifuatilii habari zao ila usisahau Peter cech, Ramsey, beki wao sijui ndio koscienly, welbeck, Denis suarez, etc Kuna wachezaji takriban 10 wameondoka, hao wote sitashangaa Kama Arsenal wamefree zaidi ya 50M kuspend kwenye wachezaji wapya, ambao watakuwa na values kubwa Huku wakilipwa mishahara midogo.