Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

At least wewe umeongea , sio hawa wanaoponda mchezaji mmoja.

Tuna wachezaji zaidi ya 6 kwenye first 11, ambao hawawezi kuanza kwenye timu inayoshindania makombe. Smalling, matic, herrera, young, lingard, etc.

Kule Right wing kumekufa kabisa, mashambulizi yetu yote yanapitia upande wa kushoto( hii kitu inanifnya sometime nashindwa kumlaumu martial), tuko predictable.

Kwenye midfield , matic ameisha yuko slow, yaani slow kutoa pasi za haraka, pia slow kusaidia kwenye attacking. Kinachosikitisha mbadala wake ni MCT.

Herrera, workrate yake ni nzuri but kipi kingine anacho offer.

Lingard, midtable team player.

Ili kucompete na best teams, tunahitaji best player(world class players) , sio hawa tulionao.

Summer signings
CB
Fullback
Rw
CDM , hawa ni must, tukishaleta hao ndio tulete wachezaji wakucompete Numbe ,ili waliopo wasibweteke.

Angalia Man city ,leroy sane akizingua sterring anachukua namba, mahrez akizingua ,sterring au bernado silver wapo. Hivyohivyo hata position nyingine.

Sasa ukija Man U, first11 tu ni ovyo ovyo.

Unabaki unajiuliza miaka yote hiyo tulikuwa hatusajili?. Unakumbuka kuwa kila kocha alikuwa anasajiri anavyopenda yeye, sio kulingana na falsafa za timu.
Kocha akiondoka wachezaji hao hawafai tena.
Hapa ndipo unakumbuka Ed woodward alituahidi DOF. Lakini hadi sasa kimya.



Sent using simu mbovu
Aliwaahidi lini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado nakuuliza swali hapo iyo mipango yao na morali imewafanya washike nafas ya ngapi kwenye ligi???

Sent using Jamii Forums mobile app
Wolves iliponunuliwa na wachina akakabidhiwa Mendes (wakala) alete wachezaji ambao timu nyingine watawanunua.

Target yao siyo makombe wala UEFA target ni kuhakikisha timu haitoki kwenye ligi tu. Ndiyo maana wachezaji wote wa Wolves mpaka kocha wakala wao ni Mendes

Swali lako halina maana.

Yaani umefungwa na timu ambayo haina hata haja ya kuchukua hilo kombe alilokutolea.

Piga mbuzi hao
 
Y
Bora yako wewe uliona kilichoendelea,,,
Kipind cha pili mambo yaliharibika baada vijana kuanza kupoteana na kujikuta wanapoteza mipira ovyo na kuruhusu mashambulizi! Ni kosa LA kiufundi lililochangiwa na uzembe wa wachezaji

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaah ilikuwa game nzuri tu tuli relax na kuona tutatapa bao muda huu mara muda ule
 
Kwa Kiasi kikubwa yamepungua Kama Sio kuisha yote.

Tatizo lilikuwa uwepo wa Mourihno.

Licha ya kutupa Kombe la UEFA Ndogo na kuturudisha Katika nne bora kushiriki kucheza UEFA.

Soka lililochezwa uwanjani halikuwa la kuvutia, timu ilicheza Mpira mbovu mno, haikuwa Man United tuliyoizoea Au kuitegemea.

Wachezaji walilalamika, Mashabiki tulilalamika, binafsi sikuwa Mpenzi wa soka la Mourihno hata Kidogo.

Tulipishana Katika Falsafa, Mi ni muumini wa soka la Ufundi na uwazi, la kushambulia kwa Kasi na wachezaji kuwa huru kuonyesha uwezo wao binafsi.

Soka la Mourihno lilijaa mbinu ngumu mno, Falsafa ya kukaba Muda wote Ndio iliyotaka kuwapoteza wachezaji wazuri.

Mikhtaryan ameflopy kwa sababu ya Mou, Rashford alilazimika kutumia Nguvu nyingi kuliko akili uwanjani, Martial ye yalimshinda akaanza kulalama sambamba na Pogba.

Tatizo lilikuwa kwa Kocha (Mourihno), wachezaji walilalamika kuhusu Mbinu zakena mifumo aliyotumia uwanjani.

Tuliowaona hata Ma legend wa timu wakikosoa Mbinu zake.

Alitengeneza uwadui kwa Wachezaji na kwa Ma Boss wa Timu, vyombo vya Habari.

Mourihno alikuwa kivuruge Kweli Kweli pale Carrington na Old T.

Alitunyima radha ya kuwa shabiki wa Man United.

Zaidi hakutaka kuziishi Falsafa za Man United, kuwa pale Old T inaanza Man United kisha SAF.

Alitaka kuwa zaidi ya Klabu.

Alitumia zaidi ya pound 400m kukisuka kikosi chake.

Hakuwa Manager Mzuri kote alipopita, Pale Real Madrid pia ilikuwa hivihivi.

Hizi ni timu kubwa zenye mashabiki wa kutisha zenye Falsafa zake.

Alishindwa kutofautisha Kati ya Man United/Rwal Madrid na Chelsea.

Na hata alipokuwa Darajani alikumbana na matatizo ya namna hii.

Sio Muumini wa wachezaji wenye vipaji/Makinda na Sio Muumini wa wachezaji Mastaa, alishindwa kubalance timu/Club.

Kuondoka kwa Mourihno pale Man United kumekuwa na Kheri kubwa kuliko angeendelea kuwa Kocha wetu.

Huyu Mourihno Ndio aliyetaka kutuaminisha hawa akina Mata, Lukaku, Salah, De Burnye, Sterrling kuwa Sio wachezaji wazuri.

Kwangu naamini kumfukuza Mou Klabu imeshusha Mzigo mkubwa sana.

Chini ya OGS hatuwezi kushinda match zote lakini match ambazo tunatakiwa kushinda nina uhakika tutashinda kwa Kishindo Sio kwa kinyonge kwa soka tunalocheza sasa.

Tulianza kufungwa na wajinga wajinga tena hapa hapa Old T.

Tukaanza kuvihofia hata hivi vitimu vidogo, tufungwe na timu Ndogo lakini iwe kwa bahati mbaya, tulikuwa tunafungwa kwa Shida hata Kama hatuchukui ubingwa.

Tulianza kudharaulika, lakini Sasa nina imani hata PSG wataanza kutuchukulia kwa umakini.

#Kheri ya Mwaka Mpya.





Sent using Jamii Forums mobile app
Can you say something?
 
Glazers +Woodward are very smart (in business & management )until now most United fans dont know whats wrong with their team they make us believe the problem was manager and solution was to sack him now we trying hard to find the new excuse
jambo moja kubwa ambalo washabiki na wapenzi wa manchester united tunapaswa kushukuru ni kushuhudia timu yetu imewahi kufundishwa na mwanadamu ambaye si mnafiki linapokuja suala lenye maslahi na kazi yake.
achana na madhaifu yake ya kujifanya ni msafi kwa kila jambo analoliamini lakini jamaa kwa kutumia mdomo wake usio ishiwa maneno ndiye aliyetuwezesha kufahamu kiundani madhaifu ya uongozi mzima wa manchester united.

huwa napenda kuzipitia comment zote za wachangiaji ili nipate kujifunza kwa sababu sijakamilika lakini ukizisoma hizi comment wengi wao wanarudi pale pale kwenye msimamo wa jose mourinho ambaye tulimuona shetani hata kwa lile ambalo lipo sahihi.

  1. kuna baadhi ya wachangiaji wanasema hatujawahi kusajili winga wa kulia kwa miaka 5, nadhani watakuwa wamepitikiwa kibinadamu kwa sababu chini ya david moyes tulimsajili wilfred zaha, chini ya LVG tulimsajili memphis depay, dimaria baada ya kumuona wilfred zaha hafai. Ukiifuatilia hii cinema kwa umakini ndio tunarudi pale pale kwenye mijadala yetu ya kila siku ya kwamba tulikuwa tunasajili na kuuza kwa kusikiliza zaidi porojo za walimu hata kama hawapo sahihi.
  2. alipokuja msema ukweli jose mourinho baada ya miezi kupita akamwambia ed woodward ya kwamba memphis depay bado hajawa na uwezo wa kucheza ligi ya uingereza kila wiki hivyo namhitaji ivan perisic wa inter milan, mpaka jose anaondoka hakuwahi kuletewa winga wa kulia.
  3. katika harakati zake za kujenga timu jose mourinho hakuvutiwa kabisa na juan mata lakini bodi ya klabu ilikataa kumtafutia mbadala, cha ajabu leo hii ndio kuna mashabiki ndio wanagundua udhaifu wa juan mata na wenzake.
  4. sitaki kuzungumzia ishu ya martial na jose mourinho kwa sababu sote tunafahamu jamaa alikuwa tayari hata kufanya swap deal dhidi ya willian wa chelsea, baada ya kumshuhudia jana martial akicheza ndio nimegundua jamaa alikuwa sahihi kumweka benchi antony martial na hata kumuondoa.
  5. sitaki kuzungumzia ishu ya walinzi wa kati ili nisiwachoshe, kwa sababu bado tunaendelea kuteseka licha ya jose kutokuwepo.

kama kweli united wana fedha kama wanavyojisifia zinapotolewa repoti za mapato mbona tunakimbilia kuwapa mikataba kina ashley young, jones, mata wakati wenzetu wanawatafuta mahrez, walker, sterling n.k.
Yote hayo jose alishayazungumza mara kwa mara lakini hatukumuelewa wengi wetu.
Tumuombe mungu kocha ajaye asiwe mnafiki ili aweze kuyapigania maslahi ya ukweli ya klabu la si hivyo tutashihudia tena dhoruba yenye maumivu.
mara paaaap matteo darmian, valencia wanapewa mikataba mipya huku man city wanamsajili ndombele na wanamrudisha jordan sancho.
 
Aliwaahidi lini?

Sent using Jamii Forums mobile app
vugu vugu la jose mourinho ndio lilimshajihisha ed woodward na familia ya glazer waone umuhimu wa kutafuta DOF, na mpaka muda huu hakuna aliyetangazwa mshindi wa nafasi hiyo.
kama tutashindwa kupata DOF kwa muda muafaka kuna hatari ya kuendelea kuteseka dirisha lijalo la usajili chini ya ed woodward a.k.a mzee wa biashara kwanza.
 
Wolves iliponunuliwa na wachina akakabidhiwa Mendes (wakala) alete wachezaji ambao timu nyingine watawanunua.

Target yao siyo makombe wala UEFA target ni kuhakikisha timu haitoki kwenye ligi tu. Ndiyo maana wachezaji wote wa Wolves mpaka kocha wakala wao ni Mendes

Swali lako halina maana.

Yaani umefungwa na timu ambayo haina hata haja ya kuchukua hilo kombe alilokutolea.

Piga mbuzi hao
Kwaiyo time nzima ya Wolves wana wakala mmoja tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom