Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,498
- 28,720
Hatushangai kupata ushindiMara nyingi tukicheza bahati imekuwa upande wetu lakini leo imegoma na kuhamia kwa Asernal..
Tumecheza vizuri tu lakini matokeo hayajatufever. Lukaku sijui anahitaji nafasi ngapi ili atumbukize kambani... hili nadhani hata yeye linamnyanyasa sana kuona ni kiasi gani anakosa nafasi za wazi na kuigharimu timu. Fred ameendelea kuimprove siku hadi siku... leo amecheza vizuri sana ile penalty ni tension tu ya mchezo hii ni baada ya kuona kazidiwa na jamaa anafunga hivihivi akatumia maujanja ya kumsukuma lac kwa bega bahati mbaya kwake refa alikuwa Karibu sana akilishuhudia tukio hilo umbali wa sentimita kadhaa... but kwa hakika amecheza vizuri sana, wakati ambao Matic alipwaya Fred alikuwapo kusaidia..
Sijui ni kwanini Ogs ameamua kumuanzisha Matic akimuacha Mctimaney ... binafsi nilidhani angeanza na Mctimney, Fred na Pereira kama kawaida halafu Dalot na Matic wasubiri kwanza... kwa wale waliokuwa wakilalamika ni kwanini Dalot kaanza badala ya Martial nadhani wamegundua ni kwanini.... kocha ndie anayekaa na wachezaji anajua yupi yuko fit na yupi asubiri..
So far... tumecheza poa sana, hata asernal wenyewe wanashangaa ni aje wamepata ushindi ktk mechi hii..!! Tunaendelea kusonga mbele tukirekebisha makosa ya hapa na pale kwa mchezo wa leo..
UNITED WE STAND
Sent using Jamii Forums mobile app
Mechi za kushinda zinaonekana
Leo ilikuwa afe kipa afe beki ,
Halafu pale ni emirates nina rekod nzuri mechi za home EPL ,
Ukija lazima ukubali mm ndio nitawale mchezo ,
Sent using Jamii Forums mobile app


