Fellaini alikuwa ni moja kati wachezaji wasiopendeka
Narudia pale pale, inawezekana ni psychological effect. Watu wengi wanamkumbuka Felli kwa kupiga vipepsi na kadhalika
Lakini wanasahau mara kadhaa alizoisaidia United, tena wakati mgumu
Unadhani kwanini kila National Team Felli anaitwa na hajaanza Martinez, tangu yule kocha aliyeondoka
Mimi ukiniambia nichague kati mbwembwe na magoli nitachagua magoli. After all mbwembwe tunazipata kwa wachezaji wengine, sio lazima namba 1 mpaka 11 wote wawe na mbwembwe uwanjani.
Hivi suala ni kufunga goli maeneo gani au suala ni kufunga goli? Na Lukaku hafungi nje ya 18 yard sio kwa sababu hawezi, ila ni kwa sababu ya hulka yake ya kutokuwa mchoyo mfano angeweza kujaribu kwenye mechi ya FA dhidi ya Arsenal lakini akampa pasi Sanchez (na tulimsifu), angeweza kujaribu shuti dhidi Liverpool lakini akamoa pasi Lingard.
Rashford ni mchoyo, Martial ni mchoyo na wote wamekuwa wakipata magoli nje ya 18, na wakati wanapiga mashuti wakidhani ni mshale kwamba mpira utapenya.
Umewahi kujiuliza ni mara ngapi huo uchoyo wa madogo umeinyima magoli United? Maana wamekosa mengi sana ukilinganisha na waliyopata.
Kuna magoli ya wazi hao madogo huwa wanakosa wakibaki na makipa. Au sababu ya kung'ang'ania mpira wanachelewesha move ya mpira na kutukosesha nafasi.
Harry Kane ni complete kiasi hicho? Is he that good in dribbling? Ukiondoa magoli yake ya penati pengine amezidiwa na Lukaku
Mwisho, CR7 is CR7. Messi is Messi. We can't have many Messi's or Ronaldo's in this world. Tungekuwa nao wengi, wasingekuwa special.
Sent using
Jamii Forums mobile app