Kiukweli hata yeye akijitathmini nahisi anapata msongo wa mawazo...ndo wachezaji wa Mou hao,akiona timu zingine zinamuulizia anakimbilia kununua...kuna wakati namuangalia anavyocheza naamini kuna wachezaji zaidi ya mia kwenye ndondo cup wanaocheza vizuri zaidi yake.
Sent using
Jamii Forums mobile app
hahahahahaaaaaaaa comment yako imenichekesha sana kuliko tukio la edo kurudi nyumbani bila ya mkia.
siamini ya kwamba klabu ilimnunua
fred kwa ajili ya kuwabania manchester city wasimsajili bali klabu ilishamuona
fred kama ni potential midfield ambaye atatusaidia kwenye harakati za kurudisha heshima iliopotea kwa takribani miaka 6 ila kwenye ishu ya dau ni kweli
shakhtar wametufanyia uhuni kiupande fulani.
wapo wachezaji wanaposajiliwa kwenye klabu mpya msimu wao wa kwanza wanarudisha fadhila za kusajiliwa kwao lakini wapo wengine wanastruggle sana na hii inatokana na changamoto za kimazingira na kimfumo, cha msingi ni kuendelea kuomba fred awepo kwenye hili kundi la pili kama ilivyokuwa kwa
victor lindeloff na si lile la tatu (flop player kama bebe).
nyakati fulani jose mourinho aliwahi kuulizwa na waandishi wa habari kwa sababu gani hampi nafasi fred?
jose akajibu ni sababu za kimfumo na alilezea ya kwamba klabu ina tatizo la kiulinzi ndio maana tunaruhusu kufungwa hivyo basi kwa style ya
fred uchezaji wake hauleti balance kwenye eneo la ulinzi, jose alikuwa anatuaminisha ya kwamba ili fred apate nafasi ya kucheza ni lazima defence ionyeshe mabadiliko.
Na hapo ndipo tatizo kuu la performance isioridhisha kwa
fred ndipo lilipoanzia kwa sababu jose hakutaka kumpa game mara kwa mara ili kuonyesha improvement ya kiuchezaji (match fitness).
Hata nyakati zile tulizoshuhudia vita ya maneno kati ya
jose mourinho dhidi ya
paul pogba tulishuhudia jose mourinho akiendeleza tabia ya kumweka nje
fred haliyakuwa kiucheza ndiye mchezaji pekee ndani ya timu yetu mwenye uwezo wa kuziba nafasi ya paul pogba kwa ufasaha zaidi, hatimaye jose mourinho alimuona
marouanne fellaini kama ni mtu sahihi kuziba nafasi ya
pogba pamoja na
mctominay.
ujio wa
solskjaer ametuletea falsafa ya 4-3-3 kwenye mechi zake takribani zote alizocheza, kwa hali ya timu yetu ilivyo hata kama mimi ndiye solskjaer basi ningeendelea kumbatiza kwa moto wa gesi
fred the red.
hivi ni kweli perreira na mc tominay ni wachezaji mahodari kuliko fred?
kwa mtazamo wangu si kweli, sababu kubwa inayopelekea wawili hao wapewe nafasi mbele ya
fred ni kwa sababu mpira baadhi ya nyakati hatuangalii chenga na rangi bali balance na impact inayoletwa na mchezaji akiwa uwanjani pindi unapokutana adui mwenye sifa kama za kwako.
ina maana sababu ile ile iliopelekea mourinho amweke nje fred ndiyo anayoendelea kuitumia ole gunnar solskjaer nyakati hizi nayo ni sababu ya balance kwa sababu bado defence yetu haijawa katika kiwango cha juu ukilinganisha na kuta za timu nyengine kama atletico madrid, liverpool. timu zote tunazozifahamu basi hazikosi wachezaji wenye mindset, form, uzoefu na uwezo wa kucontrol game na hapa ndipo anapozidiwa fred na vingo tulionao ndani ya klabu.
- kwa mujibu wa timu yetu anapoumia matic nafasi yake inapaswa izibwe na mctominay kwa sababu ni defensively solid player dhidi ya fred.
- anapoumia herrera nafasi yake inapaswa izibwe na perreira kwa sababu ndiye mwenye uwezo wa kuleta balance halafu pia ni rahisi kufanya naye mawasiliano kwa sababu anaweza kuzungumza lugha ya kiingereza.
- ina maana kwa mpira anaocheza fred eneo pekee ambalo ataufurahia mpira wake ni nafasi ya paul pogba, wakati huu tunaowania kuwepo top 4 je unaweza kumfanyia rotation pogba kwa ajili ya fred?
changamoto anazokutana nazo fred ni tofauti kabisa na changamoto alizokutana nazo victor lindeloff msimu uliopita na mwanzoni mwa msimu huu, wapinzani wa lindelof ambao ni smalling, bailly na jones wote kwa pamoja ni rahisi kupambana nao kwa sababu ya viwango vyao na hata takwimu zao za majeruhi.
lakini kwa
fred hali ni tofauti kwa sababu
matic, herrera na
pogba tayari wameshajijenga kama ni nguzo muhimu ndani ya timu yetu hivyo basi fred anahitajika kuutumia msimu ujao kwa kufanya bidii kubwa sana ili amuondoe mmoja wapo huku akiombea klabu ifanye usajili wa kumleta mlinzi hodari atakayemuwezesha kumpunguzia majukumu ya kulinda.
tumpe muda na nafasi ya kudhihirisha thamani yake, nataka niendelee kuamini ya kwamba fred hakuja uingereza kujifunza lugha ya malikia iliomchukua miaka mingi carlos tevez kuifahamu bali amekwenda uingereza kufanya kazi.