Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hongera yetu kwa ushindi wa jana na pole kwa mashabiki wa Chelsea wanaoishi humu ndani.... Binafsi jana nimetoa doubt zote juu ya Ole na ingekuwa kwa idhini yangu Ole angepewa mkataba wa Miaka 5 Leo kabla ya saa 4.......

Inashangaza timu ile ambayo watu humu walisema ifumuliwe tununue timu mpya, leo hii inaoerform kwa kiwango cha juu na morale kuwa ya juu sana..... Binafsi naipongeza timu nzima kuanzia benching la ufundi hadi subs ambazo hazikucheza maana umoja iliopo ndiyo chachu ya mafanikio...... Ander Herrera,, nashindwa nisemaje ila anastahili mkataba wa Miaka 5 uyu kijana kwa mchango wake katika club.....

Pia naona shida yetu bado ipo kwenye defence hasa centre na hata fullback maana Chelsea walitupa shida mno, pia kuliziba tatizo hili tunaweza sajili winger wa kulia mkali sana atakaezuia wapinzani kupanda sana upande wa kulia.....

Leo nimeahinda na scout wachezaji mbalimbalu kuwajua kiundani.... Centre half wakuja nadhani ni Kati ya skinnier au Koulibally....namba 7 nimemuangalia Federico Chiesa wa Fiorentina na Sancho nadhani Sancho mzuri kwani kiumri mdogo na speed inaruhusu....namba 2 tusisajili tungoje kina mensah na Alex tuanzebe warudi tuwapime nao......

Namba 6 msaidizi wa matic ni muhimu sana nmewaza tu endapo tungekuwa na Matic na Axel witsel ingekuwaje?..... Kulingana na takwimu nadhani tunahitaji midfielder Kati ya ndombele au Neves.... Namba 9 kutokana na kuanza kuchipukia kwa Greenwood pia Rashford kuonesha kiwango kizuri nadhani tumuache lukaku apambane nao hawa, kwani akija icardi atataka aingie kwenye timu moja kwa moja na hii itaniua confidence ya Rashford.......

But all in all hatupo mbali na ufalme kwa kikosi hiki ukiongeza Sancho, Skinnier o Koulibally na ukiongeza ndombele au Neves lazima tusumbue .....


Sijamsahau Joao Felix dogo wa Miaka 19 second striker na attacking Midfielder ya Benfica... Naona namba 10 tungeweza msajili aje awe mrithi wa Mata na baada ya kumfuatilia vzuri nahitimisha kama Jose ''the big talent is there he has a potential to be a great player" ananikumbusha kaka enzi anachipukia he is crinical.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ANDER HERRERA:"Tatizo la chelsea tulijua lipo katikati pale alipo Jorginho na kocha akaniruhusu kuwa ninafika hapo kila mara na tulifanikiwa".

Mourinho baada ya kutoa 2-2 na chelsea mwezi wa 11/2018
"kucheza na chelsea ya sasa ni rahisi mnoo kwan kazi yako kubwa nikuharibu mipango ya Jorginho basi"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ANDER HERRERA:"Tatizo la chelsea tulijua lipo katikati pale alipo Jorginho na kocha akaniruhusu kuwa ninafika hapo kila mara na tulifanikiwa".

Mourinho baada ya kutoa 2-2 na chelsea mwezi wa 11/2018
"kucheza na chelsea ya sasa ni rahisi mnoo kwan kazi yako kubwa nikuharibu mipango ya Jorginho basi"

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio inarudiwa ss3 hapa. Jana umeme ulizingua nikalala

Sent using Jamii Forums mobile app
 
OFFICIAL | Orlando City have announced the signing of former Manchester United winger Nani on a free transfer from Sporting
FB_IMG_1550595324751.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom