Mkuu kuna 2 style za defense:-
1. Defending by offense
2. Defending by defense
Mou anatumia hiyo ya 2, na amekuwa analazimisha strikers, midfielders kurudi nyuma kuzuia (unaikumbuka kazi ya kina Etoo Inter), na mfano mwaka jana kuna scenarios Lukaku anajifunga kwa sababu ya kuja huku kwenye back line.
Kwa mpira wa sasa ambao wings hazipigi cross, bali zinakufata imekuwa ni kazi sana kuwa na mafanikio kwenye eneo la defense kama unarudisha timu yote nyuma na watu wanakushambulia muda wote, back then ungekuta wings zinabanwa kwenye crosses, strikers wanapigwa pini maisha yanarahisika, toka 2010 Mou achukue UEFA, then Chelsea 2012 (almost kwa kutumia schemes za Mou) hii mbinu ya ukabaji si rafiki tena kwenye soccer.
Pep anatumia mbinu zote mbili, anakaa na mpira katikati na mbele, muda mwingi nyuma kuna relax (offensive way of defending), na ikitokea mpira ukaja nyuma anarudisha wachezaji wachache kuja kusaidia back line ili wakirecover mpira kunakuwa na watu wa kuupokea. Na ndiyo maana ni wao waliofungwa goli chache EPL na wamefunga goli nyingi. Mfumo wa Mou wa ukabaji haukupi nafasi ya kufunga goli nyingi.
Pep na Barca yake walijikita kwenye mbinu ya kwanza pekee, walikuwa hawajali sana kwenye beki isipokuwa ushambuliaji, ila hii Man City jamaa kasuka beki nzuri, anasumbua kote.
Pep ni bora vs Mou; unapopewa timu, una identify mahitaji, unapewa hela unanunua wachezaji wanaokupa matokeo kama haya wewe ni bora.
Akiwa Bayern hakuwa na mandate kama aliyonayo leo Man City, ile timu Legends ambao ni wazawa wanaangalia pale, wana sauti, na ni timu almost ya Taifa, uhuru wa kufanya utakavyo ni ngumu.
Mou kashapewa wachezaji wengi na anasema hawafit, wrong choice of resources ni almost misuse, huwezi kuwa unanunua 5, moja ndo inafanya vyema tukasema wewe ni bora.
Mimi kwangu Mou was best up to 2010.