Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Bro fella new look
IMG_20181114_150914.jpeg
 
Goals conceded in the Premier League by David De Gea per season

2016-17: 29 (35 games played)

2017-18: 28 (37 games played)

2018-19: 21 (12 games played)

If we speak, we are in big trouble...
😶😶😶
 
Mkuu jenga hoja kwanini Pep, mimi nimetoa sababu zangu
Samahan mkuu Kama approach Niliyotumia ni mbaya. Lakini mkuu pep ni kitu kingine kwangu mm. Na Pep angepata wachezaji walioachwa na kocha yyt Kati ya walioondoka OT-Old Trafford wangefanya wonders.

Nataka nikuonyeshe namna pep angemtumia de Maria, namna pep angemtumia kagawa, na wachezaji wengi wengi waliopitia utd. Naamini uhusiano mzur Kati ya manager na wachezaji ndio moyo wa ushindi.
 
Samahan mkuu Kama approach Niliyotumia ni mbaya. Lakini mkuu pep ni kitu kingine kwangu mm. Na Pep angepata wachezaji walioachwa na kocha yyt Kati ya walioondoka OT-Old Trafford wangefanya wonders.

Nataka nikuonyeshe namna pep angemtumia de Maria, namna pep angemtumia kagawa, na wachezaji wengi wengi waliopitia utd. Naamini uhusiano mzur Kati ya manager na wachezaji ndio moyo wa ushindi.
Mkuu usijali. Tujadili tu

Pep ni kweli ni miingoni kati ya makocha bora,lakini si bora kama tunavyataka kuaminishwa

Ukweli ni kwamba Pep hajawahi kujaribiwa uwezo wake akiwa na wachezaji wa kawaida ama waliochoka, mfano mzuri angalia wachezaji aliowakuta city, ukiondoa aguero , Silva na De Bruyne nani mwingine ambaye bado anayecheza pale chini ya Pep

Msimu wa kwanza wa Pep pale City ndio uliotupa picha kwamba Pep anaweza kushinda makombe akiwa na wachezaji wa kawaida ama la (Kumbuka pia wale wachezaji, akina Hart,Zabaleta, Kompany,Otamendi, Navas, Zeko n.k ndio walibeba kombe EPL mara kadhaa, hivyo hawakuwa wabovu kiivyo)

Kwahiyo mkuu Kagawa wa United ndio akina Navas wa City, pia Ihenacho wa City ndio Rashford wa United. De Maria wa United kwani kwa sasa anafanya nini kikubwa huko PSG? Lakini pia nakukumbusha hao wachezaji uliowataja wote waliondoka kabla ya Mourinho hajawa Mwalimu wa United
 
Man u ina wachezaji wazuri lakini Mou mfumo wake wa kukaba sana haufai kwa mchezaji kama rashford..
Mpira umebadilika zamani majukumu ya kukaba yalikuwa ni ya beki na kiungo mkabaji tu, lakini kwa sasa hata namba 9 anakaba (angalia mfano zinapotokea set pieces)

City wenyewe hadi akina aguero wanakaba, lakini wao wanakabia juu na sio kwenye nusu yao, angalia mfano aguero mechi ya juzi na united kama sikosei, alilambwa kadi ya njano sababu ya kukaba.

Kitu ninachoona ni kwamba, kwa sasa imekuwa ni rahisi sana kumlaumu Mou sababu matokeo hayaendi upande wake

Amin nakwambia, kwa mfumo huu huu wa sasa akipata matokeo mazuri utaona vigelegele na mapambio kutoka kila kona
 

Walikosea sana kumfukuza LVG,angepata hawa wachezaji tulionao leo,angefanya makubwa sana.

Nimesikia tetesi José hatopewa pesa za usajili January, ni bora wasimpe kabisa. Amenunua bailly anampiga bench tu huku akilalamikia CB. Leo bailly wanamtaka Spurs na Arsenal. Na akienda atakuwa bonge la beki.
 
Back
Top Bottom