Ni sawa unachokizungumza brother hao wote wapo Manchester united kwa muda mrefu ukilinganisha na wachezaji wengine waliopo lakini kwa viwango vyao wanavyovionyesha uwanjani kwa sasa umefika muda muafaka wa klabu kutafuta damu mpya zitakazorudisha heshima ya manchester united ambayo imeshapoteya kwa miaka 6 hii iliopita. Naomba uwe mkweli hivi kati ya hao wote watatu (smalling, young, valencia) ni yupi kati yao mwenye uwezo wa kucheza real madrid, barcelona, juventus,chelsea, manchester city na hata liverpool kwenye kikosi cha kwanza?
kwa kiasi kikubwa tabia hii ya kuwashikilia wachezaji ambao uwezo wao unaonekana dhahiri umepungua lakini klabu ikaendelea kuwapa mikataba mipya kwa hoja ya uzoefu walionao imechangia kwa kiasi kikubwa kutufikisha nyakati ngumu hizi na bahati mbaya ugonjwa huu ulikuwepo tokea nyakati za ferguson. Tukiangalia upande wa pili hivi kuna mchezaji anayeifahamu chelsea kuliko
john terry lakini mbona ilipofika muda klabu iliona ni bora iachane naye na watafute wachezaji wapya watakaoendeleza harakati za ushindani sasa kwa nini kwetu sisi inakuwa ni vigumu?
Unasema timu haijapata mbadala wa
ashley young ndio maana wanaendelea kumpa mkataba mpya, kwa ufahamu wangu mdogo kuna njia kuu mbili za kupata mbadala wa mchezaji unayetarajia kumuondoa nazo ni kutumia academy player kama walivyofanya liverpool walipoamua kumpa nafasi
alexander arnold awe mlinzi wao wa kulia au kufanya usajili wa mchezaji kutoka klabu nyengine kama wanavyofanya klabu nyengine, kwa mfano ukitaka kujua jinsi gani soka linabadilika wakati manchester united tunaendelea kuwapa mikataba mipya jamii ya wachezaji kama
valencia na
young upande wa pili majirani zetu wanamuondoa
alexander kolarov ambaye ana uwezo wa kucheza kwenye timu yetu na wanamsajili
kyle walker kwa 50 millioni pounds. kitendo cha
ashley young na
valencia kurudishwa eneo la ulinzi ni uthibitisho tosha wa kushuka kwa viwango vyao kwa sababu wote hao wamesajiliwa kama ni wachezaji wa mbele.
kuitwa kwa ashley young kwenye timu ya taifa hususani ya Uingereza haina maana yeyote kiupande wangu kwa sababu ukimuondoa
harry kane na
kyle walker hakuna muingereza yeyote mwenye uwezo wa kujumuishwa kwenye kikosi cha wachezaji 50 wa timu za taifa kama vile france, germany, brazil na hata spain hii ya kipumbavu inayothubutu kumweka benchi azpilliqueta mbele ya
nacho wa real madrid.
tulishafanya makosa na hatupaswi kuendelea kufanya tena makosa, ni kama masaa 24 yaliopita tulianza kushuhudia waarabu wa etihad wakimsajili robinho, santa cruz, phillips ndani ya klabu yao hatimaye mashabiki na viongozi wa manchester tukajiaminisha ya kwamba klabu haijengwi kwa nguvu ya fedha pekee na pia manchester city hawana uwezo wa kutawala jiji la manchester.
wakaleta wachezaji waliokuwa na uwezo wa kucheza kwenye kikosi chetu kama vile yaya toure, silva, dzeko, kolarov, zabaletta, aguero n.k na sisi tukaendeleza utamaduni wetu wa kuwapa nafasi wachezaji ambao walishaonyesha dalili ya kuwa wa kawaida kiviwango, kwa mfano fletcher, oshea, brown, smalling, jones, buttner na cha kushangaza zaidi tukakataa kulipa paundi milioni 33 kwa ajili ya usajili wa
sneijder na
luka modric na hatimaye tukamrudisha paul scholes kwa mwaka mmoja.
wakatupiga goli 6 uwanjani kwetu lakini bado tukaendelea kusinzia na kujifanya kama matokeo hayajatuharibia heshima yetu hatimaye leo hii manchester city wamekuwa ni bora mbele yetu.
Naamini kwa anayeangalia mpira kwa jicho la tatu basi atakuwa ameshaiona hali halisi ya timu yetu ilivyo kupitia mechi mbili zetu za juventus. Ed woodward anapaswa kuacha tabia za kifala na ujuaji mwingi kwenye kuiendesha klabu, tunahitaji damu mpya zaidi ya nne ili tuweze kupambana nao kibabe juventus na wababe wengine. Kwa muda mrefu nilishindwa kumuelewa mourinho nadhani umefika muda wa kumtafuta
bwana polepole wa thread hii ili niunge mkono juhudi za jose mourinho za kuirudisha manchester united kwenye soka la ushidani haijalishi kwa soka la Chato FC na dau langu ni konki konki konki zaidi ya mange.
jose mourinho hajawahi kuwa mnafiki kwenye maisha yake ya soka na hatokuwa mnafiki kwenye maisha yake yote ya soka ndio maana anatwambia live ya kwamba manchester united tuna wachezaji wa kawaida sana japokuwa inakuwa vigumu kumuelewa.
mkuu kuna jambo umesahau kwa bahati mbaya baada ya kuandika ya kwamba hatujawahi kufungwa mechi alizocheza ashley young kama mlinzi wa kulia msimu huu, na pia ashley young amefunga magoli 13 tu kwenye mechi 158 za manchester united, ina maana anazidiwa hata na sergio ramos wa real madrid.
View attachment 926756