Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kulikua na sababu gani zilizofanya fellain kuanza na pogba au mactomney au mata kukaa nje?,,,,pia zile mbinu alizotumia Leo kucheza unazani zilikua nzuri? ,

Huwezi kuwa unatafuta ushindi kwa kutegemea game plan ya mipira ya juu kwa timu ambayo inamiliki mpira kama sevilla

First eleven yake tu inaonesha aliingia kujihami na kutegemea long balls!mata ndo mchezaji pekee kwa sasa anayeiunganisha timu huko mbele,unamweka benchi unampanga fellaini alietoka injury mda sasa!

Kwa kweli mou akiendelea na hii timu aibu hazitatuisha leo wala kesho
 
1520979233662.png
 
Poleni sana Man U
Ndiyo soka,Seville sio team rahisi kama mlivyokuwa mnadhani!
Chukueni kutolewa huku kama ni changamoto ili mwakani muwe wazuri zaidi!
MAJOGOO yanaenda final KIEV kwa hili nina uhakika!
Poleni sana na ndiyo soka!
 
Kocha wenu anaamini Kujituma na Nguvu kazi ya mchezaji ndio kila kitu kwa mchezaji Anasahau kunakitu kinaitwa Uwezo sasa inamuadhibu
 
Kama uliona na kuchambua game ya Liverpool ungenusa hii ya leo!
Liverpool bao zote mbili KAJIFUNGA kwa makosa ambayo ni ya kipuuzi sana!
Hamna bao lolote la Rashford lililokuwa limetengenezwa
Ukikutana na beki kama Mercado na wenzake ambao makosa ni very rare huwezi shinda!
Man U ya sasa inategemea vitu viwili kushinda
(1)Uhodari wa kipa wake De Gea
(2)Team pinzani ifanye silly mistake(s)
Mnatakiwa sasa mbadirike,mcheze mpira!
 
Nafkiri kwa kumuanzisha Fellaini na kumuacha Mata na Pogba nje kunasema yoote kuhusu Mourinho
 
Wakuu najiunga na Mashabiki wa Man Utd ulimwenguni kote kuumia moyoni kutolewa mapema UCL na Seville..

Tunasubili World Cup tu hakuna kingne tena,,,
Tunashukuru ubutu wa Chelsea pengne story zingekua zingine..

Ila kuna wakati tunatakiwa tujue nini hasa shida ya Manchester Utd??
Falsafa ya Mwl?
Mbinu zake uwanjani??
Wachezaji wa kawaida??
Wachezaji hawapambani??

Utd ni team kubwa kama Jose kachemka/atachemka
Sijui nani anaweza kuokoa jahazi,, but any way tujiunge na wenzetu wa... Next Season...
 
Ninachoamini ni kwamba Mournho anatembelea kivuli chake cha zamani ila kiuwezo Wa kufundisha mpira hana jipya kilichobaki ni kubahatisha tu na jitihada za wachezaji. Ktk makocha wote wakubwa duniani Jose ndo anacheza mpira mbovu sana. Timu haina muunganiko Wa kueleweka kati ya kiungo cha kati na safu ya ushambuliaji,tunategemea zaidi mipira ya kupigwa na kipa ndo imfikie mshambuliaji.
 
Back
Top Bottom