Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu malengo nn km co ubingwa ? Unavyojihami kwenye game kubwa ukapata point 1 badala ya 3 wakat city unaikimbizananea anasaka 3 kokote kule unategemea nn ? Lbd km malengo ya bodi ni kuwa kwenye top 4 !!!
Unakumbuka Chelsea alichukua nayo ubingwa..?? Mbna ilikuwa inapaki bus hadi mechi ndogo? Mourinho ana hesabu zake kichwani
City kaanza vizur lakin mambo yanabadilika itafika kipind ataanza kupteza hizo tatu na yeye mkuu.....
 
Mie nafikiri lukaku yuko poa na ile ndio style yake sema unamuona kapwaya kidogo ni kwasababu feeders hazikuwepo nyuma yake.

Kwa tathmini yangu mikh ndio katokota sana leo na ndio alikua kete ya ushindi toka first half.
Kiujumla tuna tatizo kubwa sana kwenye namba 10 kwa sasa

Mikhi amedrop sana kiwango hivi karibuni nilitegemea kutokuwepo kwa Pogba/Fellaini yeye ndio inabidi aibebe timu lakini ameshindwa.Kama umegundua recently Mourinho ameanza kumchezesha Lingard kama namba 10 licha ya kuwa sio creative mid ukilinganisha na Mata/Mikhi .Kama Pereira angebaki msimu huu angecheza sana na huenda angejihakikishia namba
 
Mkuu jamaa anachosisitiza ni kwamba duniani Mou anajulikana kwa defensive game plan,ni kama ambavyo Pep anajulikana kwa attacking game plan.Sasa bodi ya UTD imempa mkataba Mou na inajua kwamba atakuwa anacheza hivyo ila ilimradi anafikia malengo ya club.
Pia mpira umebadilika duniani,labda hata SAF angebadilika kutokana na mazingira.Nadhani unaona kilichompata dinosour kwa kugoma kubadilika.
Dinosaur =Arsene Wenger
 
rekodi imeendelea aiseeee pochetino hajawahi mfunga mou akiwa uwanja wa nyumbani
 
Mzee baba ongeza mapicha picha....binaadamu wanafiki sana kuna kipindi RUTASHUBANYUMA alihamia katika uzi wa Likes humu watu wakaanza kusema mara uzi upo kimya nk..
Hayo mapicha picha ndiyo aina ya mchango wake kama wengine kazi yao kuqoute matusi tu nk
Yes aongeze kutupasha habari
 
Mie naona Mikh anajitahidi kwa nafasi yake ila anashuka sana na anashidwa kupanda kwa haraka,ila naamini viungo wetu wakirudi tutamuona Mikh akirudi kwenye ubora.
Najua Lukaku ni style anayocheza ila sasa hivi defense nyingi zimemjua kwamba hajui chenga na ukiwa unacheza na timu kubwa zinajua weakness yako inakuwa ngumu sana kufunga.Leo Mou alijua kwamba Eriksen ndio uti wa mgongo wa spurs na tulimficha kweli kufanya spurs wawatumie Winks na Aurier kufanya mashambulizi.
Lukaku inabidi kubadilika kama anataka kuongoza attack ya timu kama Utd,naomba tuangalie strikers wa elite teams in europe halafu tumsimamishe na Lukaku.
Mkuu hizo "elite teams in europe" ndiyo zipi??
 
Back
Top Bottom