Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hahahahaaaaaa.. Pyeeeeeeeee
66cb3db3e14e6d15299c42bb5f6812f8.jpg
"Hata sijaumia sana!"

Hahahaha
 
Hakuna kitu cha ajabu kilichotokea Leo.

Toka mechi ya Liver tatizo lilianza kuonekana,ikafuata mechi ya uefa na sasa Leo.

Timu ni wachezaji 11,lakini sio lazima wote wawe fiti 100% ndio upate matokeo, hapana.Kwenye timu yeyote kuna key players ambao hawa ndio hufikia mapengo madogo madogo ili kuleta matokeo.

Leo lawama kwa martial,mata...wiki iliyopita lawama kwa mick,mara Herrera...kesho tegemea lawama kwa mwingine tena.

Manchester imepoteza balance ya timu,timu imemuhelemea Matic,timu imemuheremea De gea na bado timu imemuheremea Lukaku.

Timu imewazidi hao wachezaji 3 kwa sababu key players hawapo.Mwanzoni walijitaidi kuziba mapengo lakini sasa wanachoka.

Pogba ni moja kati ya balance kubwa sana kwenye kikosi japo unaweza sema haumuelewi anacheza nini.Plan B huwa ni Fellain ambaye anajua kubadili mchezo wote kwa ujumla.Bila kumsahau Bailly huwa anafanya viungo wa ukabaji wasiwe na majukumu makubwa sana na kurahisisha mashambulizi.

Timu ni chemistry, kwaiyo zikipotea baadhi ya particles lazima timu nzima itafeli.Na kwa mwendo huu tutamchukia kila mchezaji pale kwa kuhisi atimizi wajibu wake kikamilifu.

All in all,big up mourinho....Bado timu unayo na uwezo unao.
 
Back
Top Bottom