Baada ya msimu uliopita hata Man United walianza vizuri sana kwenye game 10 za mwanzo kabla ya kufungwa na Arsenal 3-0 hata mi nilikuwa na matumaini ya ubingwa,sababu ziko nyingi
1.Majeruhi-hii ni sababu kubwa iliyosababisha haya ,tulivyoanza ligi Shaw alikuwa anacheza vizuri na walikuwa wanaelewana sana na Depay tangu alivyoumia Depay nae akapotea.Shaw,Darmian,Rojo,Smalling,Jones,Carick,Martial,Rooney,Fellaini,Young,Valencia wote wanapokezana majeruhi
2.Kutosajili striker,msimu huu tatizo kubwa la timu ni kutotengeneza nafasi na kufunga magoli,LVG alipaswa kusajili striker.Martial anacheza vizuri winga ni mzigo mkubwa kumuachia Rooney kufunga while umri ushamtupa
3.Mfumo wa kocha na substution zake, tatizo la makocha wageni na EPL ni kushindwa kuwa na mifumo ya kubalance kushambulia na ku-defence(Pelegrini,LVG,Klopp).Moja ya weakness kubwa ya LVG ni kufanya sub huwa anachemka sana
4.Wachezaji pia wamekuwa wakicheza chini ya kiwango Rooney,Mata,Fellaini,Herrera,Depay,Lingard ,Scheiderlin wamekuwa wanacheza chini ya kiwango muda mrefu.De Gea,Smalling,Blind ndio wachezaji waliokuwa na consistency msimu huu