Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,865
- 12,297
Habari zenu wana JF wenzangu
Bila kupoteza muda ndugu zangu inajulikana wazi kuwa kila binadamu yupo hapa duniani kwa siku zake maalum za kuishi, na baada ya siku hizo kuisha atakufa na kurudi kule alipotokea.
Sasa basi.. ingawa kifo kipo lakini hakuna anaependa kufa au kufiwa. Hii ni kwa sababu kwanza ukishakufa haurudi kuwa hai, pili hakuna anaejua kwa macho yake mwenyewe kwamba baada ya kufa anakwenda wapi, tatu dini zimekuwa zikitueleza kuhusu adhabu iliyopo mbele yetu baada ya vifo vyetu kutokana na matendo yetu.
Kwa vile hakuna binadamu aliekamilika, kwahiyo kila mmoja wetu anajiona ana makosa mbele ya Mungu, hivyo kuogopa kufa mapema na kwenda kukutana na adhabu zake.
Halikadhalika pia hakuna anaependa kufiwa. Hii ni kwa sababu mfiwa anajua kwamba huyo baba yake, mama yake, mtoto wake au ndugu yake aliefariki hatopata tena chance ya kuonana nae katika maisha ya duniani. Yani ndio unakuwa mwisho wao kuongea pamoja, kucheka pamoja, kuishi pamoja, kusaidiana, kupendana, kuonana nk.
Hivyo basi mfiwa huumia kwa namna ambavyo alimpenda au kuwa na ukaribu na marehemu.
Maumivu ya kufiwa, au kufa kwa yule anaekiona kifo chake huwa ni makubwa sana. Mfano mama anapoona kwamba ugonjwa alionao hauwezi kupona, na pengine anakaribia kufa huku akiwaacha watoto wake wakiwa bado wadogo mno wenye kumuhitaji na kuhitaji malezi yake, ni lazima ataumia sana tena sana ila hatokuwa na la kufanya zaidi ya kuomba dua Mungu amsaidie kumlelea watoto wake kupitia mtu fulani, (labda bibi, mamdogo, shangazi nk) pindi tu atapochukua roho yake.
Mimi nimesha experience kufiwa na mzazi ambae tulimpenda sana, na yeye alitupenda mno watoto wake. So i know how it feel kuondokewa ghafla au hata kwa maradhi na mzazi au ndugu, lakini kuna njia ambayo ukiitumia kipindi cha msiba huo mzito itakusaidia kwa kiwango fulani kupunguza maumivu utayopata wewe mfiwa.
Je unatakiwa ufanyaje baada ya kushuhudia kwa macho yako kifo cha baba yako, mama yako, au ndugu yako, au pengine kuletewa habari za kifo chake.
1) Jambo la kwanza kama ni Mkristo unatakiwa hapo hapo useme ama kwa hakika bwana wewe ndio ametoa na wewe ndio umetwaa, jina lako lenye nguvu kuliko majina yote lihimidiwe daima milele AMEN
Kama ni Muislamu unatakiwa kusema Inna lillah Wainna Illayhi rajiun (Hakika sisi wote ni wa kwako Mola wetu mtukufu, na kwako wewe Mola wetu mtukufu sisi sote tutarejea)
Kwa wale wasiofatilia kauli hizi za dini unaweza kusema sisi tulimpenda, lakini wewe Mungu ndio umempenda zaidi.
Hii itakupa faraja kubwa mfiwa kwani itambidi ukubaliane na ukweli kwamba Mungu mwenyewe ameamua kuchukua kilicho chake, kwahiyo huna budi kukubaliana na hali hiyo hata kama hukutarajia au kupendezewa nacho.
2) Jambo la pili unatakiwa umuombe Mungu kwa imani yako akuongoze katika kipindi hiki kigumu kwako, lakini pia akupe subira na ustahamilifu, na pia kukuepusha na kufuru. Hii ni kwa sababu kuna baadhi ya watu wakifiwa na watu wao wa karibu huluzi fasta control na kupelekea wengine kukufuru Mungu kwamba "kwanini umemchukua mama yangu tu na sio mama wa kina Nusrat, Jessica, Abdallah, John nk" sijui "nimekukosea nini Mungu hadi kunipa msiba huu mzito ambao unajua kabisa siwezi kuubeba", "Eeh Mungu wangu kwanini umemchukua mwanangu mkubwa ambae ndio alikuwa tegemeo langu, je maisha yangu yatakuaje baada ya kumchukua mwanangu huyu mwenye msaada mkubwa kwangu nk. Yani inafika kipindi mtu anasahau kwamba kila kiumbe hapa duniani ni cha Mungu, kwahiyo hakuna mwenye uwezo au ruhusa ya kumzuia kukichukua, iwe leo, kesho au siku yoyote aitakayo yeye muumbaji.
Kumbuka Mungu huwa hakosei na wala haonei. Kila analofanya limekamilika tangu enzi na enzi.
3) Jambo la tatu ni kumuomba Mungu akupe muongozo wa maisha yako mapya ambayo utaishi bila kuwa karibu na yule alieondoka.
4) Jambo la nne tumia muda mwingi kumuombea marehemu ili apate makazi mema au Mungu aipokee roho yake na kuiweka katika roho za walio wema.
Kifupi ya kwangu ni hayo tu, ila kama kuna mungine anayo ya zaidi ya haya basi ruhusa kuyaorodhesha hapo chini kwenye comments.
Hii ni kwa wale tunaoamini uwepo wa Mungu, bila kujali dini ya mtu. Ila wasioamini uwepo wa Mungu naomba wasome tu lakini wasiandike chochote kuharibu uzi huu.
Karibuni ndugu zangu.
Bila kupoteza muda ndugu zangu inajulikana wazi kuwa kila binadamu yupo hapa duniani kwa siku zake maalum za kuishi, na baada ya siku hizo kuisha atakufa na kurudi kule alipotokea.
Sasa basi.. ingawa kifo kipo lakini hakuna anaependa kufa au kufiwa. Hii ni kwa sababu kwanza ukishakufa haurudi kuwa hai, pili hakuna anaejua kwa macho yake mwenyewe kwamba baada ya kufa anakwenda wapi, tatu dini zimekuwa zikitueleza kuhusu adhabu iliyopo mbele yetu baada ya vifo vyetu kutokana na matendo yetu.
Kwa vile hakuna binadamu aliekamilika, kwahiyo kila mmoja wetu anajiona ana makosa mbele ya Mungu, hivyo kuogopa kufa mapema na kwenda kukutana na adhabu zake.
Halikadhalika pia hakuna anaependa kufiwa. Hii ni kwa sababu mfiwa anajua kwamba huyo baba yake, mama yake, mtoto wake au ndugu yake aliefariki hatopata tena chance ya kuonana nae katika maisha ya duniani. Yani ndio unakuwa mwisho wao kuongea pamoja, kucheka pamoja, kuishi pamoja, kusaidiana, kupendana, kuonana nk.
Hivyo basi mfiwa huumia kwa namna ambavyo alimpenda au kuwa na ukaribu na marehemu.
Maumivu ya kufiwa, au kufa kwa yule anaekiona kifo chake huwa ni makubwa sana. Mfano mama anapoona kwamba ugonjwa alionao hauwezi kupona, na pengine anakaribia kufa huku akiwaacha watoto wake wakiwa bado wadogo mno wenye kumuhitaji na kuhitaji malezi yake, ni lazima ataumia sana tena sana ila hatokuwa na la kufanya zaidi ya kuomba dua Mungu amsaidie kumlelea watoto wake kupitia mtu fulani, (labda bibi, mamdogo, shangazi nk) pindi tu atapochukua roho yake.
Mimi nimesha experience kufiwa na mzazi ambae tulimpenda sana, na yeye alitupenda mno watoto wake. So i know how it feel kuondokewa ghafla au hata kwa maradhi na mzazi au ndugu, lakini kuna njia ambayo ukiitumia kipindi cha msiba huo mzito itakusaidia kwa kiwango fulani kupunguza maumivu utayopata wewe mfiwa.
Je unatakiwa ufanyaje baada ya kushuhudia kwa macho yako kifo cha baba yako, mama yako, au ndugu yako, au pengine kuletewa habari za kifo chake.
1) Jambo la kwanza kama ni Mkristo unatakiwa hapo hapo useme ama kwa hakika bwana wewe ndio ametoa na wewe ndio umetwaa, jina lako lenye nguvu kuliko majina yote lihimidiwe daima milele AMEN
Kama ni Muislamu unatakiwa kusema Inna lillah Wainna Illayhi rajiun (Hakika sisi wote ni wa kwako Mola wetu mtukufu, na kwako wewe Mola wetu mtukufu sisi sote tutarejea)
Kwa wale wasiofatilia kauli hizi za dini unaweza kusema sisi tulimpenda, lakini wewe Mungu ndio umempenda zaidi.
Hii itakupa faraja kubwa mfiwa kwani itambidi ukubaliane na ukweli kwamba Mungu mwenyewe ameamua kuchukua kilicho chake, kwahiyo huna budi kukubaliana na hali hiyo hata kama hukutarajia au kupendezewa nacho.
2) Jambo la pili unatakiwa umuombe Mungu kwa imani yako akuongoze katika kipindi hiki kigumu kwako, lakini pia akupe subira na ustahamilifu, na pia kukuepusha na kufuru. Hii ni kwa sababu kuna baadhi ya watu wakifiwa na watu wao wa karibu huluzi fasta control na kupelekea wengine kukufuru Mungu kwamba "kwanini umemchukua mama yangu tu na sio mama wa kina Nusrat, Jessica, Abdallah, John nk" sijui "nimekukosea nini Mungu hadi kunipa msiba huu mzito ambao unajua kabisa siwezi kuubeba", "Eeh Mungu wangu kwanini umemchukua mwanangu mkubwa ambae ndio alikuwa tegemeo langu, je maisha yangu yatakuaje baada ya kumchukua mwanangu huyu mwenye msaada mkubwa kwangu nk. Yani inafika kipindi mtu anasahau kwamba kila kiumbe hapa duniani ni cha Mungu, kwahiyo hakuna mwenye uwezo au ruhusa ya kumzuia kukichukua, iwe leo, kesho au siku yoyote aitakayo yeye muumbaji.
Kumbuka Mungu huwa hakosei na wala haonei. Kila analofanya limekamilika tangu enzi na enzi.
3) Jambo la tatu ni kumuomba Mungu akupe muongozo wa maisha yako mapya ambayo utaishi bila kuwa karibu na yule alieondoka.
4) Jambo la nne tumia muda mwingi kumuombea marehemu ili apate makazi mema au Mungu aipokee roho yake na kuiweka katika roho za walio wema.
Kifupi ya kwangu ni hayo tu, ila kama kuna mungine anayo ya zaidi ya haya basi ruhusa kuyaorodhesha hapo chini kwenye comments.
Hii ni kwa wale tunaoamini uwepo wa Mungu, bila kujali dini ya mtu. Ila wasioamini uwepo wa Mungu naomba wasome tu lakini wasiandike chochote kuharibu uzi huu.
Karibuni ndugu zangu.