Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Umeona eee watu wamechangia sana kwenye thread ya Kongamano la CDM Udom jamaa hata hakuona umhimu wa kuchangia wakati ni kongamano la viongozi wake wakuu sasa hili la ukatibu wa CCM ndio kaona lina muhimu zaidi.
Nimeona eee zitto kaaaazi kumuamini anawezana na jk tu
 
Kinana kawa deputy Tz bara, Nape kapelekwa itikadi na Zakhia Meghji kaenda fedha wakati Rehema Nchimbi akienda Organisation

Huwezi kumtenganisha Kinana na RA, Kinana ndiye manager wa campaign za CCM tokea 1995, amekuwa ni archtecture mzuri sana wa kufanikisha uchotaji wa public resources kwa kigezo cha kupeleka kwenye Campaign. JK katika hili amekwaruza tu gamba, na kwa nyoka ukimkwaruza gamba basi umemfupishia maisha yake ni lazima atakufa tu kwani molting haiwezi kufanyika tena katika maisha yake na akifanya gamba halitoki, anakufa nalo.

Sehemu ambayo naweza toa credit kidogo ni kwa Nape. Haitoshi CCM kufanya mabadiliko ya uongozi, ingetakiwa wabadili na Jina kabisa kutoka CCM ili wananchi wasilikumbuke dude linaloitwa CCM, Sasa hivi kuvaa kijani mtanii unaokana mwizi wa mali ya umma. Mukama sina historia yake kwa undaji japo alipokuwa Jiji wakati wa Keenja alikuwa na mawazo positive sana kuhusu usafi wa jiji. Kingine CCM waache propaganda za kitoto sasa, wa-focus kwenye ku-invest kwa wananchi, ikifikia 2015 90% ya vijana wakiwa na ajira nzuri kabisa basi hawana haja hata ya kuiba pesa za umma kwa ajili kampeni au kuandaa mbinu za chakachua bali ni kusubiri kuchaguliwa tu. Anything short of that will not work.
 
Too late we have new katibu mkuu already W.Mkama your story is old
 
Mukama katulia sana alikuwa utendaji wake si wa kubwabwaja ni msomi anapenda kujibu hoja alikuwa JIJI THEN katibu mkuu afya then katibu mkuu maji mpaka akastaafu.akateuliwa na rais kuwa mkurugenzi wa bodi habari.na amehusika sana kutunga ilani ya ccm 2010-2015 hivyo watu wenye bongo zao wanarudi chamani pia ni mtu wa system.
Hakuna kitu hapa, Mukama fisadi tu kama wengine. Alifipokuwa Jiji alifisadi sana. akumbuke alivyofanya wakati wa kununua magari ya zima moto ya jiji.
 
Most probably is not big news to you because you have no idea how this CCM NEC have costed our nations. The instability of our economy and you so called TRA, PTA etc. are caused by corrupt CCM NEC. And you know why? they hid in there in order to take advantage of the system and play their malicious games.

Sasa hizi cosmetic changes unafikiri zitasaidia vipi kuondoa msururu wa meli zilizojazana kule Oyster bay beach?

CC kubadilishwa kutasaidia vipi kuondoa longo longo la TRA na unfair taxation ?

CCM kuchagua mwenyekiti mpaya kutasaidia vipi wanafunzi kupata madawati kwa wanfunzi?

kila mwaka these lot wanafanya cosmetic changes zao na hakuna kinachobadilika zaidi ya headlines to make us look stupid

In short wanasiasa wana tucost and these guys kupeana kula wont change a thing trust me
 
Nina bahati ya kumfahamu Mukama binafsi wakati wakiwa Mkuregenzi wa jiji. Ni mtu mzuri sana na tena ana akili sana, ila linapokuja swala la kutafuta pesa kwa njia yoyote hata ya kifisadi, ndugu huyu huwa habaki nyuma hata siku moja. Inawezekana kwa vile ni mtu mwenye akili sana akatambua kuwa vita dhidi ya ufisadi ndiyo iliyomueweka pale, na hivyo akashidana na vishawishi vya ufisadi. Vinginevyo inawezekana CCM imeondoa a Rock na kuweka a Hard Place.
Mkuu Kichuguu umenena. hapo kwenye red umemaliza. Ndivyo ninavyomfahamu Mukama ni fisadi tu.
 
Mkuu invisible,

Naomba niwafahamishe wakuu hapa kuwa hizi habari japo watu wanaweza kutoziamini lakini ndo kinachoendelea hapa, Wilson Mukama hayupo Dodoma, yupo Kibaha kwa dharura maalum.

Nirejee kuhusiana na Meghji
 
Nothing, kitakachosaidia ni kuwa hawajafamiana. wakifamiana watakuwa mafisadi zaidi
 
Naona niwakosoe baadhi yenu, jamaa anaitwa MUKAMA na sio MKAMA. Shomile kutoka kagera lazima kuwe na MU yani OMUKAMA wange. Na watu kutoka mara ni MKAMA. Naomba msichanganye hayo majina mawili tofauti.
 
Mukama katulia sana alikuwa utendaji wake si wa kubwabwaja ni msomi anapenda kujibu hoja alikuwa JIJI THEN katibu mkuu afya then katibu mkuu maji mpaka akastaafu.akateuliwa na rais kuwa mkurugenzi wa bodi habari.na amehusika sana kutunga ilani ya ccm 2010-2015 hivyo watu wenye bongo zao wanarudi chamani pia ni mtu wa system.
Alifanya kazi chini ya huyo muheshimiwa kwenye picha(kulia).Hawakukosea waliposema simba mwenda kimya(pole) ndio mla nyama.


GO9G5073.JPG
 
Kuchaguliwa kwa Nape liwe Fundisho kwa vijana wenzake wanaotumiwa na mafisadi kama yule msomari. Simamia ukweli na ukweli utakuponya. Wao walibenk kwa LA. kiko wapi. Nape alijitahidi kujiepusha na mafisadi mwisho wa siku analia kivulini. Vijana wadogo kama msomari kuanza kuwa groomed kuwa mafisadi inasikitisha. Anyway for the sake of our country hii timu mpya iangamize mafisadi wote vijana na wazee! I am for change regardless inaletwa na Chadema au CCM. Hatuhitaji tu sura mpya ila tunataka mtusafishie hii nchi jamani.
nape anafadhiliwa na mengi au huoni kwamba mengi naye ni fisadi? katika vijana ni vita kati ya lowassa na mengi.
 
, ikifikia 2015 90% ya vijana wakiwa na ajira nzuri kabisa basi hawana haja hata ya kuiba pesa za umma kwa ajili kampeni au kuandaa mbinu za chakachua bali ni kusubiri kuchaguliwa tu. Anything short of that will not work.

Mambo haya yanawezekana kwa ilani ya CDM, huo uchumi wa kuajili vijana wote hao unapatikana wapi wakati vijana wapo bize kuandamana. Hizi namba zinakwenda na majukumu, unless wananchi wanaacha kulalamika na kufanya kazi uchumi huu hauwezi kuletwa kama mana. unawezekana tu kwa documents itakayotumika miezi miwili then kuwekwa library kama ile ya cement 5000/- ilivyofanywa.
 
Meghji ndiye kammaliza kabisa RA.

Katika CC Meghji alisema:

"Jamani, katika watu hatari RA ni mmojawapo na ndiye anayetumaliza. Yeye ndiye Kagoda, alikuja akafanya usanii wakati nikiwa waziri. Alichota hela nyingi na nikashtuka tukaita wakaguzi"

RA wakati Meghji anaongea alionekana kumnyooshea kidole.

Meghji aliendelea kuongeza "Alikuwa rafiki yangu na wa chama kabla sijajua ubaya wake. Nilipoteuliwa ubunge ndipo nikagundua ubaya wake zaidi kwani akitumia magazeti yake alihakikisha ananichafua. RA ni mtu hatari kwa chama na asipochukuliwa hatua sasa na si kesho basi tutaelekea papaya sana"
 
makala za wazushi wa mengi wanatunga habari kwenye vyumba vyao
 
..Kinana ni mtu wa karibu sana na Edward Lowassa.

..haya mabadiliko ni kama yamefanywa na Lowassa kwa kutumia remote control.

People leave the guy alone, nxt mtasema sasa yeye ndio anaharibu ndoa zenu.
Pure speculation
 
Je, mabadiliko haya ndani ya CCM yataleta ahueni yoyote katika maisha ya Watanzania walio wengi na pia kuleta maendeleo ambayo nchi yetu inastahili kuwa nayo? Je, mabadiliko haya yatamaliza ufisadi uliokithiri ndani ya Chama Cha Mafisadi/Majambazi na Serikalini? Kwa maoni yangu jibu ni HAPANA. Hivyo bado tuna safari ndefu sana ya kuikomboa nchi yetu toka mikononi mwa mafisadi.
 
Msomali Kinana ndani, wasomali watazidi kuingia kwa siri nchini, na genge la mafia wa kisomali walioko TZ wataongezeka


Acha ubaguzi wewe, huyo unayemuita msomali anaweza kuwa mzalendo kuliko hata RA na Chenge wako
 
JK alidakia na kusema "Hata mimi napata taarifa sehemu mbalimbali kuwa ufisadi ndilo donda la CCM na unaichafua, na kibaya tupo nao humumumu ndani.

Msekwa aliongezea "Sisi tumezunguka nchi nzima na ile kamati yetu ya Mzee Mwinyi, wananchi wamechoka na ufisadi na wanatuambia mafisadi tuko nao ndani ya chama tunawalinda"
 
Back
Top Bottom