Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Zakhia Megji Ni mkwe wa Kilaza Wetu, Sio Mchapa kazi labda huo uchapakazi kazi alikuwa anamfanyia Mzee Ruksa akilala

Duduwasha huyu ni mtu mzima, japokuwa sio mzazi wetu ni mzazi wa wenzetu, Haya maneno mengine tunayotoa ni vizuri tukawa na uhakika nayo.
 
WanaJF,
Ni kweli hali ya watanzania ni mbaya sana kwa sababu ya ugumu wa maisha. Tunaamini hali hiyo imesababishwa na uongozi mbovu wa Serikali ya CCM ambayo kwa miaka zaidi ya mitano dereva wake mkuu ni Jakaya Mrisho Kikwete.

Kwa muda mrefu sasa tumemlaumu JK kwa kushindwa kuchukua maamuzi magumu ili kuinusuru nchi.

Lakini kwa alichofanya juzi Dodoma ndani ya chama chake, anastahili PONGEZI.

Kama mwanadamu yoyote ni vigumu kumtosa rafiki yako wa karibu kwa sababu yoyote ile. Kama mwanadamu amewatetea maswahiba wake wa karibu kwa sababu anazojua yeye. Lakini juzi tumeona amechukua uamuzi wa kuwatosa maswahiba wake wa karibu RA, EL, Yusufu M, na washirika wa siku nyingi akina mzee wa vijisenti n.k., ili kuinusuru chama chake, bila shaka kwa lengo la kuinusuru nchi yetu kwa ujumla.

Hatuna hakika kama malengo yake yatatimia kuleta matumaini kwa watanzania tuliokata tamaa. Hatuna hakika kama hao waliochukua nafasi za uongozi ndani ya chama chake watakuwa msaada kwake na kwa chama chake. Hatuna hakika kama ana dhamira njema ya kuleta matumaini. Hatuna hakika na mengi kwa sasa..... lakini amefanya ujasiri mkubwa kuwatosa maswahiba wake.

Ni vema tukalaumu pa kuhitaji lawama, na kusifu au kupongeza japo kidogo panapohitaji kufanya hivyo. Kinyume chake tutakuwa wanafiki tukilalama tu.

Hatusemi amemaliza kazi, ndiyo anatakiwa kuanza.... bado anakazi kubwa... bado kama dreva wa chama chake ana nafasi ya kuponya walau baadhi ya majeraha ya watanzania bila kusahau hali ya Arusha... ili ufanyike uchaguzi wa meya kihalali na mengine mengi. Kama ana dhamira njema ya kufanya hivyo anaweza kufanya ndani ya muda mfupi.

Ni maoni yangu tu wanaJF
 
Pongezi kwa samaki kuparua samaki wenzake?
Ni nini gamba kutoa magamba mengine?

Me nakumbuka magamba magumu ndo hutoa malaini,JK ndio gamba lenyewe hafai kupongezwa kwa lolote
 
Hata kama wengejiuzulu wote isingekuwa suluhisho la haraka kwa hali iliyopo. Kwa alichofanya kama ni kwa dhamira njema hata ugamba wake utapungua. Swali bado linabaki kwetu sote ikiwa hao waliwekwa kwenye nafasi hizo watafaa kuleta mabadiliko.
 
Kila jambo ina pa kuanzia. Asingekuwa na kigugumizi cha kusafisha chama chake muda mrefu hali isingefika ilipofikia. Hata hivyo walau amefika mahali akafunga macho kwa uamuzi aliofanya anastahili kupongezwa japo kidogo kwa hili.
 
jamani kabla hujamuhukumu mwenzako jiangalie na wewe. ungekuwa ktk nafasi ya jk ungefanya kama unavyosema yy afanye. au tunabaki kujua kuangalia mapungufu ya wenzetu tu? kiukweli ktk hili jk amejitahidi japo bado ana deni kubwa kwa watanzania. tunachotaka hawa watu si tu waondoshwe ktk kamati kuu au kujiuzulu tunachotaka dola ifanye kazi yake ipasavyo na kuwafikisha mahakamani na kuiachia mahakama kazi yake iwahukumu kwa mujibu wa sheria.
 
WanaJF,
Ni kweli hali ya watanzania ni mbaya sana kwa sababu ya ugumu wa maisha. Tunaamini hali hiyo imesababishwa na uongozi mbovu wa Serikali ya CCM ambayo kwa miaka zaidi ya mitano dereva wake mkuu ni Jakaya Mrisho Kikwete.

Kwa muda mrefu sasa tumemlaumu JK kwa kushindwa kuchukua maamuzi magumu ili kuinusuru nchi.

Lakini kwa alichofanya juzi Dodoma ndani ya chama chake, anastahili PONGEZI.

Kama mwanadamu yoyote ni vigumu kumtosa rafiki yako wa karibu kwa sababu yoyote ile. Kama mwanadamu amewatetea maswahiba wake wa karibu kwa sababu anazojua yeye. Lakini juzi tumeona amechukua uamuzi wa kuwatosa maswahiba wake wa karibu RA, EL, Yusufu M, na washirika wa siku nyingi akina mzee wa vijisenti n.k., ili kuinusuru chama chake, bila shaka kwa lengo la kuinusuru nchi yetu kwa ujumla.

Hatuna hakika kama malengo yake yatatimia kuleta matumaini kwa watanzania tuliokata tamaa. Hatuna hakika kama hao waliochukua nafasi za uongozi ndani ya chama chake watakuwa msaada kwake na kwa chama chake. Hatuna hakika kama ana dhamira njema ya kuleta matumaini. Hatuna hakika na mengi kwa sasa..... lakini amefanya ujasiri mkubwa kuwatosa maswahiba wake.

Ni vema tukalaumu pa kuhitaji lawama, na kusifu au kupongeza japo kidogo panapohitaji kufanya hivyo. Kinyume chake tutakuwa wanafiki tukilalama tu.

Hatusemi amemaliza kazi, ndiyo anatakiwa kuanza.... bado anakazi kubwa... bado kama dreva wa chama chake ana nafasi ya kuponya walau baadhi ya majeraha ya watanzania bila kusahau hali ya Arusha... ili ufanyike uchaguzi wa meya kihalali na mengine mengi. Kama ana dhamira njema ya kufanya hivyo anaweza kufanya ndani ya muda mfupi.

Ni maoni yangu tu wanaJF

Ccm sio Tanzania. Anahurumia chama si waTanzania🙂
 
Pongezi kwa samaki kuparua samaki wenzake?
Ni nini gamba kutoa magamba mengine?

Me nakumbuka magamba magumu ndo hutoa malaini,JK ndio gamba lenyewe hafai kupongezwa kwa lolote

Kumpongeza kwa hili ni kukosa busara.
 
Wakuu, mtanisamehe sana sikuwahi kufuatilia mada hii toka mwanzo.. Nina maswali machache nataka kuuliza..
Kwanza, Kabla ya kamati hii, kamati iliyokuwepo mwanzo ilikuwa na majina yapi ktk nafasi za wajumbe wa NEC wa kuteuliwa tofauti na hii ktk nafasi zao..

Kwa mfano mtu anaweza nambia list nzima na kina nani wamekuwa replaced na nani toka list hii - Wajumbe wapya wa NEC wa kuteuliwa na Mwenyekiti ni Nchimbi, Januari Makamba, Anna Abdallah, Ali Juma Shamhuna, Peter Kisumo, Wilson Mukama na Lameck Mwigulu.

Katibu Mkuu mpya wa CCM atakuwa ni Wilson Mukama, Naibu wake atakuwa ni John Chiligati, Fedha atakuwa ni Mwigulu, Nape atakuwa Uenezi, Mambo ya nje ni Januari Makamba.

Hussein Mwinyi, Mbarawa, Omar Yusuf, Seif Khatib, Samia, Maua Daftari, Meghji, Kinana, Lukuvi na Mwenyekiti wa Kagera wa CCM (Mama Buhie), Kigoda, Wassira na Pindi Chana - CC...
 
Back
Top Bottom