Katiba ya Chama cha Mapinduzi inasema wazi kuwa majukumu ya kuleta nidhamu yako kwa Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC)katika ngazi mbalimbali za uongozi kitaifa. Katiba hiyo inasema hivi (Ibara ya 107 inayoshughulikia na Kazi za Halmashauri Kuu ya Taifa):
Kwa hiyo kwa vifungu hivyo viwili tu tunaweza kuona kuwa NEC inaweza kufanya mambo mbalimbali ikiwemo "kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake uifanywa na NEC".
Ibara ya 109 inaweka mojawapo ya mjukumu ya Kamati Kuu ya Taifa ni:
Halafu inabidi tuangalie kuwa Sekretariati ya CCM wajumbe wake wote wanaingia kutoka na nyadhifa zao. Hii ina maana hakuna ambaye anaingia kwa kuteuliwa na Mwenyekiti. Mwenyekiti wa CCM Taifa hana madaraka ya kumuondoa au kumsimamisha kiongozi yeyote wa CCM. Hata kama Mwenyekiti huyo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hii ina maana gani?
Ina maana ya kwamba lolote lililofanyika Dodoma litakuwa ni tendo la Kamati Kuu au Halmashauri Kuu ya Taifa. Tukumbuke kuwa Mwenyekiti ana kura ya turufu pale tu endapo kura za wajumbe zinalingana katika vikao visivyo husiana na vya uchaguzi - kwani huko ana kura moja.
Ina maana:
a. JK hakuvunja Sekretariati ya Halmashauri Kuu kwani hana madaraka hayo
b. JK hakuvunja Kamati Kuu kwani hana madaraka hayo
c. JK hakumuondoa mtu yeyote uongozi
Hii ina maana kuwa lolote lililotokea Dodoma limetokana na NEC au CC; na hii ina maana ya kwamba wale watu waliokuwa wanaonekana ni vigogo kweli na wana influence ndani ya Chama inawezekana hawana influence ambayo walidhania wanayo. The only x-factor katika hili lote ni kuwa Mwenyekiti wa CCM ndiye Rais vile vile na Katiba ya CCM haitoi maelekezo ya M/Kiti atumie madaraka yake vipi endapo ndiye Rais? Hivyo kama hana nguvu fulani kama mwenyekiti anaweza kutumia madaraka ya Urais kutimiza mambo mbalimbali.
Na hicho ndicho ambavyo kitakuwa kimetokea.
Mkuu,
Nafikiri umequote vipengele wrong. Kwanza kabisa tuanze na ibara ya 104 ambayo inasema kuwa kutakuwa na vikao vifuatavyo vya CCM vya Taifa:-
(1) Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa.
(2) Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.
(3) Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.
(4) Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (Zanzibar).
(5) Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.
(6) Sekretarieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.
(7) Kamati ya Wabunge wote wa CCM.
(8) Kamati ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wote wa CCM (Zanzibar).
Kikao kilichoanza jana ni Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa. Nakubali Ibara ya 107(22) inaipa mamlaka Halimashauri kuu ya Taifa
kumwachisha au kumfukuza Uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho ulifanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa. Swali linakuja, je Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa ina mamlaka gani ya kuteua viongozi wa chama? Ibara ya 107(12) inasema kuwa Halimashauri Kuu ya Taifa inayo mamlaka ya kuteua Makatibu wa CCM wa Mikoa. Hakuna sehemu nyingine kwenye hiyo ibara inayoonyesha kama Halimashauri ya Taifa inaweza kuteuwa watu wengine zaidi ya makatibu wa Mikoa. Kwa mantiki hiyo Halimashauri Kuu ya Taifa haiwezi kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yoyote kwenye Ibara ya 107(12) isipokuwa Makatibu wa Mikoa ambao ndio imewateua.
Ninafikiri the relevant provsion ni Ibara ya 107(8) ambayo inasema kuwa kazi za Halimashauri kuu ya taifa ni pamoja na
Kudumisha uangalizi juu ya vitendo vya Wanachama na Viongozi wa CCM na endapo itadhihirika kwamba tabia na mwenendo wa Mwanachama fulani vinamwondolea sifa za Uanachama au Uongozi itakuwa na uwezo wa kumwachisha au kumfukuza Uanachama au Uongozi alio nao.
Umeghusia Ibara ya 107(21) ya kumsimamisha Mwenyekiti wa CCM au Makamu Mwenyekiti wa CCM iwapo mwenendo na utendaji wao wa kazi vinamwondolea sifa za uongozi. Sijaelewa hiki kipengele kinaingiaje hapa kwani wanaoshukiwa kuachishwa au kusimamishwa uongozi sio Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti.
Nakubaliana na wewe Mwenyekiti wa CCM hana madaraka yoyote ya kumsimamisha kiongozi yoyote uongozi. Pia kwa kuongezea hapo hana mamlaka yoyote ya kuvunja hivyo vyombo vinane nilivyovitaja hapo juu, ikiwemo Sekretarieti ya Halimashauri kuu ya Taifa. Yaani katiba ya CCM inambana sana Mwenyekiti wao katika kutoa maamuzi lakini akiwa rais katiba yetu inampa madaraka luluki. I don't get it! Pia inaonyesha kuwa kama kwenye hivyo vikao kukiwa na rebels wa kutosha mwenyeti anaweza kuondolewa kiulani. Mwenyekiti kama Mwenyekiti ni toothless.
Umeghusia kuwa kwa vile hana mamlaka kama mwenyekiti then anaweza kutumia madaraka ya Urais kutimiza mambo mbalimbali. How? If that is possible then anaweza pia kutumia madaraka yake ya urais kumsimamisha uongozi kiongozi wa chama cha upinzani au kuvunja sekretarieti ya ya chama kingine?
Ibara ya 37(1) ya katiba inasema kuwa mbali na kuzingatia masharti yali yomo katika Katiba hii, na sheria za Jamhuri ya Muungano katika utendaji wa kazi na shughuli zake, Rais atakuwa huru na hatalazimika kufuata ushauri atakaopewa na mtu yeyote, isipokuwa tu pale anapotakiwa na Katiba hii au na sheria nyingine yoyote kufanya jambo lolote kulingana na ushauri anaopewa na mtu au mamlaka yoyote. Bado sioni ni jinsi anaweza kutumia hiki kifungu.
Unless uamuzi umefanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, Kikwete kama mwenyekiti wa CCM hawezi kufanya maamuzi yoyote ya kichama yeye mwenyewe. labda atumie udictator. Is he actually the leader of this revolutionary party? Compare him with Gaddafi - the leader of the revolution.