Wana CCM naomba mnisaidie, maana naona kuna watu wanaweza kuwa wanashangilia mafisadi kuvuliwa nyadhifa zao ndani ya Chama na kumbe uvuliwaji huo umefanyika kimakosa.
Kulingana na Katiba ya CCM ni nani au kikao gani chenye maamuzi ya kumvua kiongozi wa CCM uongozi kwenye ngazi ya Kamati Kuu au NEC?
Chenge alikuwa Mjumbe wa CC kwa kigezo kwamba alipata kura nyingi kwenye uchaguzi wa wajumbe wa NEC kupitia vile viti 20 vya Bara. Je, replacement yake itafanyika vipi?
RA aliingia kwenye CC kwa njia ipi? AU ndio wale wateule wachache wa Mwenyekiti?
Kama Kamati Kuu imevunjwa, je ilivunjwa baada ya kuwavua uongozi hao watuhumiwa?
Mantiki ya kuvunja CC iko wapi? Maana wajumbe wengi wanaingia huko kwa Nyadhifa zao mfano, wenyeviti wote wa Jumuiya za Chama, Spika, Makamu Mwenyekiti Bara na Visiwani, Katibu Mkuu, nadhani na manaibu wake wa Bara na Visiwani. Waliobaki wengine akina Mkapa, Mwinyi na wengineo kibao wanaingia kwa kuwa walishawahi kuwa viongozi wa kitaifa wa CCM.
Je, kuvunja CC sasa hivi ina maana kwamba Kikwete ataleta sura mpya ndani ya CC? Atazipataje na ilihali uchaguzi wa CCM ni mwakani?
Hapo sioni kama JK ametatua mgogoro wa CCM, tatizo siyo Lowassa, RA na Chenge, tatizo ni kundi zima lililo nyuma ya hao mafisadi na hao ndio wamekuwa vinara wa kuongoza utetezi dhidi ya mafisadi na hao ndio waliojaa kwenye NEC. Ngoja tusubiri kesho.
Kama NEC ikibariki hayo maamuzi, basi tusubiri vita kuu ndani ya CCM, hakuna atakayepona. Vita vya panzi ni furaha ya kunguru, wapinzani kazeni buti Ikulu inazidi kuwa wazi na hili limetokea kipindi kizuri sana, inawezekana kabisa wabunge wa CCM wanaweza kuungana na wabunge wa upinzani kuupinga mswaada wa Katiba Mpya, maana hawajui kesho watakuwa wapi.
Kikwete aliingia madarakani kwa siasa za makundi akisaidiwa na ufisadi wa EPA ambao ulimpa fedha za kampeni. Ni makundi hayo hayo na ufisadi huo huo ndio ambao utasababisha CCM imfie mikononi mwake.