Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Kweli inachanganya. hata mimi nilikuwa nafikiri NEC imekaa jana lakini gazeti la Mwananchi linasema kuwa wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC-CCM), wameendelea kuvutana na kusababisha kuahirishwa kwa Mkutano wa Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho kilichokuwa kianze jana. Kikao cha CC ambacho kilianza juzi jioni kilitarajiwa kumalizika usiku wa siku hiyo na jana kilikuwa kifanyike kikao cha NEC, ajenda kuu ikiwa ni kujadili tathmini ya Mchaguzi Mkuu uliopita. Hata hivyo, Kamati Kuu iliyoanza kikao saa 10 jioni juzi, iliahirisha kikao chake saa 1:00 usiku na kurejea tena saa 3:00 hadi saa 5:00 usiku, bila kumaliza kupanga ajenda za NEC. Kwa hiyo hata NEC haijakaa then.

Ahsante EMT.
Kwa mantiki ni kuwa sekretariati imevunjwa wakati CC ikiandaa agenda za kikao cha NEC kwa taratibu za CCM.
CC wanaingia wajumbe wa kuchaguliwa na wale wanaoingia kwa heshima zao kama marais wastaafu.
NEC wanaingia wajumbe wa kuchaguliwa na wale wa heshima kama mawaziri wakuu wastaafu.

Kikao cha NEC cha Butima kiligubikwa mjadala mkali sana wa ufisadi. Kabla ya kikao, wenyeviti wa CCM wa mikoa chini ya mwenyeji wa mkutano Makongoro Nyerere waliazimia wale wanaokichafua chama wafukuzwe. Hoja yao iliungwa mkono na wazee wastaafu wakiwamo mawaziri wakuu na wanafunzi wa kweli wa Mwalimu Nyerere. Hoja ilizimwa kibabe na mwenyekiti ili kuokoa wanamtandao waliomsaidia kufika hapo.

Uchaguzi uliopita pamoja na viongozi kuficha ukweli kwa maneno ya kejeli umewatisha sana CCM. Kuingiliwa ngome za Dar, Mbeya na Mwanza haikuwa dalili nzuri. Hii imelazimisha baadhi yao wakubali ukweli kuwa ufisadi na kashfa kama za Richmond na Dowans vimechangia sana, na kibaya zaidi wahusika ni viongozi ndani ya chama na kuharibu taswira nzima ya chama.
Wajumbe wengi wa NEC wamedhamiria kukinusuru chama wakiungwa mkono kichini chini na wastaafu maarufu. Nguvu ya kundi la mafisadi ndani ya NEC imepungua.

Uwezekano wa NEC kujadili hoja za kushindwa kwa chama unaweza kuleta mpasuko na uwezekano wa watuhumiwa kupoteza nyadhifa zao kichama au kufukuzwa. Ili kupunguza jazba,mwenyekiti amevunja sekretariati inayolaumiwa kwa utendaji mbovu kama njia ya kuua agenda hiyo kwa vile suala limeshughulikiwa (pre-emptive strategy). Hii itawaokoa watuhumiwa kutojadiliwa mbele ya NEC kwa kina kuzuia jaribio kama la Butiama kuweza kujirudia kwa nguvu zaidi.

Kuwafukuza uanachama kundi lenye nguvu kifedha ni jambo lisilowezekana ikizingatiwa kuwa limeshajipanga vema ndani ya CC, NEC na bunge. Jambo linalofanyika hapa ni 'funika kombe mwanaharamu apite'. Ni mbinu ya hali ya juu sana kuwanusuru watuhumiwa kwa kupunguza nguvu za hoja iliyoko mbele kwa majibu kuwa chama kipo mbioni kujiunda upya na kipewe nafasi.
Mabadiliko hayatalenga kujivua gamba bali kufunika kombe. Hii itakuwa sawa na kunywa 'asprin' homa ipungue bila kutibu tatizo.
Kwa maoni yangu kama hatua kali hazitachukuliwa dhidi ya watuhumiwa ikiwa ni pamoja na kuvuliwa nyadhifa au kufukuzwa, hakutakuwa na mabadiliko yoyote na itakuwa ni njia rahisi ya kukipeleka chama kule UNIP na KANU zilipopunzika.
 
TBC1 Bulletin imemnukuu Chilligati akiongea na waandishi wa habari akisema:


  1. CC imejiuzulu
  2. Sekretariat kuu ya CCM imejiuzulu
Amedai nia ni kumsaidia mwenyekiti kukijenga chama upya kama ilivyokubalika ajali.

Alipoulizwa kama wanajiuzulu kwa sababu ya pressure ya UV-CCM kuwa CC imeshindwa kumsaidia Rais na mwenyekiti JK, Chilligati alibeza UV-CCM kuwa wanajisemea tu lakini wao hawajalazimishwa na UV-CCM.
Sasa NANI kawalazimisha?
 
Wakuu,

Nipo maeneo ambayo huenda nikawapasha kidogo juu ya nini kinaendelea hapa, naweza kuwa natoweka online lakini nitawapa dondoo za kinachoendelea.

Wakuu hapa wanajadili nini kifanyike dhidi ya wanaokipaka matope chama, hapa namaanisha watuhumiwa wa ufisadi pamoja na mzee Makamba.

Nashukuru MUNGU Kuwa tuna Mashushushu ndani ya CC na NEC za CCM....Endeleeni kutupasha Habari...na Mkiacha ushushushu Tunawakaribisha CHADEMA Ila mkifika kwetu Tabia zenu za Ushushushu mziache
 
quote_icon.png
Originally Posted by Superman
TBC1 Bulletin imemnukuu Chilligati akiongea na waandishi wa habari akisema:

  1. CC imejiuzulu
  2. Sekretariat kuu ya CCM imejiuzulu
Amedai nia ni kumsaidia mwenyekiti kukijenga chama upya kama ilivyokubalika ajali.

Alipoulizwa kama wanajiuzulu kwa sababu ya pressure ya UV-CCM kuwa CC imeshindwa kumsaidia Rais na mwenyekiti JK, Chilligati alibeza UV-CCM kuwa wanajisemea tu lakini wao hawajalazimishwa na UV-CCM.

Sasa walipoambiwa kuwa chama chao kimeoza walikuwa wanabisha nini? Sasa wajifunze kuwa kuna watu wana akili zaidi yao nje ya CCM
 
Wajemeni, mimi nakubali JK amefanya maamuzi magumu ila kwa mijibu wa katiba ya CCM M/kiti hana uwezo wa kuivunja CC wala Secretariat ila alichofanya JK ni kuwalazimisha kujiuzulu wenyenye ili kutimiza masharti ya katiba yao ambayo inaruhusu kujiuzulu kwa hiyari.

Hivyo credit ya JK ni kitendo tuu cha kutoa shinikizo CC ijiuzulu kwa lazima huku wakijinadi ni kwa hiari kama alivyofanyiwa Jumbe kule nyuma, alipewa kibano CC na kusainishwa kinguvu barua ya kujiuzulu na NEC kupewa taarifa. Ndicho kitakachofanyika Dodoma asubuhi hii kwa NEC kupokea taarifa ya ajenda zilizotayarishwa na CC kabka ya kujiuzulu hivyo ufanyike uchaguzi wa CC mpya na Secretariat yake.
 
Hawana lolote nchi ishawashinda hii....wanatuletea usanii tu hapa. Hata wafanyenini, CCM ishapoteza mvuto wake kwenye macho na akili za watanzania....achilia mbali kujivua gamba.... hata wakisema wajichune ngozi na kubadilisha damu yao kwa kuiingiza mpya,bado haitasaidia kitu.
ccm imechokwa na hatuitaki tena....Hata KANU ya kenya walifanya hayo yote lakini mwisho wa siku KANU kikajifia na kutokomea kusiko julikana.
lol ccm! acha niiteme mate twuuuuh....
 
bila ya mafisadi kukalia madebe segerea, bado hakuna kujivua gamba hapo
 
Wajemeni, mimi nakubali JK amefanya maamuzi magumu ila kwa mijibu wa katiba ya CCM M/kiti hana uwezo wa kuivunja CC wala Secretariat ila alichofanya JK ni kuwalazimisha kujiuzulu wenyenye ili kutimiza masharti ya katiba yao ambayo inaruhusu kujiuzulu kwa hiyari. Hivyo credit ya JK ni kitendo tuu cha kutoa shinikizo CC ijiuzulu kwa lazima huku wakijinadi ni kwa hiari kama alivyofanyiwa Jumbe kule nyuma, alipewa kibano CC na kusainishwa kinguvu barua ya kujiuzulu na NEC kupewa taarifa. Ndicho kitakachofanyika Dodoma asubuhi hii kwa NEC kupokea taarifa ya ajenda zilizotayarishwa na CC kabka ya kujiuzulu hivyo ufanyike uchaguzi wa CC mpya na Secretariat yake.

Mashabiki wa JK uwa mnatafuta jinsi ya kum-link JK na mafanikio. Si leo tu, kama kuna jema serikali utasikia JK kaamua lakini baya likiwepo utasikia hawa ni wanaotaka kumuharibia JK!

Soma habari ya Mwananchi utajua kuwa JK alikuwa anapinga sekeretarieti kujiuzulu, je iweje useme amewalazimisha kujiuzulu?????

TAFAKARI NA CHUKUA HATUA.......!



 
Bomoa bomoa, ijengwe upya. Saga meno, tupa nje taka nunua vyombo vipya. Fanya kweli JK. Ikibidi tembeza mabomu ya machozi:angry:
 
Mh, tafsiri ya hii picha ni ndefu. Je ni kweli au ni technology tu ndio imepakaza, maana siamini macho yangu.

Vipi hii picha hapa chini
GO9G5089.JPG

Nani anataka kujiunga na ccm kama sio mwendawazimu?[/QUOTE]
 
Kazi ipo hapa ndipo kipimo cha uwezo wa JK utaoneka katika mikakati na muelekeo wa chama hapo siku za usoni, lakn upande mwingine sekretariet itakayochaguliwa itakuwa na changamoto ya kujipanga na kuweka mikakati kuelekea uchaguz ujao
 
he! Hii bomoabomoa haikukutana na resistance kama ile ya Tegeta!!
 
Huo ni mwanzo tu shughuli baaaado! Waache wapigane mieleka sisi tuuchukue ubingwa jangwani kiulaiiini............tehe tehe!
 
Hata CCM wageuze vipi viongozi, kwangu naona ni sawa na samaki kudondoka toka kwenye flampeni na kuangukia kwenye makaa ya moto, bado ataendelea kuungua tuuuuuu!
Hiki chama kife tu, we are TIRED!
 
JAKAYA KIKWETE AVUNJA SEKRETARIETI YA CCM

kikwete%252Bpemba.jpg


MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amevunja sekretarieti ya chama hicho inayoongozwa na Katibu Mkuu, Yusuf Makamba, hatua inayoelezwa kufuatiwa na maamuzi mazito zaidi.

Uamuzi huo wa Kikwete umefanyika usiku huu, huku hali ikiendelea kuwa tete mjini Dodoma kunakofanyika vikao vya chama hicho vilivyotanguliwa na sekretarieti na baadae Kamati Kuu.

Kwa mujibu wa habari hizo, Kikwete toka jana ameonekana kuwa mkali na ambaye amekua akitembea na ajenda mkononi huku wasaidizi wake wengine wakiwa hawaelewi undani wa ajenda yake ya mageuzi mazito ndani ya CCM.

‎​Moto ulianza kuwashwa katika kikao cha Kamati Kuu ambako zile tetesi kwamba kuna mkakati wa kumuondoa Kikwete zilipodhihiri kuwa kweli ilipoibuka ndani ya Kamati Kuu hoja ya “kutenganisha kofia za Urais na Uenyekiti”

Taarifa ambazo zinasema Kikwete alipoona hoja hiyo imetajwa ndipo alipobaini kuwa “sasa mafisadi wamepania kumng’oa”.

Katika kamati kuu hoja ilikua ni nini kifanyike kuwadhibiti watuhumiwa wa ufisadi na pia kuhusu hatima ya Makamba.

imeelezwa kuwa Kikwete anayo ripoti ya kitaalamu ikielezea sababu za yeye kupata asilimia 60 katika uchaguzi wa mwaka 2010 na kwamba ilipendekeza kuwa mafisadi watoswe.

Imeelezwa kwamba mjadala wa vikao vya Dodoma utazingatia hotuba ya Kikwete katika sherehe za CCM Februari 5, 2011.

Katika hotuba hiyo Kikwete alisema;

“Hatuwezi kuacha jukumu la kugharamia uendeshaji wa Chama chetu mikononi mwa wafadhili matajiri. Tunahatarisha uhuru wa Chama chetu.

“Chama cha Mapinduzi kiige tabia ya nyoka ya kila baada ya muda fulani hujivua gamba lake na kupata jipya.

“Hatuna budi kufanya hivyo na kufanya hivyo sasa. Wakati wa vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa vya tathmini tutalijadili pia suala zima la mageuzi katika Chama.

“Nitapenda tuelewane juu ya namna tutakavyotekeleza agenda hii muhimu kwa uhai na maendeleo ya Chama chetu. Hili ndugu zangu haliepukiki.

“Lazima tukihuishe ili kukiongezea mvuto mbele ya watu. Tuutazame muundo wetu kama unakidhi haja.

“Tuwatazame viongozi watendaji kama wanakidhi haja na kama siyo mzigo unaokipaka matope Chama chetu. Wale tunaoweza kuachana nao sasa tuachane nao kwa maslahi mapana ya Chama chetu.”

MATUKIO UK: JAKAYA KIKWETE AVUNJA SEKRETARIETI YA CCM

Mtazamo:

Mpasuko ndani ya CCM unakifanya chama hiki kupoteza mvuto na mwelekeo. Mambo mengi yanayokitafuta kwa mtazamo wa juu juu wa mwenyekiti wake unaoekana kana kwamba chanzo ni ndani ya chama. Lakini kwa upeo mpana, mengi yanahusiana na matatizo yaliyomo katika Serikali ya chama hicho.

Maamuzi ya kichama yanataka yahusishwe na Serikali (wapo wanachama wasio na sifa lakini wamepewa nguvu za maamuzi katika Serikali huko ndiko wanakotumia madaraka yao kuongoza mambo yaende kwa maslahi yao au ya wale waliowapepetea kuingia madarakani). Kuvunja Sekretariati pengine hakuwezi kusaidia sana kwani wajumbe wengi wa vikao vikuu vya chama hicho ambao hawaridhiki kwa kiasi kikubwa na utendaji wa Serikali ya chama pampoja na uongozi mzima na maamuzi ya chama hicho akiwemo mzee Six, Mwakyembe na wale wa mfano wake wapo katika ngazi za juu za Serikali ya chama hicho. Pengine tungedhani JK atarejea na kuifumuafumua Serikali yake na kuipanga upya ili CCM na Serikali yake ikubalike vilivyo kwa wananchi.
 
JK bwana ananifurahisha sana jinsi anavofanya kazi..yaani anafanya kazi as if ni mwenyekiti wangu wa mtaa kule kunduchi mtongani...yaani hafai na hawezi kuwa mwenyekiti wa chama...hivi hamuoni mkapa alipokuwa mwenyekiti na mangula katibu mkuuu
 
Back
Top Bottom