Mali za Kapteni Komba kupigwa mnada na CRDB

Mali za Kapteni Komba kupigwa mnada na CRDB

Pasco hebu tuweke sawa, zile list ndeeefu zinazotoka magazetini zikitangaziwa minada ya mali za wadaiwa wa mabenki, ndio ukosefu wa hii privacy unayoisema hapa? Nafikiri mpaka wafike hatua hii watakuwa wameshawasiliana na wadaiwa wao sugu kwa kipindi cha kutosha tu...

Huyo kaka msomi utamuweza basi! Anasema ili mradi tu naye aonekane anajua jua sheria (hata kama ha-make sense yoyote ile).

Good catch!
 
Pasco hebu tuweke sawa, zile list ndeeefu zinazotoka magazetini zikitangaziwa minada ya mali za wadaiwa wa mabenki, ndio ukosefu wa hii privacy unayoisema hapa? Nafikiri mpaka wafike hatua hii watakuwa wameshawasiliana na wadaiwa wao sugu kwa kipindi cha kutosha tu...
Dina, unapokopeshwa na benki, miongoni mwa vipengele vya mkopaji na mkopeshwaji ni kipengele cha confidentiality, kama ili kwa mwanasheria na mteja wake, mwalimu na mwanafunzi, daktari na mgonjwa, benker na mteja etc!.

Kwenye ulimwengu wa biashara kuna kinaitwa "corporate veil", unapokopeshwa kama kampuni, jina rasmi la kutumika ni jina la taasisi, benki hairuhusiwi to dislose details za wadeni wake, mpaka kwanza waende mahakamani kuomba kibali cha ku unveil ile corporate veil, ndipo wamiliki wanakuwa disclosed na kushitakiwa as individuals!.

Bahati mbaya wengi humu ni vijana wajuzi juzi tuu, kwa wale wazamani wanaweza kukumbuka kisa cha Gazeti la Mtanzania na Banki ya NBC kushitakiwa katika kesi ya madai ya mabilioni ya shilingi, baada ya gazeti hilo kutoa story ya jinsi tajirti fulani anavyodaiwa na NBC.

Tajiri yule alikwenda mahakamani kuishitaki NBC kwa breach of confidentiality kwa ku leak details za madeni ya mteja, mshtakiwa wa pili lilikuwa ni gazeti la Mtanzania enzi hizo chini ya Generali Ulimwengu, ilikuwa gazeti lifilisiwe!. NBC na Mtanzania waka opt for out of court, wakamalizana!.

Japo siyajui mazingira haswa ya deni husika, Komba ni VIP, Mhe. Mbunge, Mjumbe wa NEC ya CCM ni heavy weight, kitendo cha kutajwa tuu anadaiwa ni aibu!. Miradi yake kudaiwa is fine not him!. Kuandika kuwa anafilisiwa kwa kumtaja jina at personal capacity ni kumchafulia jina!. Akipata mwanasheria nguli, anafungua kesi ya madai kuchafuliwa jina na anashinda!.

Pasco.
 
Kwani CRDB wanamtangaza mtu au wanatangaza mnada? Na Komba alitumia jina gani wakati anakopa?
Hili neno!, unaikumbuka kesi ya tycoon wetu pale gazeti la Mtanzania lilipomuandika ni mdaiwa wa NBC?!.

Kudaiwa sio kosa la jinai, ila kutajwa kwa jina kuwa unadaiwa ni kuvunjiana heshima na kuchafuliana majina!.
Pasco
 
Japo siyajui mazingira haswa ya deni husika, Komba ni VIP, Mhe. Mbunge, Mjumbe wa NEC ya CCM ni heavy weight, kitendo cha kutajwa tuu anadaiwa ni aibu!. Miradi yake kudaiwa is fine not him!. Kuandika kuwa anafilisiwa kwa kumtaja jina at personal capacity ni kumchafulia jina!. Akipata mwanasheria nguli, anafungua kesi ya madai kuchafuliwa jina na anashinda!.Pasco.

Unaandika kwa certitude as if you know the ins and outs of the situation. Una uhakika gani wewe kuwa akipata mwanasheria nguli na akifungua kesi ya madai kuwa atashinda?

Nini kinakufanya uwe na uhakika kuwa atashinda?
 
poverty=You spend too much, You do not save enough,You have to much debit,You put all your eggs in one basket, You do not have insurance,You do not invest in yourself,You do not have goals and plans,You are not patient and persistence,You do not give back and You keep doing the same thing.
Excel njoo ufafanue hii paragraph ili niielewe vizuri
 
Last edited by a moderator:
Angewekeza tu kwenye mikwaya yake ya CCM shule atuachie walimu.

Pia alitakiwa kujifunza kwa shule za CCM
 
poverty=You spend too much, You do not save enough,You have to much debit,You put all your eggs in one basket, You do not have insurance,You do not invest in yourself,You do not have goals and plans,You are not patient and persistence,You do not give back and You keep doing the same thing.
Excel njoo ufafanue hii paragraph ili niielewe vizuri
mkuu hiyo signature?

hayo ni mambo kumi ambayo yanadidimiza maendeleo na kuleta umasikini bwana!

1.You spend too much.. unaona hapo, yani una matumizi makubwa kuliko mapato, hivyo unapelekea kwenda mikoponi!

2.You do not save enough.. hapa hivi, Warren Buffet aliwahi sema kuwa, spend what is left after saving! hivyo alimaanisha kwamba save more and more as you can instead of spending..

3.You have to much debit, madeni yakizidi kile unachopata, halafu madeni hayo pia yakiwa katika non productive debts, hapo ndipo tunapokuwa na shida kaka.

4.You put all your eggs in one basket. unashauriwa kuwa, unapokuwa na pesa ukiwa na lengo la kuwekeza, usizielekeze pesa zooote katika biashara moja, huwezi jua nini kinakuja mbele, je likitokea janga katika biashara uliyowekeza itakuwaje? si ndio mwanzo wa kuchanganyikiwa? hivyo, tunashauriwa kuwa na decentralization katika biashara!

Mkuu mpaka hapo tuko pamoja?
 
Ndo maana anamuunga mkono lowasa; ili amkopeshe ............................. Janja sana


KUMBE NA WEWE UMEIONA HIYO JANJA YA KOMBA KUMPIGIA DEBE lOWASSA ILI AKIINGIA MAGOGONI AMSAIDIE KULIPA DENI!!! UJINGA WA HAWA WABUNGE WA MAGAMBA NI PALE WANAPOCHANGANYA SIASA NA BIASHARA!!!
 
ni leo kwenye vyombo vya habari tumeskia kwamba mali za mmbunge Kapteni John Komba zitapigwa mnada kwa kudaiwa na benk ya crdb zaidi ya billion moja fedha ambazo ameshindwa kurudisha. Swali langu ni je kwa nini mtu ukope zaidi ya uwezo wako wa kurejesha? Jamani hili liwe fundisho kwetu sisi. Ni kweli saa nyingine tunakuwa na tamaa ya kukopa na kuanzisha biashara ili kufanikiwa haraka. Ila kaa ukijua kuwa biashara hata siku moja haitabiriki

Ndio watu waamini maneno ya msigwa juu ya viongozi wa chama cha ....... kuwa na uwezo mdogo
 
Benki ya CRDB iko njiani kufilisi mali za mheshimiwa Kapteni John Komba kutokana na kushindwa kulipa deni . Ikiwepo shule zake kupigwa mnana.

Jumla ya deni lote ni shilingi bilioni moja za kitanzania.

======

TUNAWAOMBA WASISAhAU KUUNGANISHA NA ZILE MALI ZA TOT ALIZOJIKATIA , SHUKRANI KWA MAKAMBA aliyesema huyu ni ' MWENZETU '
 
KUMBE NA WEWE UMEIONA HIYO JANJA YA KOMBA KUMPIGIA DEBE lOWASSA ILI AKIINGIA MAGOGONI AMSAIDIE KULIPA DENI!!! UJINGA WA HAWA WABUNGE WA MAGAMBA NI PALE WANAPOCHANGANYA SIASA NA BIASHARA!!!

hivi jitu kama hilo likiingia jela itakuwaje aisee !
 
Unaandika kwa certitude as if you know the ins and outs of the situation. Una uhakika gani wewe kuwa akipata mwanasheria nguli na akifungua kesi ya madai kuwa atashinda?

Nini kinakufanya uwe na uhakika kuwa atashinda?

BHANA WEE ! Hii nchi kila ' mdukuzi ' ni mshindi ! Yetu macho !
 
Benki ya CRDB iko njiani kufilisi mali za mheshimiwa Kapteni John Komba kutokana na kushindwa kulipa deni . Ikiwepo shule zake kupigwa mnana.

Jumla ya deni lote ni shilingi bilioni moja za kitanzania.

======


Habari


Mali za mbunge kupigwa mnada

Mwandishi Wetu Toleo la 359 25 Jun 2014

359_komba.jpg



  • Waziri Mkuu Pinda aingilia bila mafanikio

ZIMESALIA siku tano tu, kuanzia Jumatano wiki hii, kabla ya baadhi ya mali za Mbunge maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kapteni John Komba, kupigwa mnada ili kufidia deni kubwa alilonalo katika Benki ya CRDB.

Kwa mujibu wa nyaraka mbalimbali zilizopatikana, Komba anayemiliki shule kadhaa jijini Dar es Salaam, ikiwamo ya Bakili Muluzi, anadaiwa na Benki ya CRDB zaidi ya Sh bilioni moja, ikiwa ni deni la msingi pamoja na riba ya asilimia 17 katika miaka mitano anayodaiwa kushindwa kulipa deni hilo.


Deni la msingi ni Sh milioni 900, lililotolewa katika mikupuo miwili; kwanza Sh milioni 300 na baadaye Sh milioni 600, baada ya maombi ya mkopo aliyoyatuma CRDB mwaka 2007, kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa madarasa, nyumba za wafanyakazi, mabweni, uchimbaji wa visima na ununuzi wa samani kwa ajili ya madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule yake hiyo ya Bakili Muluzi.


Marejesho ya mkopo huo uliopaswa kulipwa ndani ya miaka mitano, yalitakiwa kufanyika katika mikupuo 22 na kumalizika Juni 30, 2014.


“Januari 14, 2009, Mbunge huyo alipewa na CRDB mkopo wa jumla ya Sh milioni 900 zilizopaswa kulipwa kwa ‘installments’ (mikupuo) 22 na kukamilika Juni 30, 2014,” alisema mtoa habari wetu ambaye ni wazi jina lake hatuwezi kuliweka gazetini kwa sasa.


Katika makubaliano hayo, mbunge huyo kupitia taasisi isiyo ya kiserikali (NGO) anayoimiliki, alipewa ‘grace period’ (kipindi cha muda wa matazamio) wa miezi sita, lakini hata alipoanza kulipa, malipo yake hayakwenda kama ilivyotarajiwa.


“Dhamana ya mkopo huo iliyowekwa benki ni hati tatu za viwanja anavyovimiliki namba 121244 (Plot No, 167/1 Block 1), namba 121245 (Plot No 167/2 Block 1 na namba 55920 (Plot No 1030) vyote vipo Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam,” alisema mtoa habari wetu huku nyaraka kadhaa zikithibitisha.


Uchunguzi zaidi wa Raia Mwema ulibaini kuwapo kwa jitihada za dhati za Mbunge huyo kulilipa deni lake hilo, lakini hadi Aprili 16, mwaka jana, alikuwa amelipa malimbikizo ya deni ya Sh 214,126,678 ambapo Sh 146,126,678 zililipwa katika Akaunti ya Benki ya CRDB, Lumumba namba 01J1008525300.


Fedha nyingine kati ya hizo ambazo ni Sh 68,000,000 zililipwa kwa Mbunge huyo na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) katika akaunti yake iliyopo CRDB Tawi la Kijitonyama, jijini Dar es Salaam na kisha yeye mwenyewe akazihamishia Tawi la CRDB Lumumba.

Gazeti hili halikuweza kufahamu mara moja sababu za TACAIDS kumlipa Mbunge huyo kiasi hicho kikubwa cha fedha.

Kutokana na kuchelewa kulipa deni katika mtiririko waliokubaliana, hadi Novemba 2011, miaka miwili tu tangu apewe mkopo huo, deni hilo liliongezeka na kufikia Sh 1,252,110,349.14, kitendo kilichosababisha Benki ya CRDB kutafuta dalali wa Mahakama na kumtaka akamate mali za mbunge huyo na kuzipiga mnada wa hadhara.


Dalali huyo, Bani Investment Limited, alipewa kazi hiyo Februari 8 mwaka jana, lakini kabla ya kufanya hivyo, Mbunge alikimbilia Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kuweka pingamizi, ingawa tayari wanafunzi kadhaa wa shule anazozimiliki walilazimika kuhamia shule nyingine kutokana na kutofahamu mustakabali wao.


“Wakati wa mgogoro kati yake na CRDB, Mbunge huyo alikuwa akihaha kuhamisha umiliki wa shule zake, kiasi cha kufikia makubaliano na kampuni ya IKS Tanzania kuiendesha moja ya shule zake kwa miaka mitano huku ikilipa deni hilo kwa niaba ya Mbunge, lakini suala hilo lilishindikana,” taarifa zaidi zinafafanua.


Baada ya kuona kuwa suala hilo linazidi kuwa gumu kwake, Raia Mwema linafahamu kwamba, Mbunge huyo ambaye ana uhusiano mzuri na baadhi ya viongozi wa juu wa CCM na Serikali, aliiomba Ofisi ya Waziri Mkuu (PMO) kuingilia kati suala hilo na kumshawishi Mkurugenzi wa CRDB, Dk. Charles Kimei, amuongezee muda wa kulipa deni lake.


Aprili 23, 2012, PMO ilimwandikia barua Dk. Kimei ikimshawishi kuangalia uwezekano wa kumwongezea muda wakati huo Serikali inatafuta namna stahiki ya kumsaidia kwa kuzinunua shule zake, lakini CRDB iliendelea na msimamo wake wa kutoongeza muda zaidi.


Machi 21 mwaka jana, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliijibu barua ya Mbunge huyo ya Februari 20 mwaka huo huo ambayo haikuwa na kumbukumbu namba, ikimtaarifu kuwa pamoja na kupokewa kwa barua hiyo, Taarifa zilizokifikia chumba cha habari zilisema kwamba, maombi ya Jiji kununua shule na ardhi anayoimiliki, kwamba yatashughulikiwa na Kamati ya Huduma za Jamii; na hadi sasa hakuna majibu aliyopewa.


Kwa sasa, zikiwa zimesalia siku hizo tano tu kufika Juni 30, 2014 ambayo ni siku ya mwisho wa makubaliano, CRDB imekuwa ikiiomba Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kuiruhusu kuuza mali zote za Mbunge huyo kufidia deni lao, lakini Mbunge anadai kuwa thamani ya shule zake na ardhi ipatayo mita za mraba 34,735, ni zaidi ya deni analodaiwa.


Mbunge huyo pamoja na mkurugenzi wa CRDB Dk. Charles Kimei hawakuweza kupatikana hadi tunakwenda mitamboni, simu ya Dk. Kimei ikiita bila majibu wakati simu ya Komba ambaye mwandishi wetu hakuweza kumpata licha ya kumfuatilia bungeni mjini Dodoma ana kwa ana, haikuweza pia kupatikana.



- See more at: Raia Mwema - Mali za mbunge kupigwa mnada - See more at: Raia Mwema - Mali za mbunge kupigwa mnada
 
Back
Top Bottom