Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,129
- 35,153
Nimefuatilia mwitikio wa waumini wa kanisa la Lutheran hapa Tanzania (KKKT) baada ya Askofu Alex Malasusa kuchaguliwa kuwa askofu mkuu wa kanisa hilo hapa Tanzania. Hali imekuwa tofauti kidogo, kwa waumini kadhaa ambao nimefanikiwa kuwasikiliza ni kama vile hawajafurahia hilo au wamechukizwa kimtindo. Hili nimeligundua zaidi kwa waumini wa dayosisi ya Mashariki na Pwani (dayosisi ambayo inaongozwa na Askofu Malasusa takribani miaka 20 sasa). Machache niliyoweza kuyagundua yakisemwa (kwanini wamekwazika na kuchaguliwa kwa Malasusa) na wale ambao hawakufurahishwa na kuchaguliwa kwa Askofu Malasusa ni haya;
1. Askofu Malasusa kukaa muda mrefu kupitiliza katika dayosisi ya Mashariki na Pwani huku akibadilisha katiba imruhusu kukaa hata milele. (Askofu Malasusa amekuwa askofu wa dayosisi ya Mashariki na Pwani kwa wastani wa miaka 20 sasa)
2. Kurudia kukalia nafasi hiyo hiyo ya uaskofu mkuu wa kanisa. (Miaka kadhaa nyuma alishakuwa askofu mkuu tena).
3. Skendo mbaya ya Uzinzi ya miaka kadhaa ya nyuma (Askofu Malasusa alihusishwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mchungaji mmoja wa kike ambaye alikuwa mke wa mtu, na mwenye mke alikuwa akipambania arejeshewe mke wake)
4. Misimamo kadhaa yenye utata kiimani ambayo hukinzana na baadhi ya wachungaji, mafundisho ya kilutheri au mafundisho mapya katika dayosisi ya Mashariki na Pwani (Malasusa aliwahi kuhusishwa na kuleta fundisho jipya la kuruhusu unywaji pombe kwa walutheri hapa Tanzanua, kupingana na mafundisho na mapokeo ya kilokole ndani ya kanisa la Lutheran)
5. Tabia za Askofu Malasusa kujipendekeza/kujihusisha na watawala hususani kipindi cha Magufuli kiasi cha kukinzana hadharani na misimamo rasmi ya kanisa la Lutherani hapa Tanzania. (Askofu Malasusa inasemekana alikuwa 'chawa' rasmi wa Magufuli na alikuwa mwiba mkali dhidi ya utawala wa Kikwete)
6. Ubabe na ukiritimba wa kimadaraka alionao Askofu Malasusa katika dayosisi ya Mashariki na Pwani. (Sakata la kutaka kumzimisha kinguvu mchungaji Kimaro wa Kijitonyama ni mfano mmojawapo)
Mtu msiyemtaka ndio huyo kaja sasa?
1. Askofu Malasusa kukaa muda mrefu kupitiliza katika dayosisi ya Mashariki na Pwani huku akibadilisha katiba imruhusu kukaa hata milele. (Askofu Malasusa amekuwa askofu wa dayosisi ya Mashariki na Pwani kwa wastani wa miaka 20 sasa)
2. Kurudia kukalia nafasi hiyo hiyo ya uaskofu mkuu wa kanisa. (Miaka kadhaa nyuma alishakuwa askofu mkuu tena).
3. Skendo mbaya ya Uzinzi ya miaka kadhaa ya nyuma (Askofu Malasusa alihusishwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mchungaji mmoja wa kike ambaye alikuwa mke wa mtu, na mwenye mke alikuwa akipambania arejeshewe mke wake)
4. Misimamo kadhaa yenye utata kiimani ambayo hukinzana na baadhi ya wachungaji, mafundisho ya kilutheri au mafundisho mapya katika dayosisi ya Mashariki na Pwani (Malasusa aliwahi kuhusishwa na kuleta fundisho jipya la kuruhusu unywaji pombe kwa walutheri hapa Tanzanua, kupingana na mafundisho na mapokeo ya kilokole ndani ya kanisa la Lutheran)
5. Tabia za Askofu Malasusa kujipendekeza/kujihusisha na watawala hususani kipindi cha Magufuli kiasi cha kukinzana hadharani na misimamo rasmi ya kanisa la Lutherani hapa Tanzania. (Askofu Malasusa inasemekana alikuwa 'chawa' rasmi wa Magufuli na alikuwa mwiba mkali dhidi ya utawala wa Kikwete)
6. Ubabe na ukiritimba wa kimadaraka alionao Askofu Malasusa katika dayosisi ya Mashariki na Pwani. (Sakata la kutaka kumzimisha kinguvu mchungaji Kimaro wa Kijitonyama ni mfano mmojawapo)
Mtu msiyemtaka ndio huyo kaja sasa?