Makonda kutoa Katapila 20 kusaidia kurekebisha barabara za Jimbo la Kawe

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,568

Katibu wa Itikadi , Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Paul Makonda leo Januari 19, 2024 ameahidi kukabidhi katapira 20 kwa mbunge wa jimbo la Kawe, Josephat Gwajima kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa barabara.

Makonda ametoa ahadi hiyo kutokana na wananchi wa jimbo hilo kulalamikia ubovu wa barabara, huku akiagiza katapila hizo zianze kazi mapema wiki inayokuja.

Sambamba na hilo, Makonda amempa maagizo Waziri wa Ardhi, Jerry Slaa kufika Bunju leo hii ili kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi katika eneo hilo.

Hii ni awamu ya pili ya ziara yake kitaifa ambapo anaangazia kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Pia Soma:
- DOKEZO - Ni aibu Kawe - Dar kuwa na Kituo cha Daladala cha hali hii. Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya na Mbunge wajitafakari

My Take:
Barabara na Kituo cha Kawe zimekuwa zikilalamikiwa miaka yote lakini sioni jitihada zozote zilizofanywa na na Mbunge wa Kawe Josephat Gwajima. Au ndiyo mambo ya Uchaguzi?
 
Ni kazi juu ya kazi huku mwenezi huku katibu mkuu.ni lazima upinzani wakate pumzi
IMG-20240119-WA0008.jpg
IMG-20240119-WA0014.jpg
IMG-20240119-WA0013.jpg
 
Mbunge wetu wa Kawe huyu. Huku Kawe hatutaki kusikia mtu mwingine zaidi ya Mh Makonda.
 
Nimekumbuka ile vita ya Gwajima na bwana Albert Malyangalya Bashite a.k.a Makonda.
 
Sasa milioni themanini Kila miezi mitatu itafanya nn Mzee?
Unamaanisha ni ndogo sana? kwa hiyo kama ndogo ndio mmeamua kuitafuna ili msubiri msaada wa Makonda?

Ok fine, kwani kukodisha katapila hata tano ili zikarekebishe maeneo yenye kasoro ndani ya jimbo, hizo pesa milioni themanini zisingetosha?

Anyway kuleni tu kwa urefu wa kamba zenu, mlisharuhusiwa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Mbunge alitupa jina halisi la mwenezi kuwa ni Albert Bashite na kwamba alipata 0 kwenye mtihani wa form four.
Bashite nae katuambia huyu Gwaji boy ni Zungu la unga.
Sasa leo wamekutana Bashite wa sifuri na muuza unga mwizi wa kura.
Propaganda za kipuuzi kama hizi ziliishapitwa na wakati
Sasa hivi ni mda wa siasa za kisayansi.
Maandamano ya amani ni haki ya kikatiba na msingi wa haki za binadamu.
Kutuambia tupuuze maandamano ni sawa na kutuambia tukubali matatizo ya ughali wa maisha ya raia unaosababishwa na anasa za waandamizi wa serikali.
Pia ni kutuambia tusishughulikie matatizo ya uchaguzi yaliyofanya nchi iwe na uchafuzi wa uchaguzi unaodaiwa kuwa uchaguzi.

Kama serikali haitaki na imepuuza maoni ya wadau katika suala zima la tume huru kama ilivyopuuza uandikishwaji wa katiba mpya hakuna namna ila kudai hii haki kwa maandamano ya amani.
 
Tumeanza kuambiwa tutapeleka makatapila. Tunazindua na kukabidhi makatapila...hizi siasa bado zinafaa kwa wananchi?

Kwanini ikifika uchaguzi tunatumia mazingaombwe majukwaani? Tutafanikiwa?
 
Back
Top Bottom