Makato ya HESLB: Rais Samia tunaomba mrudishe makato ya 8%, pia yazingatie sheria ya kubaki na 1/3 ya basic salary

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,018
144,377
Raisi Samia, japo umetukwaza sana na hii issue ya bandari, kuna mambo mazuri umefanya hasa katika kurekebisha baadhi ya mambo yaliyofanyika wakati wa utawala Marehemu Magufuli. Moja ya eneo ulilogusa ni kuboresha masilahi ya wafanyakazi kama kupandisha watumishi vyeo, kuongeza mishahara ingawa ni kwa kiwango kidogo na sasa ahadi ya kurudisha annual increments kwenye mishahara ya wafanyakazi kila mwaka.

Hata hiyo, kuna jambo moja muhimu na linagusa sana wafanyakazi(linaumiza) na hili si lingine bali ni uamuzi wa serikali ya awamu iliyopita kuongeza makato ya kulipia deni la Bodi ya Mikopo(HESLB), kutoka asilimia 8 mpaka asilimia 15 bila kujali mkataba wanufaika walioingia wakati wa kuomba mkopo(kukatwa asilimia 8), na pia makato haya kutozingatia sheria inayotaka Mfanyakazi abaki walau na moja ya tatu(theluthi moja) ya mshara ghafi wake(basic salary) baada ya makato yote ya lazima na mengineo kama mikopo ya mabenki n.k.

Kwa bahati mbaya, hata kama mtumishi ameshafikia ukomo wa hiyo moja ya tatu kwenye take home yake, makato ya HELSB hayazingatii hii sheria bali wanakata tu na matokeo yake mtumishi anabaki na take home iliyo chini ya moja ya tatu ya basic salary yake huku mishahara yenyewe ikiwa ni duni kabisa kwa wafanyakazi wengi wa nchi hii hasa wa serikali na pia hata wale wa sekta binafsi.

Kumbekuni hata CAG aliepita, aliwahi pinga haya makato na akatamka kabisa kuwa yanavunja sheria.


Binafsi sio muumini sana wa hii sheria ya kulazimisha mtumishi abaki na moja ya tatu kwasababu ina mapungufu mengi(niliwahi andika kuhusu haya mapungufu siku za nyuma) na pia sheria hii haikufanyiwa utafiti wa kutosha, ila kwakuwa serikali yenyewe sasa ndio kinara wa kuivunja, basi hii inangeza sababu ya kuona ni bora tu sheria hii ifufutwe kabisa au ifanyiwe marekebisho.


Mtumishi akitaka kukopa, anabanwa na hii sheria, ila ukidaiwa na Bodi ya Mikopo, sheria haizingatiwi wanakata tu. Hii sio sawa kabisa na ni bora hii sheria ifutwe ijulikane moja.

Kuongoza ni kuonyesha njia.

Talk the talk and walk the walk.
 
Raisi Samia, japo umetukwaza sana na hii issue ya bandari, kuna mambo mazuri umefanya hasa katika kurekebisha baadhi ya mambo yaliyofanyika wakati wa utawala Marehe Magufuli. Moja ya eneo ulilogusa ni kuboresha masilahi ya wafanyakazi kama kupandisha watumishi vyeo, kuongeza mishahara ingawa ni kwa kiwango kidogo na sasa ahadi ya kurudisha annual increaments kwenye mishahara ya wafanyakazi kila mwaka.

Hata hiyo, kuna jambo moja muhimu na linagusa sana wafanyakazi(linaumiza) na hili ni kitendo cha serikali ya awamu iliyopita kuongeza makato ya kulipia deni la Bodi ya Mikopo(HESLB) kutoka asilimia 8 mpaka asilimia 15 bila kujali mkataba wanuafaika walioingia wakati wa kuomba mkopo(kukatwa asilimia 8) na pia makato haya kutozingatia sheria inayotaka Mfanyakazi abaki walau na moja ya tatu ya mshara ghafi wake(basic salary) baada ya makato yote ya lazima na mengineo kama mikopo ya mabenki n.k.

Kwa bahati mbaya, hata kama mtumishi ameshafikia ukomo wa hiyo moja ya tatu kwenye take home yake, makato ya HELSB hayajali hii sheria bali wanakata tu na matokeo yake mtumishi anabaki na take home iliyo chini ya moja ya tatu ya basic salary yake huku mishahara yenyewe ikiwa ni duni kabisa kwa wafanyakazi wengi wa nchi hii hasa wa serikali na pia hata wale wa sekta binafsi.

Binfsi sio muumini sana wa hii sheria ya kulazimisha mtumishi abaki na moja ya tatu kwasababu ina mapungufu mengi na haikufanyiwa utafiti wa kutosha ila kwakuwa serikali yenyewe ndio kinara wa kuivunja, basi ni bora tu sheria hii ifafutwa kabisa au ifanyiwe marekebisho.

Mtumishi akitaka kukopa, anabanwa na hii sheria ila ukidaiwa na Bodi ya Mikopo sheria haizingatiwi. Hii sio sawa kabisa futeni hii sheria ijulikane moja.
Mama ajatukwanza popote kwenye issue ya bandari iko sahihi , mtakuja kumshukuru badaye kwa kubinaifusisha badari anapenda maendeleo ya Tanganyika, isipo kua wengi ni slow learners.
 
Moja kati ya bodi za kipuuzi kabisa kuwahi kuanzishwa nchini, basi ni hii bodi ya mikopo. Yaani unaweza ukawa siyo mnufaika wa mikopo yao, lakini katika hali ya kustaajabisha! Unashangaa tu wameanza kukukata. Ukienda kusitisha makato na kudai hela zako, unazungushwa!

Bado kuna watu wanufaika walimaliza madeni yao, lakini miezi kadhaa iliyopita wamebambikiwa madeni na kuanza kukatwa tena kibabe kwenye mishahara yao; huku makato yakilenga 15% ya basic salary ya mfanyakazi! Badala ya take home yake! Imagine mtu una vimeo vyako vya Bayport, Platinum, nk! Halafu na hawa wahuni wanachukia yena 15% ya basic salary, na wakati ulishamalizana nao miaka zaidi ya 5 iliyopita! Kama siyo uhuni ni nini!

Sijajua ni kwa nini DP World wanapewa bandari, badala ya kupewa takataka kama hizi. Binafsi Waarabu wangebinafsishiwa takataka kama hii inayoitwa Bodi ya mikopo, aisee ningewapigia debe wapewe hata bure tu. Maana ina watendaji wa hovyo mpaka basi.
 
Moja kati ya bodi za kipuuzi kabisa kuwahi kuanzishwa nchini, basi ni hii bodi ya mikopo. Yaani unaweza ukawa siyo mnufaika wa mikopo yao, lakini katika hali ya kustaajabisha! Unashangaa tu wameanza kukukata. Ukienda kusitisha makato na kudai hela zako, unazungushwa!

Bado kuna watu wanufaika walimaliza madeni yao, lakini miezi kadhaa iliyopita wamebambikiwa madeni na kuanza kukatwa tena kibabe kwenye mishahara yao; huku makato yakilenga 15% ya basic salary ya mfanyakazi! Badala ya take home yake! Imagine mtu una vimeo vyako vya Bayport, Platinum, nk! Halafu na hawa wahuni wanachukia yena 15% ya basic salary, na wakati ulishamalizana nao miaka zaidi ya 5 iliyopita! Kama siyo uhuni ni nini!

Sijajua ni kwa nini DP World wanapewa bandari, badala ya kupewa takataka kama hizi. Binafsi Waarabu wangebinafsishiwa takataka kama hii inayoitwa Bodi ya mikopo, aisee ningewapigia debe wapewe hata bure tu. Maana ina watendaji wa hovyo mpaka basi.
Hiyo aya ya mwisho imenifanya nicheke peke yangu!!!

Mzazi mwenye uwezo ni bora mwanao umsomeshe kuliko kuchukua mkopo HESLB maana baadae ni majuto makubwa kwa makato yanayofanyika. Magufuli hii ni moja ya legacy yake.
 
Kwani Lucas Mwashambwa anasemaje!!!
Kati ya watu ambao wanaweza kukusababishia kushinda na njaa kutokana na hasira kali iliyokaba kooni, basi ni huyo jamaa!

Utamsikia "Hongera Mheshimiwa Rais Samia kwa kukata kiu ya Watanzania na pia kuigusa mioyo yao kwa kuwaongezea tozo na kodi kwenye mafuta ya taa/dizeli na petroli, na pia kwa kuongeza 1000 kwenye bei ya kila mfuko mmoja wa cement! Sasa unajiuliza huyu jamaa yuko timamu kweli!! 🤔
 
Kwa bahati mbaya, hata kama mtumishi ameshafikia ukomo wa hiyo moja ya tatu kwenye take home yake, makato ya HELSB hayazingatii hii sheria bali wanakata tu
Vipi kama ikiwa 8% halafu mtumishi amekopa taasisi nyingine za fedha na kufikia ukomo wa hiyo moja ya tatu?

Nadhanimuhimu ni watumishi kuwa na nidhamu ktk matumizi ya fedha. Acheni kujitutumua kwa kukopa na vitu vya hovyo (liabilities) kama magari na kupelekea kuishi kwa shida.

Magari tuachieni sisi wajasiriamali
 
Bandari irudi kwanza, mengine baadaye
Kwani u.eambiwa bandari imehama? Kama upo Namanyere huko panda basi kesho asubuhi, utafika Dar usiku halafu kesho kutwa ukaangalie bandari. Ipo pale pale. Usiamini fya kuambiwa.
 
Moja kati ya bodi za kipuuzi kabisa kuwahi kuanzishwa nchini, basi ni hii bodi ya mikopo. Yaani unaweza ukawa siyo mnufaika wa mikopo yao, lakini katika hali ya kustaajabisha! Unashangaa tu wameanza kukukata. Ukienda kusitisha makato na kudai hela zako, unazungushwa!

Bado kuna watu wanufaika walimaliza madeni yao, lakini miezi kadhaa iliyopita wamebambikiwa madeni na kuanza kukatwa tena kibabe kwenye mishahara yao; huku makato yakilenga 15% ya basic salary ya mfanyakazi! Badala ya take home yake! Imagine mtu una vimeo vyako vya Bayport, Platinum, nk! Halafu na hawa wahuni wanachukia yena 15% ya basic salary, na wakati ulishamalizana nao miaka zaidi ya 5 iliyopita! Kama siyo uhuni ni nini!

Sijajua ni kwa nini DP World wanapewa bandari, badala ya kupewa takataka kama hizi. Binafsi Waarabu wangebinafsishiwa takataka kama hii inayoitwa Bodi ya mikopo, aisee ningewapigia debe wapewe hata bure tu. Maana ina watendaji wa hovyo mpaka basi.
Bodi hawakati hela ya mtu, hela anakata mwajiri wako halafu ndio anaipeleka HESLB, wewe banana na mwajiri wako akupe hela yako ambayo amekukata bila utaratibu
 
Bodi ya kidwanzi sana hiyo. Na hapo wamekufyeka huku mshahara nao ukiwa na vimeo kibao!!

Yaani kwa wazazi wenye uwezo wa kuwasomesha watoto wao, ni bora wakawalipia tu ada ya chuo kikuu ili kuepukana na hawa wahuni.
Kweli kama una uwezo, bora tu mwanao umlipie kuliko kuchukua mkopo HELSB kwani baadae ni kilio kwa walio wengi.
 
Hongera na kongole kwa vijana wa BAVICHA maana bila kuwa na vijana walio na chachu ya mabadiliko kama waliopo CHADEMA nchi haiwezi kusonga mbele. Tunaona wenzetu kule UVCCM wao hawaongozi chochote zaidi ya kusifu na kuabudu huku kusubiri waletewe boom vyuo vya elimu ya juu ..

UMUHIMU WA JUKWAA HURU LA VIJANA

VIJANA WA TANZANIA KUANZISHA JUKWAA LAO HURU, NDIYO JIBU LA KUPATA NAFASI YA KUSHIRIKISHWA KTK NGAZI YA MAAMUZI KITAIFA

Duniani ni vijana wa vyuo vikuu ndiyo wanaoongoza kuchagiza mageuzi

Historia inaonesha mara baada ya uhuru wa kwanza kupatikana ktk mataifa mbalimbalii iwe kwa mtutu wa bunduki au maandamano ya kuondoa wakoloni, baadaye kulifuatia msuguano wa wananchi wenyewe kwa wenyewe kwa kutoridhishwa na wale waliochukua utawala toka kwa wakoloni.

Sababu mbalimbali zilizua msuguano ktk nchi huru kama udiktekta, tawala kamdamizi ya chama kimoja, utawala mbovu, ubaguzi wa kielimu mfano mtoto aliyesoma shule za kata / st. Kayumba anadanganywa kuwa akihitimu chuo kikuu atakuwa na nafasi sawa na mwenzake aliyesoma St. Mary's akamaliza elimu ya chuo kikuu pia anayekimanya kiingereza / kispaniola vizuri zaidi na wajomba wake wapo ktk nafasi za kiutawala n.k

Vijana wengi pamoja na umasikini wa familia zao wanashawishiwa kwenda vyuo vikuu kwa kuchukua mikopo wakiwa na matumaini ambayo ni hadaa kuwa kwa kumaliza elimu ya juu watakuwa sawa na wale watoto wa tabaka la watawala anasema kiogozi wa vuguvugu la wanafunzi wa chuo kikuu wa Chile kamanda Gabriel Boric mwaka 2017.

Hapo ndipo Wanafunzi waliopo ktk nchi kama Sudan, Chile, Cuba, Afrika ya Kusini, Kenya walishiriki kudai mageuzi ili kuondokana na tawala zilizomngoa mkoloni mweupe.

Tanzania vijana hawajishughulishi kuhoji mambo yasiyowaridhisha wananchi kama matumizi mabaya ya kodi za wananchi, tozo zilizokifu uvumilivu wa wananchi, demokrasia kubinywa, katiba kandamizi, mikopo ya elimu ya vyuo vya elimu ya juu n.k

Chile nchi iliyo na kiongozi kijana Gabriel Boric ambaye ndiye rais kijana kabisa wa kuchaguliwa amezaliwa 11 February 1986 ambaye alichukua madaraka ya urais tarehe 11 March 2022 baada ya kushinda uchaguzi mkuu nchini Chile tarehe 19 December 2021 kwa kupata asilimia 60% ktk uchaguzi wa urais.

Gabriel Boric on the Chilean student movement 14 June 2017

Gabriel Boric on the Chilean Student Movement

Likes
59,554
Views
2017
14 Jun
In a presentation at the School of Public Policy on June 7, 2017; Gabriel Boric offers a historical perspective and reflects on lessons learned. He focuses especially on the role of social movements in a well-developed democracy and provides insights on how to sustain collective action over an extended period of time. He speaks also about his transition from being a member of a political movement to being a member of Parliament. Gabriel Boric is a Chilean parliamentarian, and a former leader of the national student movement. He was the president of the Student Federation of the Universidad de Chile, one of the most important student unions in the country. Boric currently represents the Magallanes and Antarctic Region in Chile’s Chamber of Deputies. He was elected as an independent candidate and is not associated with either one of the two political coalitions that have traditionally dominated politics in Chile. Source:

Department of Public Policy at CEU​

Mwanafunzi wa chuo kikuu toka familia masikini anazama ktk mkondo wa madeni ya fedha za mkopo wa elimu ya juu huku akiwa na matumaini potofu ya kupata ajira au kuwepo mazingira hewa ya kujiajiri.


Vijana vyuo vikuu na mijini pia vijijini badala ya kumezwa na ukiritimba wa UVCCM na ahadi kuwa ni viongozi wa kesho huku watoto wa vigogo wa CCM wanapewa nafasi sasa na siyo kesho wanatakiwa kuunda chombo chao kipya cha kutambulika kama mdau muhimu anayehitaji kuonekana katika majukwaa ya siasa pia ktk vituo vya redio, televisheni na mitandao ya kijamii kuchagiza mabadiliko na mageuzi ikiwemo pia kupewa nafasi nje ya mfumo wa vyama ili wagombee nafasi za kuchaguliwa na wananchi.


Gabriel Boric - The 100 Most Influential People of 2022 - TIME

time.com › collection › gabriel-boric

gabriel boric presidente from time.com
23 May 2022 · He is making Chile the social, economic, and political laboratory of the world once again. Stiglitz is a Nobel Prize–winning economist
 
Back
Top Bottom