Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,017
- 144,373
Awamu ya tano chini ya Rais wa wakati huo, Marehemu Magufulli, ilikuwa kinara wa kukiuka sheria na kuvunja mikataba na matokeo yake leo hii serikali inashitakiwa huko katika mahakama za kimataifa na nchi kushindwa kesi na kulazimika kulipa mabilioni ya shilingi kama fidia.
Walichokifanya katika kuvunja mikataba ya kimataifa, ndicho walichokifanya katika kubadili sheria/taratibu inayotumika kuamua kiwango cha kukata mshahara kwa ajili ya kulipia deni la Bodi ya Mikopo.
Kwa wasiolewa, miaka ya 2016 kurudi nyuma, mkataba kati ya Bodi ya Mikopo na Wanafunzi ambao ni Wanufaika wa mikopo hii, ulielekeza Mnufaika kukatwa asilimia 8 ya mshashara wake ghafi(basic salary) ili kulipia mkopo wake kila mwezi na siku zote mambo yalienda hivyo kama mkataba unavyosema.
Serikali ya awamu ya tano chini ya Magafuli, wakabadilli sheria/taratibu na kuongeza kiwango cha makato kutoka asilimia 8 mpaka asilimia 15 ya sasa na makato yamekuwa yakifanyika bila kujali mkataba baina ya mkopeshaji na mkopeshwaji.
Hivyo, jambo hili lingekuwa ni jambo la kimataifa, serikali ingeshitakiwa na wangeshindwa kesi na wangelazimika kuwalipa fidia wanufasika wote wa Bodi wanaokatwa/waliokatwa viwango tofauti na jinsi mkataba unavyoeleza unless mkataba ulikuwa unaruhusu mkopeshaji kubadili asilimia ya makato wakati wowote bila ridhaa ya mkopeshewaji jambo ambalo sidhani kama lipo kwenye mkataba.
Humu ndani hata mkiishitaki serikali na ikashindwa kesi, bado wanaweza tu wasitekeleza hukumu ya mahakama na watu mkaishia kulalamika tu.
Hii ni sababu nyingine kwanini watanzania tunahitaji katiba mpya.
Walichokifanya katika kuvunja mikataba ya kimataifa, ndicho walichokifanya katika kubadili sheria/taratibu inayotumika kuamua kiwango cha kukata mshahara kwa ajili ya kulipia deni la Bodi ya Mikopo.
Kwa wasiolewa, miaka ya 2016 kurudi nyuma, mkataba kati ya Bodi ya Mikopo na Wanafunzi ambao ni Wanufaika wa mikopo hii, ulielekeza Mnufaika kukatwa asilimia 8 ya mshashara wake ghafi(basic salary) ili kulipia mkopo wake kila mwezi na siku zote mambo yalienda hivyo kama mkataba unavyosema.
Serikali ya awamu ya tano chini ya Magafuli, wakabadilli sheria/taratibu na kuongeza kiwango cha makato kutoka asilimia 8 mpaka asilimia 15 ya sasa na makato yamekuwa yakifanyika bila kujali mkataba baina ya mkopeshaji na mkopeshwaji.
Hivyo, jambo hili lingekuwa ni jambo la kimataifa, serikali ingeshitakiwa na wangeshindwa kesi na wangelazimika kuwalipa fidia wanufasika wote wa Bodi wanaokatwa/waliokatwa viwango tofauti na jinsi mkataba unavyoeleza unless mkataba ulikuwa unaruhusu mkopeshaji kubadili asilimia ya makato wakati wowote bila ridhaa ya mkopeshewaji jambo ambalo sidhani kama lipo kwenye mkataba.
Humu ndani hata mkiishitaki serikali na ikashindwa kesi, bado wanaweza tu wasitekeleza hukumu ya mahakama na watu mkaishia kulalamika tu.
Hii ni sababu nyingine kwanini watanzania tunahitaji katiba mpya.