Makato kwa utaratibu wa asilimia kwenye mishahara ya watumishi, ni utaratibu usiofaa; Kuwe na utaratibu wa kuomba kibali cha kuongeza makato hayo

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Katika mishahara ya watumishi wa umma, kuna makato ya lazima ambayo ni PAYE, Bima ya Afya, Makato ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii na makato mengine ya kujiunga kwa hiari kama ya vyama vya wafanyakazi, nk.

Nachojiuliza, ni sahihi mshahara unapopanda na makato haya kupanda automatically?

kwa maneno mengine, mshahara wa mtumishi unapopanda kwa mtumishin kupandishewa cheo au serikali inapoongeza mshahara, gharama za kuendesha mfuko wa Bima ya Afya au taasisii kama vya wafanyakazi nazo zinaongezeka?

Binafsi nafikiri wakati umefika utaratibu huu wa kukata mishahara kwa asilimia ya mshahara ghafi(basic salary), utazamwe upya na kuwe na restrictions fulani na sio makato kuongezeka automatically kila mshara wa mtumishi unapopanda kwani kwa kufanya hivi, kuna muathiri mtumishi kama ambavyo anaathirika na kupanda kwa bei ya unga, mkate, mafuta, nk.

Makato pekee ambayo naona yanafaa kupanda automatically kila mshahara unapoongezeka, ni labda PAYE tu ili kuiongezea serikali uwezo wa kulipa hiyo mishahara ingawa PAYE nayo teyari iko juu mno katika nchi yetu.

Hakuna uhusiano wowote wa kuongezeka kwa mshara kwa mfanyakazi na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji wa Vyama vya Wafanyakazi, Mifuko ya Hifadhi ya jamii, Bima ya Afya n.k, na tukumbuke mifuko ya hifadhi ya Jamii imekuwa ikijidendesha kibiashara kwa kufanya uwekezaji ingawa kuna kasoro zimejitokeza na kuathiri mifuko hii na kusababisha iunganishwe lakini ilikuwa inatengeneza fedha na hivyo kuondoa ulazima wa kuongeza makato yanayokwenda katika mifuko hii kila mara mishahara inapoongezwa.

Mifuko na taasi hizi zinapohitaji kuongezewa makusanyo kutoka kwenye makato ya wafanyakazi, ziwe zinapeleka maombi serikalini kama ambavyo TANESCO wanatakiwa kupeleka maombi ya kupandisha bei ya umeme EWURA kabla ya kupandisha bei hizo na si kwa kutumia huu utaratibu unaotumika hivi sasa.

Uholela au kukosekana kwa udhibiti katika makato ya wafanyakazi, kuna changia sana kufanya mishahara duni ya watumishi wa umma kuwa duni zaidi na pia ni matokeo ya watu kuongezewa shilingi 3000/= na wengine shilingi 12,000/= katika take home yao kama ilivyotokea mwezi July mwaka huu.
 
Umeongea kweli tupu hivi vyama vya wafanyakazi ndio mchwa wa mishahara ya wafanyakazi kila mwezi wanakata ada ya uanachama wakati hakuna tija yoyote anayoipata huyo mfanyakazi mfano Mh Magu alitolea mfano cwt wanapata bilioni 4 hadi 5 kwa mwezi hayo mabilioni wanafanyia nini kwa mfano?
 
Umeongea kweli tupu hivi vyama vya wafanyakazi ndio mchwa wa mishahara ya wafanyakazi kila mwezi wanakata ada ya uanachama wakati hakuna tija yoyote anayoipata huyo mfanyakazi mfano Mh Magu alitolea mfano cwt wanapata bilioni 4 hadi 5 kwa mwezi hayo mabilioni wanafanyia nini kwa mfano?
Unaweza hata kujuta kuzaliwa katika hii nchi.
 
Hili ni wazo la Msingi sana
Inatakiwa walau makato kwa watumishi yaangaliwe
Badala kukata kwa asilimia yaanze kukata kwa amount fulani
 
Hili ni wazo la Msingi sana
Inatakiwa walau makato kwa watumishi yaangaliwe
Badala kukata kwa asilimia yaanze kukata kwa amount fulani
Labda serikali iamue tu ila wakisema wapate maoni kutoka kwa wanufaika mfano cwt Talgu na wenzao hawawezi kukubali kabisa kwani ukwasi waupatao na mishahara wanayolipana ni kufuru wanakusanya mabilioni kama ada ya uanachama kutoka kwenye mishahara kiduchu ya wanachama wao.Hivi vyama visiwepo tu mfyuuuuuuuu
 
Nakusahihisha hapo, makato ya vyama vya wafanyakazi siyo makato ya hiari
 
Pay as you earn
Lipa Kwa unachokipata
Kikiongezeka utalipa kadiri ya ongezeko
 
Umeongea kweli tupu hivi vyama vya wafanyakazi ndio mchwa wa mishahara ya wafanyakazi kila mwezi wanakata ada ya uanachama wakati hakuna tija yoyote anayoipata huyo mfanyakazi mfano Mh Magu alitolea mfano cwt wanapata bilioni 4 hadi 5 kwa mwezi hayo mabilioni wanafanyia nini kwa mfano?
Na bahati mbaya watumishi wa umma hawajitambui na ni waoga.
 
Ni makato ya hiari na si ya lazima kisheria isipokuwa watumishi hulazimishwa kujiunga na wengine hushawishiwa.
Ujiunge usijiunge utakatwa tu. Wanaita Ada ya uwakala. Ni kiwango kile kile sawa na wanachama wao.

Sheria iko hivyo
 
Ujiunge usijiunge utakatwa tu. Wanaita Ada ya uwakala. Ni kiwango kile kile sawa na wanachama wao.

Sheria iko hivyo
Kubali kusahihishwa Mkuu, Makato ya CWT, TUGHE, TALGWU, TUICO nk ni hiari unaweza ukakatwa au ukakataa kukatwa na Endapo unakatwa makato hayo na hujawahi kujaza fomu ya Uanachama kukiri kukwata haya Makato, kesho nenda kwa mwajiri wako Uandike barua ya Ombi la kurejeshewa pesa yako na utaipata na msamaha juu.
Makato ya Lazima ni PAYE, NHIF, HESLB, PSSSF/NHIF baaaaasi. Mengine yooote kukatwa hadi ukubali na utie saini ya kuidhinisha mwajiri akate.
 
Ni makato ya hiari na si ya lazima kisheria isipokuwa watumishi hulazimishwa kujiunga na wengine hushawishiwa.
Ni makato ya hiari ya lazima. Yaani ukikataa kuwa mwanachama wao wanakata kitu wanaita agency fee. Ni aslimia hiyohiyo.
Hiyo ni kulazimishana haijakaa sawa.

Serikali iangalie upya. Mtu akikataa kuwa mwanachama basi asikatwe hela yake
 
Ni makato ya hiari ya lazima. Yaani ukikataa kuwa mwanachama wao wanakata kitu wanaita agency fee. Ni aslimia hiyohiyo.
Hiyo ni kulazimishana haijakaa sawa.

Serikali iangalie upya. Mtu akikataa kuwa mwanachama basi asikatwe hela yake
Sisi watanzania ni watu wa kuonewa na kuburuzwa kwasababu hatujui na hatuna ujasiri wa kupinga uonevu wa wakubwa iwe ni katika sehemu za kaz au katika uongozi wa nchi.
 
Back
Top Bottom