
MITHALI 18
10.Jina la BWANA ni NGOME IMARA mwenye haki huikimbilia akawa SALAMA.

Neno

likawe faraja yako siku ya jumatatu ya leo na wiki nzima BWANA MUNGU awe ngome yako IMARA katika jina la YESU LIPITALO MAJINA YOTE AMEN
TUOMBE
Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu wetu kwa ulinzi wake usiku kucha,umetukinga na mengi Baba asante,tunaomba ulinzi wako katika familia zetu na baraka zako katika kazi za mikono yetu,Tunawaombea uponyaji wagonjwa hasa ndugu yetu SHIMBA YA BUYENZE anayesumbuka na jino,wafiwa,yatima na wajane wasipungukiwe,wasafiri nchi kavu,majini,angani akiwemo SHIMBA WA BUYENZE wafike salama damu ya Yesu iwafunike,Tunawaombea watumishi wa Mungu watumike sawasawa na mapenzi yako,kutana na hitaji la kila mmoja wetu Baba maana ulisema Ombeni nanyi mtapewa Mathayo 7:7,Bariki Makapuku wote na tuwe mfano mzuri kwa wengine na watu wazidi kukujua wewe Mfalme wa Amani.Tubariki tuingiapo na tutokapo
Tunaomba yote katika jina la Yesu .
Amen
MBARIKIWE SIKU NJEMA