Makapuku Forum

Makapuku Forum

ZABURI 121

1.Nitayainua macho yangu niitazame milima,Msaada wangu utatoka wapi?

2.Msaada wangu u katika BWANA,Aliyezifanya mbingu na nchi.

3.Asiuache mguu wako usogezwe,Asisisinzie akulindaye.

4.Naam,hatasinzia wala hatalala usingizi.Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5.BWANA ndiye mlinzi wako;BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

6.Jua halitakupiga mchana,Wala mwezi wakati wa usiku.

7.BWANA atakulinda na mabaya yote ,Atakulinda nafsi yako.

8.BWANA atakulinda utokapo na uingiapo,Tangu sasa na hata milele.


TUOMBE

Mwenyezi Mungu
Asante kwa ajili ya leo
Tunaomba uzidi kuwa nasi
Tutakase makosa yetu
Kutana na haja za mioyo yetu
Tukumbatie kama kuku akumbatiavyo vifaranga
Malaika walinzi waweke vituo katika nyumba na vitanda vyetu ,watuzunguke
Wakeshe pamoja nasi
Naenda kinyume na nguvu zote za giza
Damu ya Yesu itufunike
Asante maana utatenda zaidi ya tunavyoomba
Katika jina la Yesu Kristo
Tunaomba na kuamini
Amen

USIKU MWEMA WAPENDWA
Amen mama mchungaji

Nawe pia usiku mwema
 
karibu sana mkuu

pia hii ni barua yangu

YAH: KUACHA KAZI
Kchwa cha habari taja hapo juu nimeamua kwa akili yangu mwenyewe kuacha kazi kwasababu zifwatazo
umli
-kama unavyojua boss umli wangu umekwenda kwakweli miezi 2 mizima nakulindia mke kwakweli boss nimechoka

mke
-na ndio kilichofanya nikuandikie barua hii boss nimeamua kuoa boss nimeona umli unaenda ukizingatia sina hata mtoto mmoja boss ......the end

wako mtiifu katika kazi
kwa kuwa umeamua mwenyewe kwa akili zako bila kushurutishwa na shimba wa buyenzee nooo na mtu yeyote ..hutopata kiinua mgongo wala penshenii
 
kwa kuwa umeamua mwenyewe kwa akili zako bila kushurutishwa na shimba wa buyenzee nooo na mtu yeyote ..hutopata kiinua mgongo wala penshenii
Wakati mwingine nanyi matajiri mnapotaka kuajiri hata kama ni walinzi mfanye background check jamani. Hii itawaepusha na vioja kama hivi. Seriously, mlinzi wako huyo alikuwa kioja aisee. Na huyu ndiye ulimkabidhi uhai wa mkeo, na wanao? Una bahati sana!
 
Wakati mwingine nanyi matajiri mnapotaka kuajiri hata kama ni walinzi mfanye background check jamani. Hii itawaepusha na vioja kama hivi. Seriously, mlinzi wako huyo alikuwa kioja aisee. Na huyu ndiye ulimkabidhi uhai wa mkeo, na wanao? Una bahati sana!
ahahahaaaaa sema alikubana kila angle...

goodmorning lakini
 
Kunakucha. Tumshukuru Muumba wetu. Siku ya leo basi Muumba na Akatuwezeshe kutenda yaliyo mema machoni pake. Na zaidi ya yote tukaweze kuwasaidia wenzetu wenye shida ili kupitia kwetu wakaweze kuuonja upendo wa Muumba wao. Love you guys. I will be off the internet for at least 8 hrs.Tutaonana jioni Mungu Akipenda. Muwe na siku njema!
0609a5788e97caf1d7046752ad5d3248.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom