Makapuku Forum

Makapuku Forum

Come on Mukongoman! Una batophobia? Ndege huwa unapanda na huogopi? Ulianza anzaje kuogopa haya majengo marefu?

Ila hizi phobia zingine hizi hata sijui zinaanzaje. Mimi siku hizi nikiona mende chumbani silali aisee mpaka nimtafute nimuue. Nikilala bila kumuua basi nitaota limende likuuuubwa linaninyemelea sasa hata kulikimbia siwezi. Hapo mwanaume ni kutoka jasho balaa. Ajabu wadudu wengine na hata nyoka sina tatizo nao kabisa. Huwa nashangaa sana kwa sababu nimekulia kijijini na mende kibao and it was no big deal.
Ndege na Boti nimepanda no problem.....ila majengo marefu nitaota sakafu/floor imejengwa kwa mbao nyembamba au zilizooza then zinaanza kuvunjika usiombe kukutwa na bwana pepsi
 
KUMTEGEMEA MUNGU KUNA FAIDA

ISAYA 40

29 Huwapa nguvu wazimiao ,humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo

Pale unapochoka fikra unapowaza sana unapokata tamaa ndipo Mungu anapokupa nguvu na kinga za kila shambulizi pia kukuvusha juu ya hali uliyo nayo ,hivyo pambana na hali hiyo kwani Bwana anatamalaki na kukupa utulivu na ushindi ili kumshinda adui anapotaka kukudhuru

Tumuombe Mungu atusaidie tumkabidhi Mungu njia zetu zote naye hatatuacha

TUOMBE

MUNGU BABA MWENYEZI tunakushukuru sana kwa ulinzi wako na yote unayotutendea,Mungu,umetutoa mbali tunakushukuru sana.

Ponya wagonjwa,fariji wafiwa,fariji wajane na yatima,tembea nasi Baba nyoosha mapito yetu,peke yetu hatuwezi

Tunajikabidhi miili na roho zetu tukinge na hatari zote za mwili na roho.

Roho Mtakatifu Mfariji wetu tufundishe ,tuongoze,tuonyeshe njia sahihi ya kuishi maisha ya kumpendeza Mungu

Asante kwa kila linakotokea maishani mwetu

Tunaomba yote kwa jina la Yesu mpatanishi na mwokozi wetu .

Amen


Muwe na siku njema,wiki njema,mwezi mwema.....MBARIKIWE
Amen Mama Mchungaji
 
Anz kukemea kwanzq utajua ni nini,pia inategemea nq imani yako penda kumwaga maji ya baraka ndani ya nyumba nq mazingira au nunua mafuta ya mzeituni ,chumvi changanya kwenye maji, yaombee yawe damu ya Yesu,kwa imani mambo mengi yatabadilikq


Kuna mapaka yakikua kila siku yanalala dirishani kwangu na kulia vibayaaaa,nikaombea maji nikaweka chumvi nikaweka imani ,hakika baada ya wiki nilsikia harufu za ajabu,yalikufa
Aisee. Nitafanya hivyo. Hali hii imenifanya niwe msafi sana ili mende wasiweke makazi. Watu wananisifia kwa usafi uliopindukia kimo kumbe hawajui sababu yake. Uzuri hali hii haijitokezi mara kwa mara. Naweza kumaliza miezi sita hata mwaka halafu siku moja nikiona mende tu nightmare zinakuja.

Asante sana mtumishi. Halafu eti wanasema huku Makapuku hakuna lolote la maana!
 
Aisee. Nitafanya hivyo. Hali hii imenifanya niwe msafi sana ili mende wasiweke makazi. Watu wananisifia kwa usafi uliopindukia kimo kumbe hawajui sababu yake. Uzuri hali hii haijitokezi mara kwa mara. Naweza kumaliza miezi sita hata mwaka halafu siku moja nikiona mende tu nightmare zinakuja.

Asante sana mtumishi. Halafu eti wanasema huku Makapuku hakuna lolote la maana!
Asante kushukuru,amini utashinda,USIOGOPE,HUKU MAKAPUKU BWANA MIMI NAJIFUNZA MENGI,NAJISIKIA VIZURI KUWA HAPA MUNGU AWABARIKI WALIOWAZA HILI
 
Nyagei, wewe huna phobia yo yote?
Ila kuna siku nilikuwa site huko wilayani Bahi mida ya usiku nilikuwa niko na mrembo wa kigogo jirani nasi kulikuwa na mti, so ili kuweza kumlaghai yule manzi nilipitisha mkono kwa mabega yake ili awe close nami suddenly nilihisi kuchomwa na kitu ila nilipotezea nikidhani ni sungusungu mdudu kumbe ni nge, nilishtuka maumivu yalipozidi na mkono kuanza kuishiwa nguvu, yule manzi nilimuacha na kurejea nilipofikia. Nilijichanja kidogo na kukamua sumu ila sikulala usiku ule na asubuhi ndio mkono hauna nguvu kabisa.

After 20hrs nikapona kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom