Makapuku Forum

Makapuku Forum

Huko ndio usiseme ile siku manusura nikimwage kwenye Azam.

Maboti ya kule kwetu sasa kwenda burundi ndio usiseme naregea kama mtoto hadi naumwa
Kuna dawa ukiwa safarini unaweza tumia ninao watu wa namna hii katika familia hadi niliwapeleka hospital tukaandikiwa dawa kwa hiyo kila tukianza safari majini,bus,ndege wanakunywa dawa na haitokei tena
 
Nisikudanganye Mtumishi. Mimi siyo mwanasheria na kusema kweli mbali na kujua haki zangu za msingi kama raia wa Jamhuri ya Tanzania sijui cho chote kuhusu sheria.

Umesema kuwa walifeli kidato cha nne wakafanya mbinu wakabadili matokeo yao kinyemela (wakagushi vyeti) na matokeo hayo feki ndiyo yakawafanya wapate nafasi ya kuendelea na masomo yao mpaka wakapata ajira; na leo kosa lao walilofanya zamani ndiyo limesababisha watumbuliwe. Sijui tafsiri ya kisheria lakini nadhani kubadili matokeo kinyemela ni kosa. Kama kuna kapuku mwanasheria anaweza kutufafanulia zaidi.

Nimesikia TLS chini ya Tundu Lissu imewashauri wafanyakazi wote wanaoamini kuwa wametumbuliwa kimakosa waungane wafungue class action suit dhidi ya serikali na TLS itawapa msaada wa kisheria bure. Wanaweza kupata ufafanuzi wa kosa lao kisheria (kama wametenda kosa) na watajua cha kufanya baada ya hapo. Washauri wawasiliane na TLS au mwanasheria ye yote angalau wajue kosa lao limekaaje kisheria...and then they can go from there.

Bashite yeye alipiga ziro form 4 akanunua cheti cha mtu mwingine. Hawa matokeo hayakutosha wakajazia jazia kinyemela kwa majina yao yale yale. Sijui yupi ana kosa kubwa zaidi ya mwingine. Uwe na amani mtumishi na wape pole sana. Waambie wasikate tamaa. Maisha ni lazima yaendelee ati! Mungu Atawafungulia milango mingine!
Amina sana sana nawaombea tu,maana shida ni namna ya kupokea hili lililotokea lakini wote wanaelewa kosa lao ,huwezi amini ilikua siri yao hakuna aliyejua,nilipowauliza wakasema walichofanya ngoja wafike nitajua la kufanya,nawashukuru sana kwa ushauri na kunitia moyo Mungu awabariki
 
Huyo nyoka alifikaje mgongoni? Hata mimi nikisali na kukemea tatizo linaisha ila ikitokea nikaona mende hasa usiku nightmare zinajirudia. Naota mamende makubwa kama bajaji yananinyemelea halafu sasa nakuwa kama nimeganda kukimbia siwezi na nakuwa niko nusu macho na naweza kusikia kinachoendelea mf. maongezi n.k. Sijui ni mapepo haya au nini hii mtumishi?
Anz kukemea kwanzq utajua ni nini,pia inategemea nq imani yako penda kumwaga maji ya baraka ndani ya nyumba nq mazingira au nunua mafuta ya mzeituni ,chumvi changanya kwenye maji, yaombee yawe damu ya Yesu,kwa imani mambo mengi yatabadilikq


Kuna mapaka yakikua kila siku yanalala dirishani kwangu na kulia vibayaaaa,nikaombea maji nikaweka chumvi nikaweka imani ,hakika baada ya wiki nilsikia harufu za ajabu,yalikufa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom