BlessedHope
JF-Expert Member
- Jan 29, 2016
- 7,988
- 32,649
JINSI GANI KIJANA AISAFISHE NJIA YAKE?
ZABURI 119
9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?kwa kutii akilifuata neno lako.
Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
10 Kwa moyo wangu wote nimekutafuta.Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
11 Moyoni mwako nimeliweka neno lako,Nisije nikakutenda dhambi.
12 Ee BWANA,umehimidiwa ,unifundishe njia zako,unifundishe amri zako.
Mungu wetu ni wa Upendo na hapendi tupotee,yupo tayari kutuongoza siku zote za maisha yetu na yupo tayari kusikiliza mahitaji yetu na mawazo yetu,hapendi tupotee wala kuishi maisha yasiyo na malengo na yasiyompendeza.
TUNAPASWA:
Kutii sauti yake.
Kufuata neno lake
Kumfuata kwa moyo wote
Kushika mafundisho ya amri zake
NAYE HATATUACHA TUPOTEE MBALI NA MAAGIZO YAKE
MIOYONI MWETU TULIWEKE NENO LA MUNGU TUSIJE TUKATENDA DHAMBI TUANGAMIE
Bwana Yesu wewe ni mkombozi wetu milele,Tunakushukuru wewe husinzii wala hulali na umetulinda mpaka asubuhi ya leo.
Fungua macho yetu tuweze kuona wema huu na upendo huu mkubwa na pia tufungue tuone baraka zote ulizotuandalia siku ya leo,kwa upendo wa marafiki wote mahali hapa watatufanya tujisikie vizuri.
Nakushukuru sana Mungu kwa nafasi hii ya kuhudumia marafiki na wapendwa wetu mahali hapa,nakuheshimu sana Mungu wangu.bila wewe hatuwezi chochote. ...nayaweza yote kupitia wewe Mungu unitiaye nguvu.
Tubariki siku ya leo safarini,ponya wagonjwa,fariji wafiwa na wenye dhiki,nyoosha mkono wako katika mapito yote na utuongoze kukupenda ,kukutii,kulifuata neno lako na kukutafuta kwa bidii.
Asante Baba maana utatenda sawa na mapenzi yako
Tunaomba na kushukuru katika jina la Yesu Amen
MBARIKIWE

ZABURI 1199 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?kwa kutii akilifuata neno lako.
Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
10 Kwa moyo wangu wote nimekutafuta.Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
11 Moyoni mwako nimeliweka neno lako,Nisije nikakutenda dhambi.
12 Ee BWANA,umehimidiwa ,unifundishe njia zako,unifundishe amri zako.
Mungu wetu ni wa Upendo na hapendi tupotee,yupo tayari kutuongoza siku zote za maisha yetu na yupo tayari kusikiliza mahitaji yetu na mawazo yetu,hapendi tupotee wala kuishi maisha yasiyo na malengo na yasiyompendeza.TUNAPASWA:
Kutii sauti yake.
Kufuata neno lake
Kumfuata kwa moyo wote
Kushika mafundisho ya amri zakeNAYE HATATUACHA TUPOTEE MBALI NA MAAGIZO YAKE
MIOYONI MWETU TULIWEKE NENO LA MUNGU TUSIJE TUKATENDA DHAMBI TUANGAMIE
Bwana Yesu wewe ni mkombozi wetu milele,Tunakushukuru wewe husinzii wala hulali na umetulinda mpaka asubuhi ya leo.
Fungua macho yetu tuweze kuona wema huu na upendo huu mkubwa na pia tufungue tuone baraka zote ulizotuandalia siku ya leo,kwa upendo wa marafiki wote mahali hapa watatufanya tujisikie vizuri.
Nakushukuru sana Mungu kwa nafasi hii ya kuhudumia marafiki na wapendwa wetu mahali hapa,nakuheshimu sana Mungu wangu.bila wewe hatuwezi chochote. ...nayaweza yote kupitia wewe Mungu unitiaye nguvu.
Tubariki siku ya leo safarini,ponya wagonjwa,fariji wafiwa na wenye dhiki,nyoosha mkono wako katika mapito yote na utuongoze kukupenda ,kukutii,kulifuata neno lako na kukutafuta kwa bidii.
Asante Baba maana utatenda sawa na mapenzi yako
Tunaomba na kushukuru katika jina la Yesu Amen
MBARIKIWE
