Makapuku Forum

Makapuku Forum

teh teh teh! Hiyo avatar itajamponza, nilitaka nimpe offer ya Muungano.
27a08956ee63d67fd26164f68e9e8370.jpg
 
JINSI GANI KIJANA AISAFISHE NJIA YAKE?
ZABURI 119

9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake?kwa kutii akilifuata neno lako.
Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.

10 Kwa moyo wangu wote nimekutafuta.Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.

11 Moyoni mwako nimeliweka neno lako,Nisije nikakutenda dhambi.

12 Ee BWANA,umehimidiwa ,unifundishe njia zako,unifundishe amri zako.

Mungu wetu ni wa Upendo na hapendi tupotee,yupo tayari kutuongoza siku zote za maisha yetu na yupo tayari kusikiliza mahitaji yetu na mawazo yetu,hapendi tupotee wala kuishi maisha yasiyo na malengo na yasiyompendeza.
TUNAPASWA:
Kutii sauti yake.
Kufuata neno lake
Kumfuata kwa moyo wote
Kushika mafundisho ya amri zake


NAYE HATATUACHA TUPOTEE MBALI NA MAAGIZO YAKE

MIOYONI MWETU TULIWEKE NENO LA MUNGU TUSIJE TUKATENDA DHAMBI TUANGAMIE


Bwana Yesu wewe ni mkombozi wetu milele,Tunakushukuru wewe husinzii wala hulali na umetulinda mpaka asubuhi ya leo.

Fungua macho yetu tuweze kuona wema huu na upendo huu mkubwa na pia tufungue tuone baraka zote ulizotuandalia siku ya leo,kwa upendo wa marafiki wote mahali hapa watatufanya tujisikie vizuri.
Nakushukuru sana Mungu kwa nafasi hii ya kuhudumia marafiki na wapendwa wetu mahali hapa,nakuheshimu sana Mungu wangu.bila wewe hatuwezi chochote. ...nayaweza yote kupitia wewe Mungu unitiaye nguvu.

Tubariki siku ya leo safarini,ponya wagonjwa,fariji wafiwa na wenye dhiki,nyoosha mkono wako katika mapito yote na utuongoze kukupenda ,kukutii,kulifuata neno lako na kukutafuta kwa bidii.

Asante Baba maana utatenda sawa na mapenzi yako

Tunaomba na kushukuru katika jina la Yesu Amen

MBARIKIWE
Amen

Na kwako pia mama mchungaji
Ubarikiwe Blessedhope
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom