Bitoz
JF-Expert Member
- Aug 27, 2015
- 30,823
- 126,632
Muungano umewachosha kwa kiasi kikubwa sana Wazanzibar.
Hata hayati Abeid Karume aliwahi kusema Muungano ni kama koti hivyo likikubana huna budi kulivua.
Maneno hayo ya kejeli ya Karume kwa Nyerere yalimchafua mno Nyerere na wawili hao hawakuwa na uhusiano mzuri katika siku za mwisho za maisha ya Karume.
Pia Rais wa awamu ya pili ya Zanzibar, ndugu Aboud Jumbe Mwinyi alipohoji kuhusu muundo wa Muungano na kujaribu kuandaa hati za mashtaka kwaajili ya kuuvunja Muungano alijikuta akilazimishwa kujiuzulu nyadhifa zake zote ndani ya chama na serikali na alipojiuzulu tu 1984 akawekwa kizuizini nyumbani kwake Kigamboni mpaka alipofariki mwaka jana.
Akapigika kwa maradhi huko kizuizini hadi kuamua kuandika wosia asizikwe kuserikali japo alikuwa Rais mstaafu alisingizia tu ucha mungu
Hakufunikwa hata na kavendera ka CCN
....

