Makapuku Forum

Makapuku Forum

1996 - Tupac Amar Shakur anafariki Dunia.

Alikuwa ni rapa wa muziki wa Hiphop toka nchini Marekani.

Anachukuliwa kama mmoja kati ya rapa mwenye ushawishi na bora wa wakati wote.

Ni miongoni mwa watu wachache ambao wameendelea kuwa maarufu hata baada ya miaka mingi kupita baada ya vifo vyao kando ya Mwanamapinduzi Ernesto Che Guevara na mwanamuziki wa regge Bob Marley.

Tupac aka Makaveli alifariki baada ya kupigwa risasi kadhaa wiki moja baadae ndio anafariki baada ya kiasi kikubwa sana cha damu kuvuja ndani ya mwili.

Pamoja na yote hayo kuna wanaoamini Tupac hajafa, Alifeki kifo chake ili apunguze kufatiliwa.


Kwa wale wanaoamini kuwa Tupac amefariki wanaamini Big ndio aliyemuua baada ya kutoelewana kisa Tupac alitembea na mwanamke wa Big Notorius aliyitwa Faith Evans.

Pia kuna wanaoamini Tupac aliuwawa na bosi wake na mmiliki wa Death row Inc. ambaye ni Suge Knight.

Baba wa ubatizo wa Tupac alifariki na kuzikwa Tanzania, alijulikana kama Geronimo Pratt.

Leo ni miaka 20 toka 2pac afe bado anabaki kama rapa bora wa wakati wote.

Pumzika amani 2pac.
Apumzike tu maana rumors nazo zinaboa wakati mwingine
 
weka picha mkuu
1473790223330.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom