Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220322-165913_Instagram.jpg
 
Farhan jr

Siku moja wakati nipo field pale Kinondoni Islamic High School, ofcourse nilipewa ENGLISH LANGUAGE 1 & 2 nifundishe Kidato cha tano na sita, nakumbuka ilikuwa siku ya assessment

Nimeingia darasani na Assesor alikuwa nyuma ananitazama tu, Mimi nilikuwa muumini sana wa vitu viwili kwenye ufundishaji wangu, kwanza ni kutoshika kitabu wakati nafundisha pili nilichagua LEARNER CENTRED APPROACH, Wanafunzi wangu wanafahamu hilo

Walimu wenzangu watanielewa vyema naposema Learner centred au Student centred approach, nilikuwa na imani kubwa sana na Wanafunzi wangu na natengeneza material kutoka kwenye vichwa vyao

Hiyo siku Madam alikaa nyuma kabisa nikamkabidhi copy ya notes zangu kisha original nikawa nayo, well nikaanza kipindi changu! Nikifungua notes nilikuwa nachukua hints tu kisha naflow tofauti na kilichomo kwenye notes

Kisha muda mwingi nawauliza Wanafunzi maswali na kukazia majibu yao, ilikuwa hivyo kwa dakika zote 80 za kipindi mpaka Assesment ilivyoisha na baadae Madam akaniita

Kwa haraka akaniambia kila taaluma ina misingi yake na kila Mwanataaluma ana misingi yake au kile anachokiamini (Falsafa) akaniambia wewe unaamini kwenye LEARNER CENTRED iwe hivyo usiache na usibadili kisa Mimi

Kwenye kazi yoyote uwe na kile unachokiamini ndicho alichosema kisha akamaliza kwa kuniambia yeye ni Daktari anafahamu vingi, aligundua imani yangu kwakuwa nilikuwa nafundisha kile ambacho kwenye notes hakipo

Kuanzia pale niliondoka na kile, kuwa na misimamo ya kile nachoamini, nikisema Simba ni bora hata kama ikifungwa sipaswi kubadili badili maneno, sipaswi kuanza Kocha sijui, mara wachezaji, HAPANA ukishasema bora maana yake uliona kila kitu

Habari ni taaluma nzuri sana, wote waliofanikiwa ni wale waliosimama na misimamo yao, Ulaya watu hufa na misimamo yao, ukibadilika unakosa hoja, unapoteza imaani, hujui unachokipigania, Mashujaa sio kwamba hawaogopi kifo bali hawapo tayari kusaliti nafsi zao

Mimi nilisema SIMBA ni bora, nilisema wanakwenda mpaka Nusu fainali hiyo itabaki kuwa hivyo kwakuwa ndio IMAANI yangu
Screenshot_20220322-170023_Instagram.jpg
 
Ni wivu wa familia yetuu ...achana nae
....ila hii ni kweli anko, familia yetu imejaa wivu sana fikiria juzi yule mtoto wa babu kaniona nimenunua toothpick akasema siku hizi nina maringo na ninajifanya myuropa sana. Sikumjibu maana angekuja kunisemea kwenu wajomba zangu nikakosa radi bure kwa kununua toothpick
 
Namafananisha na binamu Obe yaani sijui kwa nini
...huyo sio mzee kama mimi. Mimi ni kijana ila nna mambo ya kizee ndiyo sifa yangu kubwa. Stivu yeye ni mzee ila sijui kama ni msanii wa filamu, vichekesho au muziki. Zaidi nilikuwa namsikia enzi zangu nakwenda Akudo anaimbwa ""stivu nyerenyere tajiri mufupi"''. Usinifanishe naye vinginevyo nitaenda kwenye TV niite wanahabari nikupe masaa 48 ukanushe mfananisho
 
Unafahamu nini kuhusu tiba ya upandikizaji wa uboho? wamesema ni mpya sana kwenye Taifa la Tanzania ambapo sasa imeanza kutolewa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili ambayo sasa inaingia kwenye orodha ya Hospitali chache za Afrika zenye uwezo wa kutoa matibabu haya. View attachment 2160507
...habari nzuri sana hii. Itawasaidia sana wenye matatizo haya
 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Hamza Johari amesema ndege aina ya Embraer 190 (5H-FJH) iliyozuiwa nchini haiwezi kutumika kulipa madeni ya waliokuwa wafanyakazi wa Fastjet Tanzania kwa sababu haikuwa mali ya shirika hilo.

Johari aliyasema hayo baada ya waliokuwa wafanyakazi 105 wa Fastjet Tanzania, kuingiwa hofu iwapo Sh5 bilioni wanazodai shirika hilo zitalipwa, baada ya kile walichodai kuwa ndege hiyo iliyokuwa imezuiwa kama dhamana, imebadilishwa usajili na kuruhisiwa kuondoka.
View attachment 2160523
...duh, shirika hili lilikuwa muhimu sana kipindi hicho na lingekuwepo hadi leo usafiri wa anga ungekuwa rahisi sana
 
Namungo waweka kambi Zambia
.
Kikosi cha wachezaji 24 wa Namungo FC kimetua salama nchini Zambia kwa ajili ya kambi ya wiki mbili kupisha kalenda ya Fifa kwa timu za taifa.
.
Kocha msaidizi wa Namungo, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema wakiwa nchini humo watacheza michezo miwili ya kirafiki ikiwa ni sehemu ya kujiweka fiti kabla ya kurudi kwenye michuano ya Ligi Kuu Bara.

......……..
View attachment 2160540
...mmmmh, hawa ni wachezaji wa kila siku au maveterani kama mimi kwenye chama letu la kila Jumamosi pale viwanja vya Mashababi Kigamboni hospitali? Sababu kwenye chama letu la maveterani sioni kabisa kati ya hawa kunizuia winga teleza kutoa krosi za magoli
 
...huyo sio mzee kama mimi. Mimi ni kijana ila nna mambo ya kizee ndiyo sifa yangu kubwa. Stivu yeye ni mzee ila sijui kama ni msanii wa filamu, vichekesho au muziki. Zaidi nilikuwa namsikia enzi zangu nakwenda Akudo anaimbwa ""stivu nyerenyere tajiri mufupi"''. Usinifanishe naye vinginevyo nitaenda kwenye TV niite wanahabari nikupe masaa 48 ukanushe mfananisho
 
Eeenh auntie ana wasiwasi naye yaani issue ya week iliyopita nakumbushiwa leo jamani ujue auntie stress za mapenzi sitaki kabisa jamani nataka rahaa tu mimi rahaa tu yaani nataka kudekezwa jamaniiii
Mapenzi ya kweli na Wivu havitengamani Auntie...
Binafsi namuelewa sana Shem wangu..Msamehe tu Aunty akeee..

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom