

Farhan jr
Siku moja wakati nipo field pale Kinondoni Islamic High School, ofcourse nilipewa ENGLISH LANGUAGE 1 & 2 nifundishe Kidato cha tano na sita, nakumbuka ilikuwa siku ya assessment
Nimeingia darasani na Assesor alikuwa nyuma ananitazama tu, Mimi nilikuwa muumini sana wa vitu viwili kwenye ufundishaji wangu, kwanza ni kutoshika kitabu wakati nafundisha pili nilichagua LEARNER CENTRED APPROACH, Wanafunzi wangu wanafahamu hilo
Walimu wenzangu watanielewa vyema naposema Learner centred au Student centred approach, nilikuwa na imani kubwa sana na Wanafunzi wangu na natengeneza material kutoka kwenye vichwa vyao
Hiyo siku Madam alikaa nyuma kabisa nikamkabidhi copy ya notes zangu kisha original nikawa nayo, well nikaanza kipindi changu! Nikifungua notes nilikuwa nachukua hints tu kisha naflow tofauti na kilichomo kwenye notes
Kisha muda mwingi nawauliza Wanafunzi maswali na kukazia majibu yao, ilikuwa hivyo kwa dakika zote 80 za kipindi mpaka Assesment ilivyoisha na baadae Madam akaniita
Kwa haraka akaniambia kila taaluma ina misingi yake na kila Mwanataaluma ana misingi yake au kile anachokiamini (Falsafa) akaniambia wewe unaamini kwenye LEARNER CENTRED iwe hivyo usiache na usibadili kisa Mimi
Kwenye kazi yoyote uwe na kile unachokiamini ndicho alichosema kisha akamaliza kwa kuniambia yeye ni Daktari anafahamu vingi, aligundua imani yangu kwakuwa nilikuwa nafundisha kile ambacho kwenye notes hakipo
Kuanzia pale niliondoka na kile, kuwa na misimamo ya kile nachoamini, nikisema Simba ni bora hata kama ikifungwa sipaswi kubadili badili maneno, sipaswi kuanza Kocha sijui, mara wachezaji, HAPANA ukishasema bora maana yake uliona kila kitu
Habari ni taaluma nzuri sana, wote waliofanikiwa ni wale waliosimama na misimamo yao, Ulaya watu hufa na misimamo yao, ukibadilika unakosa hoja, unapoteza imaani, hujui unachokipigania, Mashujaa sio kwamba hawaogopi kifo bali hawapo tayari kusaliti nafsi zao
Mimi nilisema SIMBA ni bora, nilisema wanakwenda mpaka Nusu fainali hiyo itabaki kuwa hivyo kwakuwa ndio IMAANI yangu