Makapuku Forum

Makapuku Forum

MABOSI wa Newcastle United wameamua kuonyesha jeuri ya pesa kwa kuamua kujitosa kwenye dili la kuiwania saini ya staa wa PSG na Brazil, Neymar ambaye amekuwa akiwindwa na Manchester City na Barcelona.
Neymar anaonekana kuwa na wakati mgumu kwenye viunga vya PSG na taarifa zinadai ameomba kuondoka mwisho wa msimu huu. Mkataba wake unatakiwa kumalizika 2025.

Screenshot_20220322-161921_Instagram.jpg
 
BEKI wa kulia wa Yanga, Djuma Shabani amewachongea John Bocco na Chris Mugalu wa Simba pamoja na Heritier Makambo baada ya kufunga bao lake la pili katika Ligi Kuu Bara wakati Yanga ikiizamisha KMC kwa mabao 2-0, huku akisema kwake kufunga ni kazi rahisi kuliko ya kukaba, hivyo akipata nafasi atafunga sana tu.

Djuma alifunga bao lake la kwanza msimu huu Novemba 2 mwaka jana kwa mkwaju wa penalti katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Ruvu Shooting, huku kina Makambo, Mugalu na Bocco wakisota hadi sasa kutapa angalau bao moja katika ligi hiyo iliyopo raundi ya 18.
Beki huyo kutoka DR Congo aliliambia Mwanaspoti kuwa, ataendelea kufunga sana mabao kila anapopata nafasi ili kutimiza malengo ya timu yake katika malengo ya kutwaa ubingwa wa ligi msimu huu huku akitaja kuwa majukumu yanambana kutupia mara kwa mara.


Screenshot_20220322-162036_Instagram.jpg
 
SIMBA juzi ilipoteza mechi yake ya pili katika Kundi D la Kombe la Shirikisho Afrika kwa kufungwa na Asec Mimosas na sasa imesalia na dakika 90 za maajabu Dar.
Wawakilishi hao wa Tanzania ilifungwa mabao 3-0 mjini Cotonou, Benin na kuifanya isalie na pointi saba na sasa italazimika kushinda mechi ya mwisho ya Aprili 3 dhidi ya USGN ya Niger iliyolazimisha sare ya 2-2 nyumbani na RS Berkane ya Morocco mjini Niamey.

Simba ikishinda mchezo huo itafikisha pointi 10 na kuungana na moja kati ya Berkane au Asec zitakazovaana katika mechi ya mwisho ili kutinga robo fainali ya michuano hiyo ya Shirikisho na kuandika historia mpya.
Screenshot_20220322-162300_Instagram.jpg
 
AIR MANULA NDANI KIKOSI BORA CHA WIKI CAF CC
.
1. Aishi Manula (Simba)
2. Kouassi Attohoula (Asec Mimosas)
3. Hamza El Moussaoui (Berkane)
4. Sanad Al Werfalli (Al-Ittihad)
5. Ahmed El Trbi (Al-Ahli Tripoli)
6. Boyd Musonda (Zanaco)
7. Ghazi Ayadi (Al-Ittihad)
8. Christian Koffi (TP Mazembe)
9. Thabiso Mokenkoane (Royal Leopards)
10. Stephane Aziz Ki (Asec Mikosas)
11. Anas Al Musrati (Al-Ittihad)

Screenshot_20220322-162419_Instagram.jpg
 
Namungo waweka kambi Zambia
.
Kikosi cha wachezaji 24 wa Namungo FC kimetua salama nchini Zambia kwa ajili ya kambi ya wiki mbili kupisha kalenda ya Fifa kwa timu za taifa.
.
Kocha msaidizi wa Namungo, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema wakiwa nchini humo watacheza michezo miwili ya kirafiki ikiwa ni sehemu ya kujiweka fiti kabla ya kurudi kwenye michuano ya Ligi Kuu Bara.

......……..
Screenshot_20220322-162525_Instagram.jpg
 
OPAH AANZA NA HAT-TRICK
.
Mshambuliaji wa Simba Queens,Opah Clement Sanga (21) akiwa kwenye majaribio ya mwezi mmoja nchini Uturuki kwenye klabu ya Ikater kayser ameanza vyema baada ya hapo jana kufanikiwa kutupia goli 3 kwenye ushindi wa mabao 4-1 walioupata dhidi ya Ikabur Diame.
.
Endapo Opah atakidhi viwango wanavyohitaji basi atasajiliwa moja wa moja kwenye klabu hiyo.
Screenshot_20220322-162707_Instagram.jpg
 
EDO: ADEBAYOR ASIPOBANWA NI MSIBA KWA MKAPA
.
“Gendermarie wanaonekana kuwa bora katika ufungaji hasa kwa kupitia kwa mshambuliaji wao anayeitwa ADEBAYOR. Inawezekana yeye ndiye ambaye anaweza kuamua mechi Uwanja wa Mkapa. Akibanwa vyema basi Simba itapita. Asipobanwa vyema tunaweza kuwa na MSIBA mwingine kama ilivyotokea katika mechi dhidi ya UD Songo au Jwaneng Galaxy ya Botswana.
.
Mara nyingi tuna kumbukumbu nyingi nzuri za Simba dhidi ya wakubwa kama Al Ahly, AS Vita, JS Saoura na wengineo katika Uwanja wa Mkapa. Hata hivyo, huwa tunaamua kusahau kumbukumbu hizi mbaya ambazo zaidi zilikuwa mechi za kufa na kupona kwa Simba. Tuchague kumbukumbu hizi mbaya kwa ajili ya kuwakumbusha Simba kazi ambayo inawakabili mbele yao.
.
Hawa wote wawili walionekana kuwa vibonde kwa Simba na kama vile wangekufa nyingi Uwanja wa Mkapa, lakini hadithi ikawa tofauti.” Edo Kumwembe [via Mwanaspoti]
.
WANASIMBA mnasemaje __!!
Screenshot_20220322-162845_Instagram.jpg
 
DYBALA KUSEPA JUVE BURE !!
.
Mazungumzo ya kusaini mkataba mpya baina ya wawakilishi wa Juventus na staa wao kutoka Argentina, Paulo Dybala, 28, yameshindwa kufikia muafaka na mchezaji huyu anaonekana kuwa na nafasi kubwa ya kuondoka kwenye viunga hivyo katika dirisha lijalo la usajili wa majira ya kiangazi.
.
Dybala amekuwa akiwindwa na timu nyingi barani Ulaya ikiwa ni pamoja na Manchester United ambao wamekuwa wakimsaka tangu dirisha lililopita la usajili.
Screenshot_20220322-163002_Instagram.jpg
 
YANGA MWENDO MTAMU
.
Yanga haijaruhusu bao katika mechi 8 zilizopita za Ligi Kuu huku wababe hao wa Jangwani wakifunga jumla ya mabao 15 katika mechi hizo.
.
Mara ya mwisho kuruhusu bao ilishinda 2-1 dhidi ya Biashara Desemba 26, 2021.
Screenshot_20220322-163816_Instagram.jpg
 
RUDIGER KUTIMKIA JUVE
.
Imethibitika kuwa beki kisiki wa Chelsea, Antonio Rudiger atajiunga na Juventus katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi kwa mkataba wa miaka minne wenye mshahara mnono Pauni 5.4 milioni kila msimu.
.
Rudiger ambaye mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwisho wa msimu huu ataondoka Chelsea kwa sababu wababe hao hawana ruhusa yakumsainisha mkataba mpya kutokana na zuio la mali za mmiliki wao Roman Abramovich.
.
Mbali ya zuio la Abramovic, Chelsea ilijaribu kumpa Ridiger ofa ya kusaini mkataba mpya lakini fundi huyo alikataa kwa sababu alihitaji mshahara mkubwa zaidi uliokuwa kwenye mkataba.
Screenshot_20220322-164035_Instagram.jpg
 
Kutokana na sheria za Shirikisho la soka nchini Uingereza, Kinda Conor Gallagher hatoweza kucheza mechi ya nusu fainali ya FA dhidi ya Chelsea kwakuwa yupo kwa mkopo Palace akitokea klabu hiyo ya Chelsea

Ikumbukwe kuwa Galagher hakucheza michezo yote ya EPL dhidi ya Chelsea msimu huu kwakuwa ni Mchezaji wao na yupo kwa mkopo tu Palace
Screenshot_20220322-164304_Instagram.jpg
 
Kipa wa Ajax FC Andre Onana amepata ajali ya gari alipokuwa njiani akielekea kujiunga na kambi ya timu ya taifa Cameroon kwa ajili ya mechi dhidi ya Algeria ya kuwania kufuzu kombe la Dunia 2022 nchini Qatar.
Screenshot_20220322-164755_Instagram.jpg
 
When football meets fashion

Pichani ni wachezaji wa Chelsea, Romelu Lukaku na Hakim Ziyech wakiwa nchini Marekani kushuhudia mchezo wa mpira wa kikapu
Screenshot_20220322-164852_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Bado tupo kwenye tafakuri ilikuwaje Edouard Mendy wa Chelsea alikosa tuzo ya YASHIN mbele ya Gigi Donnarouma, bado haiingii akilini
Screenshot_20220322-165015_Instagram.jpg
 
Anaetoa pass hapo kati ni Manuel Neur, ni Kipa wa Bayern Munich, tazama nyuma yake na mbele yake, hii ndio maana ya Sweeper

Moja kati ya Makipa wenye matumizi sahihi sana ya miguu yao na akili
Screenshot_20220322-165326_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom